Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutounga Mkono Upande Wowote
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kuhusu sherehe za kizalendo, historia ya kilimwengu inasema nini juu ya maoni ya wale wanaoitwa Wakristo wa kwanza?

      “Wakristo walikataa . . . kumtolea dhabihu shujaa maliki—leo ni kama kukataa kusalimu bendera au kukariri maneno ya kiapo cha utii. . . . Ni Wakristo wachache sana waliokariri maneno hayo, ijapokuwa kwa kawaida madhabahu yenye moto unaowaka iliwekwa katika uwanja wa michezo ili waweze kuitumia. Jambo ambalo mfungwa alihitajiwa kufanya ni kutawanya uvumba kidogo juu ya mwali wa moto naye alipewa Cheti cha Dhabihu na kuachiliwa huru. Pia alielezwa waziwazi kwamba yeye hakuwa akimwabudu maliki; kwamba alikuwa akikubali tu uungu wa maliki akiwa kiongozi wa serikali ya Roma. Hata hivyo, karibu Wakristo wote hawakukubali nafasi hiyo ya kuachiliwa huru.”—Those About to Die (New York, 1958), D. P. Mannix, uku. 135, 137.

      “Tendo la kumwabudu maliki lilihusisha kunyunyiza uvumba kidogo au matone machache ya divai juu ya madhabahu iliyosimama mbele ya sanamu ya maliki. Labda kwa kuwa sasa mambo hayo ni ya zamani kwetu, tunaona kwamba tendo hilo kuwa sawa na . . . kuinua tu mkono ili kusalimu bendera au mtawala mashuhuri wa serikali, ili kuonyesha heshima, staha na uzalendo. Huenda watu wengi sana katika karne ya kwanza walikuwa na maoni hayohayo, lakini Wakristo hawakuwa na maoni hayo. Kwa ujumla waliliona jambo hilo kuwa la ibada ya kidini, kumkiri maliki kuwa mungu, na kwa hiyo kukosa kuwa washikamanifu kwa Mungu na Kristo, nao walikataa kufanya hivyo.”—The Beginnings of the Christian Religion (New Haven, Conn.; 1958), M. F. Eller, uku. 208, 209.

      Wakristo wanapokataa kuunga mkono upande wowote, je, inamaanisha kwamba wao hawawajali jirani zao?

      Bila shaka sivyo. Wao wanajua na wanajitahidi sana kufuata amri hii ambayo Yesu aliirudia: “Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe.” (Mt. 22:39) Pia wanafuata lile shauri lililoandikwa na mtume Paulo: “Tuwatendee wote mema, na hasa wale ambao katika imani ni jamaa zetu.” (Gal. 6:10) Wanasadiki kwamba wema ulio mkuu zaidi wanaoweza kuwatendea jirani zao ni kuwatangazia habari njema za Ufalme wa Mungu, ambao utatatua milele matatizo yanayowakabili wanadamu na ambao huwapa wale wanaoukubali tarajio zuri ajabu la uzima wa milele.

  • Kuwasiliana na Pepo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kuwasiliana na Pepo

      Maana: Imani ya kwamba sehemu ya roho ya wanadamu huendelea kuishi baada ya mwili kufa nayo inaweza kuwasiliana na watu walio hai, kwa kawaida inafanya hivyo kupitia mtu anayepitisha habari hizo. Watu fulani huamini kwamba kila kitu chenye mwili na matukio yote ya asili yana roho ndani yake. Ulozi ni kutumia nguvu ambazo inakubaliwa kwamba zinatoka kwa roho waovu. Namna zote za kuwasiliana na pepo zinashutumiwa katika Biblia.

      Je, kweli mwanadamu anaweza kuwasiliana na “roho” ya mpendwa aliyekufa?

      Mhu. 9:5, 6, 10: “Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe . . . Pia, upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari zimepotea, na mpaka wakati usio na kipimo hawana fungu lolote tena katika chochote ambacho kitafanywa chini ya jua. Yote ambayo mkono wako unapata kufanya, yafanye kwa nguvu zako zote, kwa maana hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi, mahali unapokwenda.”

      Eze. 18:4, 20: “Nafsi inayotenda dhambi—hiyo yenyewe itakufa.” (Kwa hiyo, nafsi si kitu fulani kinachoendelea kuishi baada ya mwili kufa na ambacho wanadamu walio hai wanaweza kuwasiliana nacho baada ya hapo.)

      Zab. 146:4: “Roho yake hutoka, naye hurudi kwenye udongo wake; siku hiyo mawazo yake hupotea.” (Roho inaposemwa kuwa ‘inatoka’ katika mwili, hiyo ni njia nyingine tu ya kusema kwamba nguvu za uhai zimeacha kutenda. Kwa hiyo, baada ya mtu kufa, roho yake haiendelei kuishi ikiwa kitu kisicho na mwili ambacho kinaweza kufikiri na kutimiza mambo kikiwa nje ya mwili. Roho hiyo si kitu ambacho walio hai wanaweza kuwasiliana nacho baada ya mtu kufa.)

      Ona pia ukurasa wa 102-104, chini ya kichwa, “Kifo.”

      Je, Biblia haisemi kwamba Mfalme Sauli aliwasiliana na nabii Samweli baada ya Samweli kufa?

      Simulizi hilo linapatikana katika 1 Samweli 28:3-20. Mstari wa 13 na 14 huonyesha kwamba Sauli mwenyewe hakumwona Samweli bali alikisia tu kutokana na ufafanuzi aliopewa na yule mwanamke mwenye kuwasiliana na pepo akisema kwamba

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki