-
Nani Atakuwa Mwenye Kukubaliwa na Yehova?Mnara wa Mlinzi—1988 | Novemba 15
-
-
kwa maana wao walikuwa wameondoshwa nje kwa kuwa wakosaji wasioonyesha toba. (Waebrania 10:38; linganisha 1 Wakorintho 10:5.) Ithibati inaonyesha ni wachache tu waliotengwa na ushirika. Walio wengi ambao walipata “fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu” na ‘wakachaguliwa kuwa wana wa kimalezi kulingana na raha njema ya mapenzi yake’ walibaki wakiwa waaminifu.—Waefeso 1:2, 5, 8-10.
24. Ni upande gani wa habari hii unaostahili kuangaliwa zaidi?
24 Ndivyo ilivyo kwa msingi katika wakati wetu, pia. Ingawa hivyo, acheni tufikirie jinsi ‘wasioitikadi au watu wa kikawaida’ wanavyoweza kusaidiwa wakubaliwe na Mungu leo na mambo yanayoweza kufanywa kuwasaidia wakikosa wanapokuwa mwendoni. Makala inayofuata itashughulika na mambo hayo.
-
-
Kusaidia Wengine Waabudu MunguMnara wa Mlinzi—1988 | Novemba 15
-
-
Kusaidia Wengine Waabudu Mungu
“Ikiwa . . . asiyeitikadi yeyote au mtu wa kikawaida anakuja ndani,... siri za moyo wake zinakuwa dhahiri, hivi kwamba yeye ataanguka juu ya uso wake na kuabudu Mungu.”—1 WAKORINTHO 14:24, 25, NW.
1-3. Ni jinsi gani wengi katika Korintho walivyosaidiwa kupata kibali cha Mungu?
KATIKA safari yake ya pili ya umisionari, mtume Paulo alikaa katika jiji la Korintho kwa mwaka mmoja na nusu. Humo yeye ‘alisongwa sana [alishughulika mno, NW] na lile neno, akishuhudia.’ Tokeo likawa nini? “Wakorintho wengi waliposikia, waliamini, wakabatizwa.” (Matendo 18:5-11) Wao wakawa “waliotakaswa . . . , walioitwa wawe watakatifu.”—1 Wakorintho 1:2.
2 Baadaye Apolo alizuru Korintho. Mapema kidogo, Prisila na Akila walikuwa wamemsaidia aelewe “njia ya Bwana kwa usahihi zaidi,” kutia na ubatizo. Hivyo yeye akawa Mkristo mwenye nia njema au kibali cha Mungu. (Matendo 18:24–19:7) Apolo naye, kwa zamu yake, alisaidia Wakorintho ambao hapo kwanza ‘walikuwa wamechukuliwa kufuata sanamu zisizonena.’ (1 Wakorintho 12:2) Inaelekea kuwa watu hao walipewa maagizo ya Biblia katika maskani zao; wangeweza pia kujifunza kwa kuhudhuria mikutano ya Kikristo.—Matendo 20:20; 1 Wakorintho 14:22-24.
3 Tokeo la fundisho hilo lilikuwa kwamba wengi ambao hapo kwanza walikuwa ‘wasioitikadi na watu wa kikawaida’ walivutwa kwenye ibada ya kweli. Lazima iwe iliridhisha sana kuona wanaume na wanawake wakifanya maendeleo kuelekea ubatizo na kibali cha Mungu! Jambo hilo lingali linaridhisha.
Kusaidia ‘Wasioitikadi na Watu wa Kikawaida’
4. Ni katika njia gani wengi leo wanasaidiwa kama wale waliokuwa katika Korintho?
4 Mashahidi wa Yehova leo pia wanatii amri ya Yesu “kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza.” (Mathayo 28:19, 20, NW) Baada ya kupanda mbegu za ukweli katika mioyo yenye upokezi, wao wanarudi na kuzitia maji. (1 Wakorintho 3:5-9; Mathayo 13:19, 23) Mashahidi wanatolea watu mafunzo ya Biblia ya kimaskani kila juma bila malipo ili watu hao waweze kujibiwa maswali yao na waweze kujifunza kweli za Biblia. Watu hao wanaalikwa pia kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova mitaani mwao, hata kama vile “wasioitikadi” wa karne ya kwanza walivyohudhuria katika Korintho. Lakini inawapasa Mashahidi wa Yehova wawe na rai gani juu ya watu ambao wanajifunza Biblia na kuja mikutanoni?
5. Kuna msingi gani wa Kimaandiko wa kuwa na tahadhari katika kushughulika pamoja na watu fulani?
5 Sisi tunafurahi sana kuwaona wakimkaribia Mungu. Na bado, sisi tunazingatia akilini kwamba wao si waitikadi waliobatizwa. Kumbuka pia masomo mawili ambayo msingi wayo ni makala iliyotangulia. (1) Waisraeli walionyesha hadhari kuelekea walowezi wa kigeni ambao, ingawa walikuwa karibu-karibu na watu wa Mungu na walitii sheria fulani-fulani, hawakuwa waongofu waliotahiriwa, akina ndugu katika ibada. (2) Wakristo Wakorintho wenye kushughulika pamoja na ‘wasioitikadi na watu wa kikawaida’ walikuwa chonjo kwa sababu ya maneno ya Paulo: “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi?”—2 Wakorintho 6:14.
6. Ni jinsi gani ‘wasioitikadi’ wanavyoweza ‘kukaripiwa’ na mikutano, na karipio hilo linakuwa la hali gani?
6 Kwa hiyo ingawa sisi hukaribisha ‘wasioitikadi na watu wa kikawaida,’ tuna habari kwamba wao hawajatimiza bado viwango vya Mungu. Kama vile Biblia inavyoonyesha kwenye 1 Wakorintho 14:24, 25, NW, huenda watu hao wakahitaji ‘kuchunguzwa kwa ukaribu,’ hata ‘kukaripiwa’ (kubainishwa, UV), na mambo ambayo wanajifunza. Karipio hilo si la namna ya kihukumu; hawaitwi mbele ya halmashauri ya hukumu ya kundi kwa kuwa bado wao si washiriki walo waliobatizwa. Badala ya hivyo, kutokana na wanayojifunza, wapya hao wanakuja kusadiki kwamba Mungu hushutumu njia zozote za ubinafsi na za kukosa adili.
7. Ni maendeleo gani zaidi ambayo wanafunzi wengi watataka kufanya na kwa nini?
7 Wengi wasiobatizwa huenda baadaye wakataka kuchukua hatua inayozidi kuhudhuria mikutano tu wakiwa wajifunzi wenye kupendezwa. Maneno haya ya Yesu yanaonyesha kwa nini: “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake, lakini kila mtu ambaye amehitimu hulingana na mwalimu wake.” (Luka 6:40) Mwanafunzi wa Biblia anaweza kuona kwamba mwalimu wake ana rai ya kwamba huduma ya shambani ni muhimu na anapata furaha kutokana nayo. (Mathayo 24:14) Kwa hiyo imani inapokua, yule ambaye amekuwa akijifunza kweli za Biblia na kuhudhuria mikutano huenda akathamini moyoni maneno haya: “Jinsi ilivyo mizuri juu ya milima miguu yake aletaye habari njema, yeye aitangazaye amani, aletaye habari njema ya mambo mema, yeye autangazaye wokovu.” (Isaya 52:7; Warumi 10:13-15) Ingawa hajabatizwa, huenda yeye akataka kuwa mhubiri wa Ufalme mwenye kujifuatanisha na kundi la Mashahidi wa Yehova.
-