-
Kuzaliwa Mara ya PiliKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
inatuonya sisi sote tusiwe na uhakika mno kuhusu tumaini letu. Tunahitaji kuendelea kujichunguza ili kuhakikisha kwamba kwa kweli tunafanya yale ambayo Mungu na Kristo wanataka tufanye. (1 Kor. 10:12)’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Yesu aliwapa wanafunzi wake wa kweli jukumu gani? (Mt. 28:19, 20; 1 Kor. 9:16)’
-
-
Kuzaliwa Upya Katika Mwili MwingineKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kuzaliwa Upya Katika Mwili Mwingine
Maana: Imani ya kwamba mtu huzaliwa tena katika mwili mwingine au mfululizo wa miili, ambayo inaweza kuwa ya mwanadamu au mnyama. Kwa kawaida, inaaminiwa kwamba “nafsi” isiyoonekana ndiyo inayozaliwa upya katika mwili mwingine. Hilo si fundisho la Biblia.
Mtu anapohisi kwamba anawajua watu ambao hajawahi kukutana nao au kwamba anajua mahali ambapo hajawahi kuwa, je, hilo linathibitisha kwamba watu huzaliwa upya katika mwili mwingine?
Je, umewahi kukutana na mwanamume au mwanamke, na kufikiri kimakosa kwamba ni mwingine aliye hai pia? Wengi wamefanya hivyo. Kwa nini? Kwa sababu watu fulani wana mazoea yanayofanana na ya wengine au huenda hata wakawa na sura inayofanana sana. Kwa hiyo, hisia ya kwamba unamjua mtu hata ikiwa hujawahi kukutana naye wakati uliopita kwa kweli haithibitishi kwamba ulimjua katika maisha mengine, sivyo?
Kwa nini huenda ukaona kwamba unatambua nyumba au mji fulani hata ingawa hujapata kuwa mahali hapo? Je, ni kwa sababu uliishi hapo wakati wa maisha ya zamani? Nyumba nyingi hujengwa kulingana na michoro inayofanana. Fanicha zinazotumiwa katika majiji yaliyo mbali huenda zikafanyizwa kulingana na vielelezo vinavyofanana. Na je, si kweli kwamba maumbo fulani ya nchi hufanana sana na yale yaliyo katika sehemu nyingine za mbali sana? Kwa hiyo, inaeleweka ni kwa nini mtu anaweza kuwa na hisia hizo, na si lazima azaliwe upya katika mwili mwingine ndipo ahisi hivyo.
-