Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 5/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu na Kuteseka?
    Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu na Kuteseka?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?
    Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?
  • Kwa Nini Kuna Mateso Mengi Ulimwenguni?
    Biblia Inatufundisha Nini?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 5/1 uku. 16

MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA

Ni nani hasa anayeutawala ulimwengu?

Picha za vita, uhalifu, jeuri, na misiba

Kama Mungu ndiye anayetawala ulimwengu huu, hakungekuwa na matatizo mengi hivi

Watu wengi wanaamini kwamba Mungu wa kweli ndiye anayetawala ulimwengu huu. Lakini kama Mungu ndiye anayetawala, je, ulimwengu ungekuwa na matatizo mengi hivi? (Kumbukumbu la Torati 32:4, 5) Kulingana na Biblia, ulimwengu unaongozwa na kiumbe fulani mwovu.​—Soma 1 Yohana 5:19.

Ilikuwaje mpaka kiumbe mwovu akaanza kuwatawala wanadamu? Mwanzoni mwa historia ya wanadamu, malaika fulani alimwasi Mungu na akawashawishi wanadamu wawili wa kwanza waasi pia. (Mwanzo 3:1-6) Wanadamu hao waliamua kumtii malaika huyo mwasi, Shetani, na hivyo kukubali awe mtawala wao. Mungu Mweza-Yote ndiye Mtawala anayestahili, lakini anataka watu wakubali utawala wake kwa hiari. (Kumbukumbu la Torati 6:6; 30:16, 19) Kwa kusikitisha, wanadamu wengi wamepotoshwa na kufanya uamuzi mbaya kama ule wa wanadamu wawili wa kwanza.​—Soma Ufunuo 12:9.

Ni nani atakayetatua matatizo yanayowapata wanadamu?

Je, Mungu ataruhusu utawala mwovu wa Shetani uendelee? Hapana! Mungu atamtumia Yesu kuondoa uovu ambao umesababishwa na Shetani.​—Soma 1 Yohana 3:8.

Yesu atatumia mamlaka aliyopewa na Mungu kumwangamiza Shetani. (Waroma 16:20) Kisha, Mungu atawatawala wanadamu na kuwarudishia maisha yenye furaha na amani kama alivyokusudia mwanzoni.​—Soma Ufunuo 21:3-5.

Kwa habari zaidi ona sura ya 3 ya kitabu hiki,Biblia inafundisha nini hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Pia, kinapatikana kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki