-
Sisi Tutamlipaje Yehova Marudishio?Mnara wa Mlinzi—1988 | Desemba 1
-
-
Sisi Tutamlipaje Yehova Marudishio?
WAKATI mtu fulani anapoonyesha upendezi halisi, ulio mchangamfu katika sisi, labda kwa kufanya jambo fulani kwa manufaa yetu, sisi huitikia jinsi gani? Kwa kawaida fadhili na ukarimu hutokeza jibizo fulani, sivyo? Basi, je! hisia zetu ni nini kuelekea Mungu wetu, Yehova, kwa ajili ya fadhili-upendo anazotuelekezea sisi daima?
Ni rahisi sana kuchukua unufaishi wa Yehova kivivihivi tu, nyakati nyingine hata kutenda kama kwamba hatuna shukrani za kweli hata kidogo, kwa sababu ya kuharakishwa-harakishwa na mikazo ya maisha ya kila siku. Kwa hiyo, ingefaa tutue kidogo na kufikiria swali hili la mtunga zaburi: “Mimi nitamlipa Yehova jinsi gani kwa manufaa zote alizonipa mimi?” (Zaburi 116:12, NW) Sisi tutajibiza kwa njia gani mbalimbali?
Manufaa Kutoka kwa Yehova
Bila zawadi ya Yehova ya Neno lake Biblia, sisi hatungejua la kufanya! Wanaume na wanawake mashujaa katika kame zilizopita walijasirisha uhai wao ili wawe na kitabu hicho na kukisoma, na sisi tumekua tukaja kuelewa ni kwa nini. Watu wa Mungu wamekuwa wenye shukrani sikuzote kwa ajili ya Andiko lililovuviwa, wakijua jinsi lilivyo lenye manufaa “kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu.”—2 Timotheo 3:16, NW.
Hata hivyo, sisi tunajua kwamba ili tuwe “tayari kabisa kwa kila kazi njema,” tunahitaji kitu ambacho ni zaidi ya kuwa na maarifa ya kichwani tu juu ya Biblia. (2 Timotheo 3:17, NW) Ni kupitia uwezo wa roho takatifu ya Mungu kwamba manufaa inaletwa kwenye maisha zetu, na uhakika huo unaletwa kwenye fikira zetu na semi za Yehova zenye uvutio kupitia Isaya mnabii wake: “Na sasa Bwana Mungu [Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, AW] amenituma, na roho yake. Bwana [Yehova, NW], mkombozi wako, mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. Laiti ungalisikiliza amri zangu! ndipo amani yako ingalikuwa kama mto wa maji, na haki [uadilifu, NW] yako kama mawimbi ya bahari.” (Isaya 48:1618) Kwa roho takatifu yake, kwa kupatana na Neno lake, Yehova hutuelekeza sisi tujinufaishe wenyewe, na tokeo ni amani na uadilifu.
Zaidi ya hilo, kani ya utendaji ya Yehova hufanya kazi kwa matokeo mazuri ili tupate manufaa kwa sababu kumeanzishwa muundo fulani, tengenezo la kidunia, ambao kupitia huo roho takatifu hutenda kazi. Kwenye 1 Wakorintho sura ya 12, Paulo anafananisha kundi la Kikristo na mwili na kutaarifu hivi katika mstari wa 7, AW; “Lakini udhihirisho wa roho hupewa kwa kila mmoja kwa kusudi lenye manufaa.” Yeye anaendelea kuonyesha jinsi sisi tunavyonufaika kutokana na kuwa sehemu ya tengenezo la Mungu la kidunia.
Miaka mitano hivi baada ya yeye kuandika maneno hayo, aliliandikia kundi la Efeso barua yake ambamo alipanua zaidi juu ya manufaa zinazokamatana na mpango huo wa kidunia. Ingawa aliyosema yalitumika kwanza kwa Wakristo wapakwa-mafuta, je! wale walio wa “umati mkubwa” leo pia ‘hawarekebishwi upya kwa ajili ya kazi ya kihuduma,’ wakiwa ‘watu waliokua kwa ukamili’ kiroho, waliothibitika katika imani, ‘si watoto wachanga tena,’ na ‘kwa upendo wakikua katika mambo yote ndani ya huyo aliye kichwa, Kristo’? (Ufunuo 7:9; Waefeso 4:12-16) Sisi sote tuna sababu njema ya kuwa wenye shukrani.
