-
“Kesheni”Mnara wa Mlinzi—1979 | Machi 15
-
-
katika miaka ya 1918 mpaka 1919. Na bado mpanda farasi huyo angali akipanda. Ijapokuwa kumekuwako maendeleo katika uvumbuzi wa dawa, jamii ya wanadamu ingali ikisumbuliwa leo na magonjwa ya kipuku (magonjwa mabaya sana ya kuambukia). Matumizi ya dawa za magonjwa yanaongezeka sana. Lakini kuongezeka kwa magonjwa ya moyo, kifafa, donda baya, kaswende na kisonono na masumbuo yasiyohesabika, kunapeleka wengi kaburini. Sana sana katika huu “wakati wa mwisho,” kaburi (katika Kiebrania Sheol) halisemi “Inatosha!” (Mit. 30:15, 16, NW) Vilevile watu wa Yehova wameumizwa na kupandwa kwa farasi huyo wa rangi kijivu, mwenye kuua, maana wao ni wanadamu wenye kupatwa na magonjwa. Lakini wao wanajua sababu ya magonjwa yao ya mwili, nao wako tayari kuyavumilia wakiwa na furaha, maana wanajua kwamba dhabihu ya Yesu itaondoa karibuni magonjwa hayo yote ya kuambukia—hata mpanda farasi mwenyewe, yaani, Mauti. Wajapokufa na kuzikwa kaburini, wameahidiwa kufufuliwa katika taratibu mpya yenye haki.—Yohana 5:28, 29.
14. Sababu gani imetupasa tushukuru kwa sababu ya maono hayo, nayo?
14 Kupanda kwa hao wapanda farasi kunaonekana wazi hata leo. Wanadamu wote sasa wanapatwa na vita vya kutumia vifaa vyote, upungufu wa chakula, magonjwa ya kipuku na kifo cha kuua watu wengi kama mainzi. Lakini ni wale tu wanaoona kwa macho ya imani, ndio wanaomwona farasi huyo mweupe, pamoja na “Mfalme wa wafalme” ambaye ni mshindi, yaani, yule mtu aliyevikwa taji na mwenye upinde. Jinsi inavyotupasa tushukuru kwa sababu ya maono hayo yenye kutia imani nguvu! Yamepaswa yatuchochee tuwe na bidii sana katika kutoa ushuhuda wa mambo hayo. Katika njia hiyo, tunaweza kuwa washikamanifu kwa agizo lililotoka kwa Yehova kwa kufuata mfano wa Yesu, ambaye akaitwa “Mwaminifu na wa kweli”—“Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli.”—Ufu. 3:14; 19:11.
USIVUTWE NA MAMBO MENGINE!
15. Sababu gani tuliamini Neno la Mungu kuliko neno la wanadamu?
15 Ulimwengu hauamini kwamba mwisho wake umekaribia. Ungependa utuvute tusiamini hivyo, vilevile. Lakini wewe utamwamini nani—maneno yao au Neno la Mungu? Ni Neno la Mungu linaloeleza wazi kwamba tunaishi katika “mwisho wa taratibu ya mambo.” Wala hata silaha za makombora ya atomiki za “mungu wa ngome”—zinazosifiwa na “mfalme wa kaskazini”—haziwezi kitu katika kupigana na “Mfalme wa wafalme” aliye mshindi kabisa.—Dan. 11:38, 45.
16. Ni shauri gani jema ambalo Paulo anatoa katika Waroma 13:11, 12, nasi tunaweza kuitikiaje?
16 Mtume Paulo anampa shauri jema ye yote anayeelekea kama amekuwa mwenye kusinzia, akisema:
“Sasa ndio wakati wa kuamka usingizini; naam, wokovu wetu u karibu zaidi sasa kuliko wakati ule tulipoanza kuamini. Usiku unakwisha na mchana unakaribia. Basi, tutupilie mbali mambo yote ya giza, tukajitwalie silaha za mwanga.” (Rom. 13:11, 12, Habari Njema kwa Watu Wote)
Silaha hizo za mwanga twazijua sana, maana limekuwa pendeleo letu la maana kuzitumia katika kutangaza “habari njema ya ufalme” katika dunia yote kuwa ushuhuda.—Mt. 24:14; Efe. 6:11-17.
17. Tunaweza kuepukaje “mambo yote ya giza”?
17 Walakini, namna gani “mambo yote ya giza”? Hayo ni matendo ya ulimwengu, mambo ambayo watu wenye kufikiria mambo ya kimwili wanapenda kufanya pasipo kumfikiria Mungu na njia yake ya nuru. Kwa hiyo imetupasa tuyaepuke. “Mwenendo wetu uwe wa adabu kama inavyostahili wakati wa mwanga; tusiwe na ulafi na ulevi, uchafu na uasherati, ugomvi na wivu.” (Rom. 13:13, Habari Njema kwa Watu Wote) Hayo ni mambo ya ulimwengu ambayo yangeingia katika maisha yetu ya Kikristo na katika kundi ikiwa tungeyaruhusu. Ni lazima tujihadhari nayo. Katika nchi zenye utajiri zaidi, kwa kawaida watu wanaona kustarehe na kuwa na mali za kimwili ni kwa maana sana. Mahali pengi, ile juma ya kufanya kazi inazidi kuwa fupi sana, kupenda anasa kunazidi kuongezeka, na watu wa Mungu wanakazwa wawe kama ulimwengu ulivyo. Je! tutashinda tatizo hilo katika roho ya Kikristo ya kujinyima?
