-
Kuwasiliana na PepoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
na kuwasiliana na pepo au kutii sheria zozote za mtu mwenye kuwasiliana na pepo.)
Vaa “mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu” ambayo yanafafanuliwa katika Waefeso 6:10-18 na uwe na bidii katika kuyadumisha yote katika hali nzuri.
-
-
Kuzaliwa Mara ya PiliKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kuzaliwa Mara ya Pili
Maana: Kuzaliwa mara ya pili kunahusisha kubatizwa katika maji (‘kuzaliwa kwa maji’) na kuzaliwa kwa roho ya Mungu, kwa njia hiyo kuwa mwana wa Mungu mwenye tumaini la kutawala katika Ufalme wa Mungu. (Yoh. 3:3-5) Yesu alizaliwa mara ya pili, hali kadhalika wale 144,000 walio warithi pamoja naye wa Ufalme wa mbinguni.
Kwa nini ni lazima Wakristo fulani ‘wazaliwe mara ya pili’?
Mungu amekusudia kushirikisha wanadamu wachache waaminifu watawale pamoja na Yesu Kristo katika Ufalme wa mbinguni
Luka 12:32: “Msiogope, kundi dogo, kwa sababu Baba yenu amekubali kuwapa ninyi ufalme.”
Ufu. 14:1-3: “Nikaona, na, tazama! Mwana-Kondoo [Yesu Kristo] amesimama juu ya Mlima Sayuni, na pamoja naye 144,000 . . . ambao wamenunuliwa kutoka duniani.” (Ona ukurasa wa 202, 203, chini ya kichwa, “Mbingu.”)
Wanadamu hawawezi kwenda mbinguni wakiwa na miili ya nyama na damu
1 Kor. 15:50: “Hili nasema, akina ndugu, kwamba nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala uharibifu haurithi kutoweza kuharibika.”
Yoh. 3:6: “Kile ambacho kimezaliwa kwa mwili ni mwili, na kile ambacho kimezaliwa kwa roho ni roho.”
Ni wale tu ambao ‘wamezaliwa mara ya pili,’ na kuwa wana wa Mungu, ndio wanaoweza kutawala katika Ufalme wa mbinguni
Yoh. 1:12, 13: “Wengi kadiri ileile waliompokea [Yesu Kristo], aliwapa mamlaka ya kuwa watoto wa Mungu, kwa
-