-
Kurudi kwa KristoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
“Mawingu” yanawakilisha nini? Ni kutoonekana. Wakati ndege inapokuwa katika wingu zito au juu ya mawingu, kwa kawaida watu walio chini hawawezi kuiona, ingawa huenda wakasikia mngurumo wa injini zake. Yehova alimwambia Musa hivi: “Nitakujia katika wingu lenye giza.” Musa hakumwona Mungu, lakini wingu hilo lilionyesha kuwapo kusikoonekana kwa Yehova. (Kut. 19:9; ona pia Mambo ya Walawi 16:2; Hesabu 11:25.) Kama Kristo angetokea akionekana kwa macho mbinguni, ni wazi kwamba si “kila jicho” lingemwona. Kwa mfano, kama angetokea Australia, je, angeonekana Ulaya, Afrika, na Amerika?
“Kila jicho litamwona” jinsi gani? Watatambua kutokana na matukio duniani kwamba yeye yupo ijapokuwa haonekani kwa macho. Pia likielekezea kuona ambako si kwa macho halisi, andiko la Yohana 9:41 linasema hivi: “Yesu akawaambia [Mafarisayo]: ‘Kama mngekuwa vipofu, hamngekuwa na dhambi. Lakini sasa mnasema, “Tunaona.” Dhambi yenu inabaki.’” (Linganisha na Waroma 1:20.) Baada ya kurudi kwa Kristo, watu fulani wanaamini; wanaitambua ishara ya kuwapo kwake. Wengine wanakataa uthibitisho, lakini Kristo atakapoanza kutenda akiwa yule aliyewekwa na Mungu kuwaangamiza waovu, wataona nguvu zake na kutambua kwamba uharibifu huo hautoki kwa wanadamu bali unatoka mbinguni. Watajua linalotukia kwa sababu walikuwa wameonywa mapema. Kwa sababu ya jambo linalowapata, ‘watajipiga-piga kwa kuomboleza.’
“Wale waliomchoma” ni nani? Kihalisi, askari wa Roma ndio waliomchoma Yesu alipouawa. Lakini walikufa zamani. Kwa hiyo, maneno hayo yanamaanisha watu wanaowatendea vibaya jinsi hiyohiyo, au ‘wanaowachoma,’ wafuasi wa kweli wa Kristo wakati wa “siku za mwisho.”—Mt. 25:40, 45.
Je, kweli inaweza kusemwa kwamba mtu ‘amekuja’ au kwamba yeye ‘yupo’ ikiwa haonekani?
Mtume Paulo alisema kwamba yeye ‘hakuwapo katika mwili bali alikuwapo katika roho’ na kutaniko lililokuwa huko Korintho.—1 Kor. 5:3.
Yehova alisema kwamba ‘anashuka’ ili kuvuruga lugha ya wajenzi wa mnara wa Babeli. (Mwa. 11:7) Pia alisema kwamba ‘anashuka’ ili kuwakomboa Waisraeli kutoka utumwani Misri. Na Mungu alimhakikishia Musa kwamba “Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe” ili kuwaongoza Waisraeli kuelekea Nchi ya Ahadi. (Kut. 3:8; 33:14) Lakini hakuna mwanadamu yeyote ambaye alimwona Mungu.—Kut. 33:20; Yoh. 1:18.
Biblia inahusianisha kuwapo kwa Kristo na matukio gani?
Dan. 7:13, 14: “Mtu fulani kama mwana wa binadamu [Yesu Kristo] alikuwa anakuja na mawingu ya mbingu; naye akaja kwa Mzee wa Siku [Yehova Mungu], nao wakamleta karibu mbele zake Yule. Naye akapewa utawala na heshima na ufalme, ili vikundi vyote vya watu, vya mataifa na lugha vimtumikie yeye.”
1 The. 4:15, 16: “Tunawaambia hivi kwa neno la Yehova, kwamba sisi tulio hai ambao tutabaki mpaka kuwapo kwa Bwana hatutawatangulia kwa vyovyote wale ambao wamelala usingizi katika kifo; kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni akiwa na mwito wenye amri, kwa sauti ya malaika mkuu na kwa tarumbeta ya Mungu, na wale walio wafu katika muungano na Kristo watafufuliwa kwanza.” (Kwa hiyo, wale watakaotawala pamoja na Kristo wangefufuliwa wawe pamoja naye mbinguni—kwanza wale waliokuwa wamekufa miaka mingi iliyopita kisha wale ambao wangekufa baada ya kurudi kwa Bwana.)