18. Kukaza fikira zetu juu ya mambo ya kiroho kutakuwa ulinzi wetu namna gani?
18 Tukiwa wenye bidii katika utumishi wa Mungu, tukiwa macho na kukesha ili tufanye utumishi huo, basi hatutakuwa na wakati wa kuvutwa na “ulafi na ulevi,” pamoja na “uchafu na uasherati.” Kumpenda kwetu Yehova na kupenda utumishi wake, na kutanguliza hayo, kutakuwa ulinzi wetu. (Mt. 6:33) Fikira zetu zikiwa juu ya mambo ya kiroho, na juu ya kusitawisha tunda la roho, tutakuwa wanyenyekevu na wenye kufahamu katika uhusiano wetu na jamaa zetu na ndugu zetu. Tutaepuka “ugomvi na wivu.”
19, 20. (a) Ni mfano gani bora ambao Yesu alituachia sisi? (b) Tutapataje faida tukitii shauri katika Waroma 13:14?
19 Mtume Paulo anaendelea kusema: “Bwana Yesu Kristo awe vazi lenu; msishughulikie tena tamaa zenu za maumbile na kuziridhisha.” (Rom. 13:14, Habari Njema kwa Watu Wote) Lo! Bwana Yesu Kristo ni mfano wetu bora kweli kweli! Katika huduma yake yote ya hapa duniani, yeye alikuwa macho ili afanye mapenzi ya Yehova, lililokuwa pendeleo lake bora. Hakuna hata wakati mmoja alipoepuka utumishi wake wa nafsi yote wa kujulisha wengine jina la Baba yake. Hata siku aliyopaswa kufa, lo! jinsi alivyoonyesha upendo na kujinyima, akitumia kila dakika ya saa zake zilizobaki ili awape wanafunzi wake maagizo yanayofaa! (Yohana sura 13 kufika 17) Yesu alipokuwa akikaribia mwisho wake katika mti wa mateso, alikataa dawa ya kulevya ambayo labda ingepunguza maumivu yake makali. Yeye alitaka atunze kabisa akili zake, awe mwenye kushika ukamilifu mpaka mwisho.—Mt. 27:34.
20 Sote na tuhesabiwe kuwa pamoja na wale wanaomfanya “Yesu Kristo awe vazi” lao, wakizifuata sana nyayo zake. (1 Pet. 2:21; Mt. 16:24, 25) Kwa kutangulia kupangia mambo ya kiroho, si ya kimwili, tunaweza kuendelea kukesha sana katika utumishi wa Yehova kama Yesu. Basi na tuendelee kukesha, tukiyajaza maisha yetu utumishi wa Ufalme mpaka ile saa ambayo “Mwana wa Adamu” atakapokuja kutekeleza hukumu. Zawadi yetu itakuwa kubwa! —Kutoka The Watchtower, Oct. 1, 1978.
-
-
Elimu InayoridhishaMnara wa Mlinzi—1979 | Machi 15
-
-
Elimu Inayoridhisha
UKITOLEWA nafasi ya kujifurahisha furaha ya kweli, afya njema pamoja na usalama wa kweli, je! ungeichukua nafasi hiyo? Bila shaka ungefanya hivyo. Walakini, huenda ukasema: ‘Hivyo ni vizuri sana. Lakini je! kweli kuna nafasi kama hiyo?’ Ndiyo, iko. Faida hizi zaweza kupatikana kutokana na elimu inayo-tolewa kwa watu wote bure duniani pote.
Leo inakubaliwa mahali pote kwamba elimu ina thamani nyingi. Watu wengi wanalinganisha elimu na ufanisi, fahari na fedha nyingi. Kwa hiyo wanakuwa na nia ya kutumia fedha nyingi na wakati mwingi ili wapate elimu bora. Kwa mfano, katika nchi za Asia wazazi wengi wanafanya kazi kwa bidii sana ili waweze kuwatuma watoto wao katika shule za pekee na katika vyuo vikuu. Watoto wenyewe wanajifunza usiku na mchana ili wafaulu mitihani yao, wakiwa na mradi wa kupata elimu bora. Hiyo, nayo, huenda ikawawezesha kupata kazi yenye mshahara mzuri na kusonga mbele katika ulimwengu. Kwa upande mwingine, wengine wa-natafuta elimu ya juu ili wajitayarishe kuwatumikia zaidi wanadamu wenzao.
Ni kweli, wale wanaopata elimu nzuri ya kilimwengu huenda wakapata kadiri fulani ya uradhi wanapofikia miradi yao maishani. Walakini, uradhi wa namna hiyo huwa wa muda
-