Mwenye kutambulishwa pamoja na kundi akili, ambaye kazi yake, ya kutulisha kiroho, ni ithibati nyingine bado ya kwamba Yehova anatunufaisha. (Mathayo 24:45, 46) Sisi ndio hawa sasa tukiwa katika wakati uliotabiriwa wa kuwapo kwa Bwana Mkubwa. Je! “mtumwa” anafanya kazi yake? Ijapokuwa hizi “siku za mwisho” zina gizagiza kwa kukosa matumaini, je! sisi tumejawa na tumaini? Je! sisi tuna kusudi lenye ustahiki maishani? (2 Timotheo 3:1-5; Warumi 5:5; 1 Timotheo 4:10) Ndiyo! Na tumaini letu si uyamkini tu bali ni usadiki hakika uliojengwa juu ya imani, ambayo nayo msingi wayo ni ithibati iliyo imara sana.—Waebrania 11:1.
Basi, ni dhahiri kwamba Yehova, Mnufaishi Mkuu wetu, ametupa vitu vingi sana vya kutolea shukrani. Kwa kufaa swali hili linafuata:
Mimi Nitamlipa Yehova Marudishio Gani?
Kwanza, ni lazima sisi tukiri kwamba Yehova hahitaji kitu chochote kutoka kwetu. Yeye ndiye mwenye kusema, “Fedha ni mali yangu, na dhahabu ni mali yangu,” na ndivyo “kila hayawani ni wangu, na makundi juu ya milima elfu.” (Hagai 2:8; Zaburi 50:10; Ayubu 41:11) Hiyo inamaanisha sisi hatuwezi kwa njia yoyote ‘kununua’ upendeleo wa Yehova; hata hivyo tunatiwa moyo tumfanyie matoleo ya kujitakia wenyewe. (Linganisha 1 Nyakati 29:14.) Hata hivyo, kuna masharti fulani ya kuruhusiwa kwetu tutolee Yehova zawadi mbalimbali.
“Nimkaribie Bwana [Yehova, NW] na kitu gani, na kuinama mbele za Mungu aliye juu? Je! nimkaribie na sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka mmoja? Je! Bwana [Yehova, NW] atapendezwa na elfu za kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je! nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu, mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho [nafsi, NW] yangu? Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na Bwana [Yehova, NW] anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!”—Mika 6:6-8.
Sisi tunajifunza kutokana na hilo kwamba sikuzote matakwa ya Yehova ni ya kiasi kinachofaa, sikuzote yanafikilika. Kwa kuongezea, Yesu alionyesha takwa la kimbele kwamba ni lazima uhusiano wetu pamoja na Yehova na pia mwanadamu mwenzetu uwe sawa ili matoleo yetu yakubalike. (Mathayo 5:23, 24) Baada ya kuweka msingi unaofaa, sasa sisi tunaweza kuona kwamba sote tuna kitu cha kumpa Yehova, kwa kuthamini wema wake kwetu.
Tunaweza Kutumiaje Tulicho Nacho?
Hiyo huchukua wakati, jitihada, na kwa kadiri fulani pesa, lakini ni pendeleo kama nini kuwakilisha Yehova katika kazi ya kuhubiri! Dhabihu hiyo ya sifa ni kitu ambacho sisi sote tunaweza kumpa Yehova. Mzee mmoja ambaye ni painia mwenye watoto wadogo watatu anahisi hivi juu ya jambo hilo:
“Kushiriki katika pendeleo la utumishi wa wakati wote kunastahiki dhabihu yoyote ya kibinafsi—hata mengi zaidi—kwa sababu hiyo ndiyo njia yenye matokeo zaidi ya kumpa sifa Baba yetu wa kimbingu. Pia, kwa kadiri fulani inaniwezesha kumtolea yeye asante kwa ajili ya fadhili zisizostahiliwa alizonionyesha mimi binafsi.”
Mke wake anaongeza hivi: “Ni pendeleo halisi kusaidia mume wangu kupainia. Hiyo inawezesha jamaa nzima kuwa na ushiriki mkubwa zaidi katika huduma, na kuona mkono wa Yehova wenye upendo ukituandalia sisi kiroho na kimwili hutufanya tutake kumsifu hata zaidi.”
Kwa zaidi ya miaka mia moja Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi imegawanya Biblia na fasihi ya Biblia kwa kujitolea yenyewe ifanye hivyo na ikachapa fasihi hiyo katika matbaa zao wenyewe tangu 1920. Wakati na jitihada za wafanya kazi wanaojitolea Betheli kutokeza vichapo vyote tulivyo navyo leo, pamoja na zile za wahubiri wa kundi na mapainia ili kueneza fasihi hiyo, kwa kweli huwa ni mchango zaidi kwenye ile kazi muhimu ya kuhubiri.—Mathayo 24:14.
Pia, Wakristo walio katika nchi zilizo na uthabiti mwingi zaidi wa kiuchumi wanafurahi kujua kwamba zawadi zao za pesa wanazotoa kwa fadhili, zinazopelekwa kwenye ofisi ya tawi ya Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi katika nchi yao, zinawezesha wengi wa ndugu zao katika sehemu nyingine za ulimwengu watumie wakati wao wote katika kuhubiri na kufanya wanafunzi. Wamisionari kutoka Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi, waangalizi wa mizunguko na wilaya, na mapainia wa pekee wanasaidiwa wote kuendelea katika utumishi wao wa wakati wote na michango hiyo ya kujitolea.