Mt. 25:31-33: “Wakati Mwana wa binadamu atakapofika katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu. Na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu, mmoja kutoka kwa mwenzake, kama vile mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi. Naye atawaweka kondoo kwenye mkono wake wa kuume, lakini mbuzi kwenye mkono wake wa kushoto.”
2 The. 1:7-9: “Kwenu ninyi mnaopata dhiki, kitulizo pamoja nasi wakati wa ufunuo wa Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika zake wenye nguvu katika mwali wa moto, anapoleta kisasi juu ya wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu. Watu hao watahukumiwa adhabu ya uharibifu wa milele kutoka mbele ya Bwana na kutoka kwenye utukufu wa nguvu zake.”
Luka 23:42, 43: “Naye [yule mtenda-maovu mwenye huruma aliyetundikwa pamoja na Yesu] akaendelea kusema: ‘Yesu, unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.’ Naye akamwambia: ‘Kwa kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja nami katika Paradiso.’” (Chini ya utawala wa Yesu, dunia yote itakuwa Paradiso; wafu walio katika kumbukumbu ya Mungu watafufuliwa na kupewa nafasi ya kupata uzima mkamilifu duniani milele.)
Ona pia ukurasa wa 284-289, chini ya kichwa, “Siku za Mwisho.”
-
-
Kusema kwa LughaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kusema kwa Lugha
Maana: Uwezo wa pekee ambao wanafunzi fulani walipewa katika kutaniko la kwanza la Kikristo kupitia roho takatifu uliowawezesha kuhubiri au kumtukuza Mungu katika lugha nyingine.
Je, Biblia inasema wote walio na roho ya Mungu ‘wangesema kwa lugha’?
1 Kor. 12:13, 30: “Kwa kweli kwa roho moja sote tulibatizwa katika mwili mmoja . . . Je, wote wana zawadi za maponyo? Je, wote husema kwa lugha?” (Ona pia 1 Wakorintho 14:26.)
1 Kor. 14:5: “Basi ningependa ninyi nyote mseme kwa lugha, lakini napendelea zaidi kwamba mtoe unabii. Kwa kweli, yeye anayetoa unabii ni mkubwa kuliko yeye anayesema kwa lugha, isipokuwa, kwa kweli, yeye atafsiri, ili kutaniko lijengwe.”
Mtu akisema kwa maneno ya kusisimuka katika lugha ambayo hajapata kujifunza kamwe, je, hilo linaonyesha kwamba ana roho takatifu?
Je, uwezo wa ‘kusema kwa lugha’ unaweza kutokana na chanzo kingine isipokuwa Mungu wa kweli?
1 Yoh. 4:1: “Wapendwa, msiamini kila neno lililoongozwa na roho [“kila roho,” UV, ZSB], lakini yajaribuni maneno yaliyoongozwa na roho ili kuona kama yanatokana na Mungu.” (Ona pia Mathayo 7:21-23; 2 Kor. 11:14, 15.)
Kati ya wale ‘wanaosema kwa lugha’ leo ni Wapentekoste na Wabaptisti, pia Wakatoliki, Waepiskopali, Wamethodisti, Walutheri, na Wapresibiteri. Yesu alisema kwamba roho takatifu ‘itawaongoza wanafunzi wake ndani ya kweli yote.’ (Yoh. 16:13) Je, wafuasi wa kila moja ya dini hizo wanaamini kwamba wengine ambao pia ‘husema kwa lugha’ wanaongozwa katika “kweli yote”? Hilo lingewezekanaje, kwa kuwa wao wote hawapatani? Ni roho gani inayowawezesha ‘kusema kwa lugha’?
Taarifa ya pamoja iliyotolewa na Fountain Trust na Church of England Evangelical Council ilikiri hivi: “Sisi tunajua pia kwamba mambo kama hayo yanaweza kutukia kwa nguvu za uvutano wa kifumbo/roho waovu.” (Gospel and Spirit, Aprili 1977, kilichochapishwa na Fountain Trust na Church of England Evangelical Council, uku. 12) Kitabu Religious Movements in Contemporary America (kilichohaririwa na Irving I. Zaretsky na Mark P. Leone, kikimnukuu L. P. Gerlach) kinasema kwamba huko Haiti ‘kusema kwa lugha’ ni tabia ya dini za Kipentekoste na dini za Kichawi.—(Princeton, N.J.; 1974), uku. 693; ona pia 2 Wathesalonike 2:9, 10.
