-
YehovaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
jina lililo juu ya kila jina lingine, ili katika jina la Yesu kila goti lipigwe la wale walio mbinguni na wale walio duniani na wale walio chini ya nchi, na kila ulimi ukiri waziwazi kwamba Yesu Kristo ni Bwana kwa utukufu wa Mungu Baba.” (Ona kwamba Yesu Kristo hapa anatofautishwa na Mungu Baba na kwamba anamtii Yeye.)
Mtu anawezaje kumpenda Yehova ikiwa anapaswa kumwogopa pia?
Biblia hutuambia kwamba tunapaswa kumpenda Yehova (Luka 10:27) na pia kumwogopa. (1 Pet. 2:17; Met. 1:7; 2:1-5; 16:6) Kumwogopa Mungu kwa njia inayofaa kutatufanya tuwe waangalifu sana tusimkasirishe. Kumpenda Yehova kutatusukuma tutake kufanya mambo yanayompendeza, kumshukuru kwa kutuonyesha upendo na fadhili zisizostahiliwa kwa njia nyingi.
Mfano: Mwana huogopa kumkasirisha baba yake, lakini kuthamini yote ambayo baba yake humfanyia kunapaswa pia kumsukuma mwana huyo kumpenda baba yake kikweli. Huenda mwogeleaji akasema kwamba yeye anaipenda bahari, lakini kuiogopa bahari humfanya afahamu kwamba kuna mambo anayopaswa kuepuka kufanya. Vivyo hivyo, kumpenda Mungu kunapaswa kuambatana na kuogopa kufanya lolote litakalomkasirisha.
-
-
Yesu KristoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Yesu Kristo
Maana: Mwana mzaliwa-pekee wa Mungu, Mwana pekee aliyefanyizwa na Yehova peke yake. Mwana huyo ndiye mzaliwa wa kwanza wa uumbaji wote. Vitu vingine vyote mbinguni na duniani viliumbwa kupitia kwake. Yeye ndiye mtu wa pili kwa ukuu ulimwenguni pote. Ndiye Mwana ambaye Yehova alimtuma duniani ili atoe uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wanadamu, na kwa kufanya hivyo, alifungua njia ya uzima wa milele kwa ajili ya watoto wa Adamu ambao wangekuwa na imani. Mwana huyohuyo, aliyerudishwa kwenye utukufu wa mbinguni, sasa anatawala akiwa Mfalme, akiwa na mamlaka ya kuwaharibu waovu wote na kutimiza kusudi la kwanza la Baba yake kwa ajili ya dunia. Katika Kiebrania, jina Yesu humaanisha “Yehova Ni Wokovu”; jina Kristo linalingana na jina la Kiebrania Ma·shiʹach (Masihi), linalomaanisha “Mtiwa-Mafuta.”
-