Labda haiwezekani wewe kutumikia Betheli au ukiwa mshiriki wa Programu ya Wafanya Kazi wa Ujenzi wa Kujitolea. Lakini labda wewe una pesa zinazoweza kutegemeza wale wanaojihusisha katika utendaji huo lakini wasio na “ziada” ya pesa za kuwadumisha humo. Kwa njia hiyo usawazisho wenye msaada unaweza kutukia, kama unavyoelezwa kwenye 2 Wakorintho 8:14. Barua zenye kuambatana na michango hiyo zimetia ndani jambo linalofuata kutoka kwa dada mmoja mzeemzee aliyeandika hivi:
“Mimi natoa sana shukrani kwa ajili ya baraka zote ambazo Yehova hunipa, nami husali kwa uendelevu kwa ajili ya miradi ya ujenzi na tengenezo.”
Dada mwingine alisema: “Naona ni afadhali kiasi kidogo hiki kifanye wema fulani wa kitheokrasi badala ya kubaki katika benki ambayo itaangamia baada ya kitambo kidogo!”
Ndugu mmoja alijieleza kwa maneno haya: “Kushauriwa kwetu na Yehova tutumie mali zetu ili kumtukuza yeye ni njia ya kupewa himaya halisi tusipatwe na ubiashara wenye pupa, ambao ndilo ‘bawa la tatu’ la mfumo mbovu wa mambo ya Shetani. Acheni nitumie fursa hii kusema jinsi ninavyoterema kuchangia kidogo uharakishaji wa ongezeko ambalo Yehova anatupa sisi, nami nampa asante kwa kufanya kuwe na uwezekano wa mimi kutumiwa.”
Zawadi Kutoka kwa Wenye Umri Mkubwa na Vijana
Inatia moyo kusoma jinsi wazeewazee wamepiga moyo konde kwa uaminifu, ambao, ingawa wanatumainia kuokoka mwisho wa mfumo huu, kwa kufanya wasia unaofaa wanahakikisha kwamba kazi ya Ufalme itanufaika wakifa. Maneno fulani yaliyopokewa kutoka kwa wenye kutekeleza maagano ya wasia, yakieleza juu ya mwelekeo mzuri sana wa wenye kufanya maagano hayo, ni pamoja na haya:
“Alikuwa mwanamke mwenye fadhili sana kwa kila mmoja, muda wa maisha yake yote . . . yeye alipenda Yehova na uumbaji wake.”
“Sikuzote, masilahi ya Ufalme yalikuwa ndilo hangaikio lake la kwanza.”
“Mwanamume huyu alifikia thawabu yake ya kimbingu baada ya miaka 70 ya utumishi mwaminifu . . . sikuzote yeye alitaka kuendeleza ukweli kwa majaliwa yake.”
Sisi huona shangwe pia kusikia kutoka kwa vijana, waliokaza nia watumie vitu vyao vya kimwili kwa ajili ya kazi ya Yehova. Barua moja iliyopokewa kwenye ofisi ya Sosaiti katika Uingereza ilitoka kwa mhubiri mwenye umri wa kwenda shule. Yeye alisimulia kwamba alikuwa ameshinda zawadi ya kwanza katika shindano la kuandika insha. Alitia zawadi yote ya pesa ndani ya bahasha aliyopeleka. Vichapo vya Sosaiti vilikuwa ndicho chanzo pekee alimotoa habari za insha yake kuhusu “Wajibu wa Kikristo,” kwa hiyo alihisi kwamba kwa haki pesa hizo zilikuwa za Yehova.
Baada ya kuuliza atamlipa Yehova marudishio gani, mwandikaji wa Zaburi 116 anaendelea kusema hivi katika mistari 13 na 14: “Nitakipokea kikombe cha wokovu; na kulitangaza jina la Bwana [Yehova, AW]; nitaziondoa [nitalipa, NW] nadhiri zangu kwa Bwana [Yehova, NW], naam, mbele ya watu wake wote.” Kwa kuthamini zawadi ya thamani kubwa sana ya wokovu kutoka kwa Yehova kupitia Mwanaye, sisi tunahisi tukisukumwa, kama mtunga zaburi, kumtangaza Yeye na kutimiza ahadi tulizomtolea Yeye.
Yehova ametunufaisha sana, na chochote tunachoweza kufanya ili kumpa marudishio huonekana kidogo kwa ulinganisho. Basi, inafaa kama nini tufanye yote tuwezayo ili kuonyesha shukrani, kwa kila njia! “Nitakutolea dhabihu ya kushukuru; na kulitangaza jina la Bwana [Yehova, NW].”Zaburi 116:17.