Je, ‘kusema kwa lugha’ kunakofanywa leo kunafanana na kule kwa Wakristo wa karne ya kwanza?
Katika karne ya kwanza, zawadi za kimuujiza za roho, kutia ndani uwezo wa ‘kusema kwa lugha,’ zilithibitisha kwamba kibali cha Mungu kilikuwa kimeondolewa kutoka katika ibada ya Wayahudi na kupewa kutaniko la Kikristo lililoanzishwa karibuni. (Ebr. 2:2-4) Kwa kuwa kusudi hilo lilitimizwa katika karne ya kwanza, je, ni lazima kuthibitisha jambo hilo tena na tena katika siku zetu?
Katika karne ya kwanza, uwezo wa ‘kusema kwa lugha’ ulisaidia kusonga mbele kwa kazi ya kutoa ushahidi kwa watu wa mataifa yote, kazi ambayo Yesu alikuwa amewaagiza wafuasi wake wafanye. (Mdo. 1:8; 2:1-11; Mt. 28:19) Je, wale ‘wanaosema kwa lugha’ wanatumia uwezo huo leo kufanya kazi hiyo?
Katika karne ya kwanza, Wakristo ‘waliposema kwa lugha,’ mambo waliyosema yalikuwa na maana kwa watu waliojua lugha hizo. (Mdo. 2:4, 8) Leo, je, si kweli kwamba ‘kusema kwa lugha,’ mara nyingi huhusisha kupaaza sauti na kusema maneno yasiyoeleweka?
Biblia inaonyesha kwamba katika makutaniko ya karne ya kwanza, watu wawili au watatu tu ndio walioruhusiwa ‘kusema kwa lugha’ katika mkutano mmoja; walipaswa kufanya hivyo “zamu kwa zamu,” na kama hakukuwa na mtu wa kutafsiri, walipaswa kunyamaza. (1 Kor. 14:27, 28, UV) Je, hivyo ndivyo inavyofanywa leo?
Ona pia ukurasa wa 243, 244, chini ya kichwa, “Roho.”
Je, inawezekana kwamba roho takatifu inawaelekeza watu wafanye matendo makuu yanayopita yale yaliyotajwa katika Maandiko?
2 Tim. 3:16, 17: “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu, ili mtu wa Mungu awe na uwezo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.” (Mtu akidai ana ujumbe ulioongozwa na roho ambao unapingana na ufunuo uliotolewa na roho ya Mungu kupitia Yesu na mitume wake, je, inawezekana kwamba ujumbe huo umetokana na chanzo kimoja?)
Gal. 1:8: “Hata ikiwa sisi au malaika kutoka mbinguni tungewatangazia ninyi kuwa habari njema jambo fulani kupita [“tofauti na,” BHN] lile tulilowatangazia ninyi kuwa habari njema, mtu huyo na alaaniwe.”
Je, maisha ya wafuasi wa dini zinazokubali ‘kusema kwa lugha’ yanaonyesha kwamba wana roho ya Mungu?
Wakiwa kikundi, je, wanaonyesha matunda ya roho kama vile upole na kujizuia kwa njia yenye kutokeza? Je, watu wanaohudhuria mikutano yao ya ibada wanaona sifa hizo upesi?—Gal. 5:22, 23.
Je, wao kweli “si sehemu ya ulimwengu”? Kwa sababu ya hilo je, wanajitoa kikamili kwa Ufalme wa Mungu au wanajiingiza katika mambo ya siasa za ulimwengu? Je, wamedumu bila hatia ya damu wakati wa vita? Wakiwa kikundi, je, wana sifa nzuri kwa sababu ya kuepuka mwenendo usio wa adili wa ulimwengu?—Yoh. 17:16; Isa. 2:4; 1 The. 4:3-8.
Je, Wakristo wa kweli leo wanatambuliwa kwa uwezo wa ‘kusema kwa lugha’?
Yoh. 13:35: “Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mkiwa na upendo kati yenu wenyewe.”
1 Kor. 13:1, 8: “Nikisema kwa lugha za wanadamu na za malaika lakini sina upendo, nimekuwa chombo cha shaba
-