Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/89 kur. 1-4
  • Kutanguliza Masilahi za Ufalme Kwanza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutanguliza Masilahi za Ufalme Kwanza
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUHESABU GHARAMA
  • ACHENI KUWA WENYE WASIWASI
  • FANYA MIPANGO SASA
  • “Fulizeni Kutafuta Kwanza Ufalme”
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • Unamtegemea Mungu Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Tafuta Ufalme, Si Vitu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Amua Kuunga Mkono Ufalme wa Mungu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 11/89 kur. 1-4

Kutanguliza Masilahi za Ufalme Kwanza

1 Wale ambao wanatumia shauri la Yesu kutafuta Ufalme kwanza wanapata kwamba wanahitaji kuweka mambo ya kutangulizwa kwanza katika maisha zao. (Mt. 6:33) Pia wanapata kwamba kufuata shauri la Yesu kunafanya iwezekane kwao kushinda vipingamizi. Ni jambo lenye kusifika kwamba ndugu na dada wengi wenye washiriki wa jamaa wasioamini wanaendelea kwa uaminifu kutanguliza masilahi za Ufalme kwanza.

2 Jinsi Yesu alivyoonyesha kwa njia yenye kusadikisha kwamba aliweka Ufalme kwanza katika maisha yake! Alipokuwa akihojiwa na Pilato, alibaki akiwa imara. (Yoh. 18:36, 37) Ndiyo, hata alipokuwa akifa kwenye mti, aliendelea kukazia tumaini la Ufalme wa Mungu, akimwambia yule mtenda uovu: “Utakuwa pamoja nami katika Paradiso.”—Luka 23:43, NW.

KUHESABU GHARAMA

3 Kwa nini Yesu aliuona Ufalme kuwa wa maana sana? Alikuwa amepelekwa kutoka mbinguni ili ‘aishuhudie kweli’ kwamba Ufalme wa Mungu ungetawala kwa uadilifu na ufanye iwezekane kwa penzi Lake kutimizwa duniani kama mbinguni. Basi ni shangwe kubwa iliyoje kushiriki katika kutimiza penzi la Yehova la kugeuza dunia iwe Paradiso ambayo ilikusudiwa hapo awali! Ndiyo, ni baraka za namna gani zilizo akibani kwa aina ya binadamu yenye kuamini chini ya utawala wa Ufalme!

4 Kuiga Yesu akiwa mtetezi wa Ufalme wa Mungu kunatia ndani kubeba “mti wa mateso” na yote ambayo kufanya hivyo kunatia ndani. ‘Kuhesabu gharama’ kunamaanisha kwamba lazima mtu awe tayari kusema “kwaheri ya kuonana” kwa vitu vya kimwili ikiwa vinamzuia kumtolea Mungu utumishi. (Luka 14:27, 28, 33, NW) Wakati ule ule, Yesu aliwatia moyo mkuu wote wawe wafuasi wake na kushiriki habari njema pamoja na wengine. Kupata uhai wa milele chini ya utawala wa Ufalme kunastahili gharama yoyote ile.—Mt. 13:44-46.

ACHENI KUWA WENYE WASIWASI

5 Kupita kwa karne 19 hakujapunguza uhitaji wa kutanguliza masilahi za Ufalme kwanza katika maisha zetu. Ni jambo njema kujiuliza wenyewe ikiwa kutumikia Yehova ni kwa maana kubwa kwetu. Yesu alieleza: “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili . . . Hamwezi kumtumikia Mungu na mali. . . . Msisumbukie [Acheni kuwa wenye wasiwasi, NW] maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini.” (Mt. 6:24, 25) Je! sisi tuna wasiwasi kuhusu nafsi zetu? Au tunapata imani ya kutosha kufuata shauri la Yesu la kutafuta Ufalme kwanza, tukitumaini kwamba tutazidishiwa mambo mengine yote?

6 Akina ndugu fulani wamekataa kazi zenye mshahara mnono kwa sababu zitaingiliana na utendaji wa kitheokrasi. Wengine wamelazimika kubadili kazi ya kuajiriwa ilipopingana na kanuni za Biblia. Waajiri wengine wamekubali kuwaajiri Mashahidi wa Yehova ambao wamethibitika kuwa wafanya kazi wenye nia, wenye kutegemeka. (Kol. 3:23, 24) Kwa kweli, kundi linaimarishwa katika njia nzuri wakati wazee, watumishi wa huduma, na wengine wanapoweka kielelezo chema katika kutafuta Ufalme kwanza.

FANYA MIPANGO SASA

7 Karibuni wengine wenu nyinyi vijana mtamaliza shule. Je! mnafanya mipango sasa kwa ajili ya kazi ya kitheokrasi? Je! mnakusudia kufanya kazi ya siku nzima kwa wakati fulani kabla hamjachukua upainia? Ni jambo lenye kusifika kwamba mnafikiria juu ya kushiriki katika kazi ya upainia wakati ujao. Hata hivyo, ikiwa kweli Ufalme ni jambo la kwanza katika maisha yenu na hali zenu zinaruhusu, mbona msitangulize kazi ya upainia kwanza? Kazi ya kimwili inapochukua mahali pa kwanza, kuna tatizo kwamba moyo wako utalemewa na wasiwasi unaovunja moyo kufanya upainia.—Mt. 6:27, 34; Luka 21:34.

8 Ulimwengu huu unataka mengi sana kutoka kwa wale ambao wana nia ya kuutumikia. Tukifanya maisha zetu ziwe sahili na kuhakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi, tutapata mibaraka kwa kutafuta Ufalme kwanza. Badala ya kutumbukia katika mitego ya ulimwengu, lingekuwa jambo zuri kama nini kumtegemea Yehova, anayejua mahitaji yetu na ametoa ahadi ya kuyatimiza! Kwa kutanguliza masilahi za Ufalme kwanza, maisha zetu zitakuwa na kusudi halisi, zikiimarishwa na taraja la mibaraka ya wakati ujao isiyokoma.—Mt. 6:32; 1 Tim. 6:17-19.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki