-
Kuwasiliana na PepoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Wasifanye nini? Inaonekana amewazuia wasichukue miili yenye nyama wanayoweza kutumia kufanya ngono na wanawake, kama walivyokuwa wamefanya kabla ya Gharika. Biblia inasema kwamba malaika waaminifu, wakiwa wajumbe wa Mungu, walivaa miili ya wanadamu katika kufanya kazi zao hapa duniani mpaka karne ya kwanza W.K. Lakini baada ya Gharika, malaika hao waliokuwa wamezitumia vibaya zawadi zao walinyang’anywa uwezo wa kuvaa miili ya wanadamu.
Hata hivyo, ni jambo lenye kupendeza kwamba inaonekana roho waovu wanaweza kuwafanya wanadamu waone maono, na yale wanayoona huenda yakaonekana kuwa ya kweli. Ibilisi alipomshawishi Yesu, inaonekana alitumia njia hizo ili amwonyeshe Yesu “falme zote za ulimwengu na utukufu wazo.”—Mt. 4:8.
Mtu anawezaje kuepuka uvutano wa pepo?
Met. 18:10: “Jina la Yehova ni mnara wenye nguvu. Mwadilifu hukimbilia humo na kupewa ulinzi.” (Hilo halimaanishi kwamba kutumia jina la Mungu ni hirizi ya kufukuza uovu. “Jina” la Yehova linamwakilisha yeye mwenyewe. Sisi tunapewa ulinzi tunapopata kumjua na kumtegemea kikamili, kujitiisha chini ya mamlaka yake na kutii amri zake. Tukifanya hivyo, na tukimwomba atupe msaada, na kutumia jina lake, atatupa ulinzi ambao ameahidi katika Neno lake.)
Mt. 6:9-13: “Basi, ninyi msali hivi: ‘ . . . Usituingize katika jaribu, bali utukomboe kutokana na yule mwovu.’” Unapaswa pia ‘kudumu katika sala.’ (Rom. 12:12) (Mungu husikia sala hizo kutoka kwa wale wanaotamani kikweli kuijua kweli na kumwabudu yeye kwa njia inayompendeza.)
1 Kor. 10:21: “Hamwezi kuwa mkishiriki ‘meza ya Yehova’ na meza ya roho waovu.” (Wale wanaotaka urafiki na ulinzi wa Yehova lazima waache kabisa kushiriki katika mikutano ya kuwasiliana na pepo. Kupatana na mfano ulioandikwa katika Matendo 19:19, pia ni muhimu mtu kuviharibu au kuviondoa kwa njia inayofaa vitu vyote vinavyohusiana na kuwasiliana na pepo.)
Yak. 4:7: “Basi, jitiisheni kwa Mungu; lakini mpingeni Ibilisi, naye atawakimbia ninyi.” (Ili kufanya hivyo, jifunze kwa bidii mapenzi ya Mungu na kuyafuata katika maisha yako. Huku upendo wa Mungu ukikuimarisha usiwaogope wanadamu, kataa kabisa kushiriki katika desturi zozote zinazohusiana na kuwasiliana na pepo au kutii sheria zozote za mtu mwenye kuwasiliana na pepo.)
Vaa “mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu” ambayo yanafafanuliwa katika Waefeso 6:10-18 na uwe na bidii katika kuyadumisha yote katika hali nzuri.
-
-
Kuzaliwa Mara ya PiliKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kuzaliwa Mara ya Pili
Maana: Kuzaliwa mara ya pili kunahusisha kubatizwa katika maji (‘kuzaliwa kwa maji’) na kuzaliwa kwa roho ya Mungu, kwa njia hiyo kuwa mwana wa Mungu mwenye tumaini la kutawala katika Ufalme wa Mungu. (Yoh. 3:3-5) Yesu alizaliwa mara ya pili, hali kadhalika wale 144,000 walio warithi pamoja naye wa Ufalme wa mbinguni.
Kwa nini ni lazima Wakristo fulani ‘wazaliwe mara ya pili’?
Mungu amekusudia kushirikisha wanadamu wachache waaminifu watawale pamoja na Yesu Kristo katika Ufalme wa mbinguni
Luka 12:32: “Msiogope, kundi dogo, kwa sababu Baba yenu amekubali kuwapa ninyi ufalme.”
Ufu. 14:1-3: “Nikaona, na, tazama! Mwana-Kondoo [Yesu Kristo] amesimama juu ya Mlima Sayuni, na pamoja naye 144,000 . . . ambao wamenunuliwa kutoka duniani.” (Ona ukurasa wa 202, 203, chini ya kichwa, “Mbingu.”)
Wanadamu hawawezi kwenda mbinguni wakiwa na miili ya nyama na damu
1 Kor. 15:50: “Hili nasema, akina ndugu, kwamba nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala uharibifu haurithi kutoweza kuharibika.”
Yoh. 3:6: “Kile ambacho kimezaliwa kwa mwili ni mwili, na kile ambacho kimezaliwa kwa roho ni roho.”
Ni wale tu ambao ‘wamezaliwa mara ya pili,’ na kuwa wana wa Mungu, ndio wanaoweza kutawala katika Ufalme wa mbinguni
Yoh. 1:12, 13: “Wengi kadiri ileile waliompokea [Yesu Kristo], aliwapa mamlaka ya kuwa watoto wa Mungu, kwa
-