Wimbo 91
Kufundishwa na Yehova
1. Yah hupeleka ukweli;
Ndiye mwalimu wetu.
Anaongoza kondoo
Akiwa na subira.
Ni wakati wa kujua
Ndiye Mukuu Sana,
Afundishaye kwa upendo
ambao ni wapole.
Na Mwanaye Yesu Kristo,
Alikuwa Mwalimu.
Alisema ya Babaye,
Kaeleza Ufalme.
Kama vifaranga-kuku,
Anasaidia wote.
Leo pia anafunza,
Kondoo zizini mwake.
2. Yah hutupa wachungaji.
Wanaotufundisha.
Ulimi umefundishwa
Ni wanyofu moyoni.
Wasaidia wanyonge.
Wanashauri pia.
Kufunza yaliyo ukweli;
Yehova hupendezwa.
Yah atufundisha sote;
Kiongozi ni Yesu.
Tuna pendeleo sana
Kweli moyo yagusa.
Mioyo ikiwakia
Wanaotaka ukweli,
Kwa kutangaza huenda
Wakaabudu Yehova.
3. “Jifunze juu ya Mungu,”
Tunakukaribisha.
Kufunza kwaendelea
Kunaleta wokovu.
Kwa vitabu na maneno
Habari za Ufalme
Zahubiriwa kote na kwa
kabila na taifa.
Sisi wanakazi-wenzi
Sharti tuendelee.
Tusonge nao ukweli,
Tukazie Ufalme.
Katika miaka elfu
Wafufuliwa ‘tapata
Elimu na kufikia
Uzima mukamilifu.