[Sanduku katika ukurasa wa 26]
JINSI WENGINE WANAVYOCHANGIA KAZI YA UFALME
◻ ZAWADI: Michango ya kujitolea ya pesa ingeweza kupelekwa moja kwa moja kwenye ofisi ya tawi la kwenu ya Sosaiti. Mali kama vile rasilmali za urithi, na pia vito vyenye thamani au vitu vingine vya bei kubwa, vinaweza kuchangwa pia. Barua fupi ikisema kwamba huo ni mchango wa moja kwa moja inapasa ifuatane na michango hiyo.
◻ MPANGO WA MCHANGO WENYE MASHARTI: Pesa zinaweza kupewa kwa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi zishikiliwe zikiwa amana, kukiwa na uandalizi wa kwamba kikitokea kisa cha uhitaji wa kibinafsi, zitarudishwa kwa mwenye kuchanga.
◻ BIMA: Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi inaweza kutajwa kuwa mwenye kunufaishwa na mpango wa bima ya maisha au katika mpango wa kustaafu kazi/malipo ya uzeeni. Sosaiti inapasa kujulishwa juu ya mipango yoyote kama hiyo.
◻ AMANA: Akiba za pesa zilizo benki zinaweza kuwekwa zikiwa amana kwa ajili ya Sosaiti. Jambo hilo likifanywa, tafadhali ijulishe Sosaiti. Rasilmali za hisa, dhamana, nyanja na majengo zinaweza pia kuchangwa chini ya mpango wa kunufaisha mwenye kuchanga katika muda wa maisha yake. Njia hiyo huondolea mbali gharama na mashaka-mashaka yanayotokana na ule mpango wa kuthibitisha usahihi wa wasia, huku njia hiyo ikihakikisha kwamba Sosaiti itapokea uwanja au jengo hilo ikiwa kifo kitatukia.
◻ MAWASIA: Uwanja na majengo au pesa zinaweza kupangiwa ziwe urithi wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi kupitia wasia wenye kutekelezwa kisheria. Nakala moja inapasa kupelekwa kwa Sosaiti.
Kwa habari zaidi na mashauri kuhusu mambo hayo, andikia ofisi ya tawi la kwenu la Sosaiti.
-
-
Sisi Tuligeukia Chanzo cha Uadilifu wa KweliMnara wa Mlinzi—1988 | Desemba 1
-
-
Sisi Tuligeukia Chanzo cha Uadilifu wa Kweli
Kama ilivyosimuliwa na Erwin Grosse
MIAKA michache iliyopita, asubuhi ya mapema ilikuwa ikinipata nikiwa kwenye kiwanda kikubwa cha kuundia meli katika Kiel, Ujeremani, nikigawa vikaratasi na kuuza Rote Fahne, gazeti la KPD/ML.a Wakati ule ule ningekuwa nikijaribu kuvuta wafanya kazi na wakurufunzi ili wahusike katika majadiliano. Ilikuwa kazi ya bure kujaribu kuwasadikisha kauli zangu za kikomunisti.
Hata hivyo, sikuacha jambo hilo linivunje moyo. Mimi nilikuwa nimegundua mradi maishani: kusaidia kutokeza hali za uadilifu kupitia mapinduzi makubwa ulimwenguni. Ni jinsi gani nilivyofikia kuwa na rai hiyo? Je! mradi huo maishani ungeridhisha njaa yangu ya kutaka uadilifu?
Kutafuta Uadilifu
Njia ya maisha ya wazazi wangu ilikuwa kujikaza kabisa wakitafuta ufanisi wa vitu vya kimwili, nayo haikunivutia kamwe. Sisi vijana tulikuwa tukitafuta kitu bora. Mitindo mipya ya maisha ilikuwa ikijaribiwa, na makusudi mapya maishani yakawa yakitangazwa. Wakati huo, vita ya Vietnam na msukosuko wa wanafunzi ndiyo mambo yaliyokuwa yakitangazwa sana magazetini. Kwetu ilionekana kwamba watu wasio na hatia walikuwa wakitoa uhai wao ili kulipia ukichaa wa fahari ya umashuhuri ya wanasiasa na wabepari. Hali hiyo ililemea sana akili yangu, nami nikaanza kuchukia mfumo wa kibepari.
Pia nilielekeza kisogo changu kwenye dini zenye kuimarika sana. Jambo moja lililonipata nikitumikia katika kani za kijeshi za Ujeremani Magharibi ndilo lililonisaidia kufanya uamuzi huo. Mbinu za kijeshi tulizokuwa tukijihusisha nazo zilikatizwa ili tufanye utumishi wa kambi, na askari-jeshi waligawanywa wawe vikundi-vikundi vya Wakatoliki na Waprotestanti. Kwenye umalizio wa utumishi huo,
-