Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/90 kur. 1-2
  • Heshimu Yesu Kristo—Msingi wa Imani Yetu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Heshimu Yesu Kristo—Msingi wa Imani Yetu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUDHIHIRISHA SHUKRANI
  • KUHUBIRI CHINI YA UKICHWA WA KRISTO
  • Endelea Kunufaika na Mnara wa Mlinzi na Amkeni!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 4/90 kur. 1-2

Heshimu Yesu Kristo—Msingi wa Imani Yetu

1 Kuelewa fungu la Yesu Kristo katika kutimizwa kwa makusudi ya Yehova ni kwa muhimu. Yesu alitoa uhai wake kuwa ukombozi kwa ajili ya aina-binadamu watiifu. (Mt. 20:28) Bila ya maandalizi ya upendo ya Yehova kupitia Yesu Kristo, sisi tungeendelea kuwa katika hali ya kufa bila tumaini lolote kwa wakati ujao.

2 Wakati wa majira ya Ukumbusho hasa, tunatafakari juu ya maisha ya Yesu, mafundisho yake, na dhabihu yake. (Luka 22:19) Kuthamini kwamba “Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi,” tunachochewa tuheshimu Mungu na Kristo kwa kushiriki kwa idili pamoja na wengine habari njema. Tunaweza kufanyaje hivyo?—Rum. 5:8, 10.

KUDHIHIRISHA SHUKRANI

3 Tunatambua kwamba tengenezo la Yehova lionekanalo hufanya kazi chini ya ukichwa wa Yesu. Hapa duniani, jamii ya mtumwa mwaminifu hutupa chakula cha kiroho tunachohitaji. Tangu ujana wake kuendelea, Yesu alionyesha uthamini wenye kina kwa ajili ya Neno la Baba yake, na sisi tunataka kufuata kielelezo chake kwa kujifunza na kuchanganua chakula cha kiroho kinachoandaliwa tukiwa na lengo la kufundisha wengine kwa njia yenye matokeo. (Mt. 24:45, 46; Luka 2:46-50) Shukrani zetu kwa ajili ya tengenezo na maandalizi ya kiroho ambayo linatoa zinaonyeshwa kwa sisi kufuata mwelekezo walo na kushirikiana na wazee.

4 Pia tunaweza kuonyesha heshima kwa Kristo na kupamba huduma yetu kwa kutumia tunayojifunza kutoka Neno la Mungu. Yesu alikuwa kuhani mkuu asiye na waa, “aliyetengwa na wakosaji.” (Ebr. 7:26) Yeye hakuwa na hatia ya kusema jambo na kufanya tofauti. Tukiwa watumwa wenzi, tunahitaji kuishi kulingana na kiwango icho hicho cha juu. Kwa hiyo tunapowaambia wengine juu ya mfumo mpya wenye uadilifu ambao Yehova ameahidi, tunataka kuwa tukiishi kwa njia ambayo itatutambulisha sisi pamoja na ulimwengu mpya huo.—Mt. 7:21; 1 Yohana 2:17.

KUHUBIRI CHINI YA UKICHWA WA KRISTO

5 Wakati wa Aprili na Mei, tutakuwa tukitoa andikisho la Mnara wa Mlinzi. Tunaweza kumheshimu Yesu kwa kuonyesha wanaotazamiwa kuwa wasomaji kwamba kusudi la Mnara wa Mlinzi, kama inavyoelezwa kwenye ukurasa wa 2 wa kila toleo ni kutia moyo watu “kuwa na imani katika Mfalme anayetawala sasa, Yesu Kristo, ambaye damu yake iliyomwagwa yaifungulia aina ya binanadamu njia ya kupata uhai wa milele.” Uhakikishe kutoa andikisho kwanza wakati wowote iwezekanapo. Andikisho lisipokubaliwa, waweza kutoa magazeti mawili na broshua, kwa njia hiyo kupanda mbegu fulani za ukweli.

6 Umati mkubwa mno wa watu ambao bado si Mashahidi wanaonyesha heshima kwa Yesu kwa kuhudhuria Ukumbusho. Je! wao wanaweza kusaidiwa wafanye maendeleo makubwa zaidi ya kiroho kupitia funzo la kibinafsi la Biblia? Ingekuwa vizuri kuhakikisha kwamba mtu fulani anawatembelea na kuwapa msaada unaohitajiwa. Kwa msaada wa upendo, huenda wengine wakafanya maendeleo kufikia hatua ya kushiriki katika huduma kabla ya sherehe nyingine itakayofuata ya Chakula cha Jioni cha Bwana.

7 Jinsi tulivyo wenye shukrani kwa ajili ya dhabihu ya upendo ya Mkombozi wetu, Yesu! Yeye ametuandalia tumaini hakika. Kigezo chake cha maisha na rekodi ya huduma yake vinatumika kuwa kielelezo kikamilifu kwetu kufuata.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki