Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • na kur. 28-31
  • Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu
  • Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sisi Tunaweza Kulitakasa Jina la Mungu Namna Gani?
  • Jinsi Linavyokuhusu Wewe
  • Baraka Zinazotokana na Kulijua Jina la Mungu
  • Jinsi ya Kujua Jina la Mungu
    Amkeni!—2004
  • Jina la Mungu na Lako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Liheshimu Jina Kuu La Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Jina la Mungu
    Amkeni!—2017
Pata Habari Zaidi
Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
na kur. 28-31

Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu

“KILA anayeita juu ya jina la Yehova ataokolewa.” (Warumi 10:13, NW) Kwa maneno hayo mtume Paulo alikazia jinsi ilivyo lazima kwetu kulijua jina la Mungu. Maneno yake yanatukumbusha ulizo letu la kwanza: Kwa nini Yesu aliweka ‘kutakaswa,’ au ‘kutukuzwa,’ kwa jina la Mungu katika mwanzo wenyewe wa Sala ya Mfano yake, mbele ya mambo mengine mengi sana ya maana? Ili tuelewe hilo, tunahitaji kufahamu vizuri zaidi kidogo maana ya neno kutakasa.

Kwanza, ‘kutakasa’ maana yake hasa ni nini? Kihalisi maana yake ni: “kufanya takatifu.” Lakini tayari jina la Mungu ni takatifu, sivyo? Bila shaka. Tunapolitakasa jina la Mungu, hatulifanyi kuwa takatifu zaidi ya lilivyo. Bali tunalitambua kuwa takatifu, tunalitenga, tunaliheshimu kwa heshima ya juu zaidi sana. Tunaposali jina la Mungu litakaswe, tunatazamia wakati uumbaji wote utakapoliheshimu kuwa takatifu.

Pili, hasa kinachodokezwa na neno “jina” ni nini? Tumeona kwamba Mungu ana jina, Yehova, na kwamba jina lake linaonekana katika Biblia mara maelfu. Pia, tumezungumza umaana wa kurudisha jina hilo mahali linapopasa kuwa katika maandishi ya Biblia. Jina hilo lisipokuwapo hapo, maneno haya ya mtunga zaburi yanaweza kutimizwaje: “Nao watatumaini kwako, wakujuao jina lako; kwani huwaati wakutakao wewe, Jehova.”—Zaburi 9:10, OTSWMSA.

Lakini, je! ‘kulijua jina la Mungu’ ni kupata maarifa ya akili tu kwamba katika Kiebrania jina la Mungu ni YHWH, au Yehova katika Kiswahili? Sivyo, kunamaanisha zaidi ya hivyo. Musa alipokuwa katika Mlima Sinai, “Jehova akashuka ndani ya hilo wingu, na kusimama mbele yakwe [Musa] huko, na kulitangaza jina la Jehova.” Kutangazwa huko kwa jina la Yehova kulitia ndani nini? Masimulizi ya sifa zake: “Jehova, Jehova, Mwenyiezi Mngu, Mwenyi kujawa ni huruma, Mwenyi fadhili, Mpole wa hasira, Mwingi wa ihisani na kweli.” (Kutoka 34:5, 6, OTSWMSA) Tena, muda mfupi kabla ya kufa kwake, Musa aliwaambia Waisraeli hivi: “Talitangaza jina la Jehova.” Mambo gani yalifuata? Ni kutajwa kwa baadhi ya sifa Zake bora, kisha kurudiwa kwa mambo ambayo Mungu alikuwa ametimizia Waisraeli kwa ajili ya jina Lake. (Kumbukumbu la Torati 32:3-43, OTSWMSA) Kwa sababu hiyo, kulijua jina la Mungu maana yake ni kujifunza mambo ambayo jina hilo linawakilisha kisha kumwabudu yule Mungu aliye nalo.

Kwa kuwa Yehova ameshirikisha jina lake na sifa zake, makusudi na matendo yake, tunaweza kuona ni kwa nini Biblia inasema kwamba jina la Mungu ni takatifu. (Mambo ya Walawi 22:32) Ni lenye utukufu mwingi, ni kuu, ni lenye kutia woga na liko juu kadiri isiyofikika. (Zaburi 8:1; 99:3; 148:13) Ndiyo, jina la Mungu ni zaidi ya kibandiko tu cha utambulisho. Linamwakilisha yeye kuwa mtu. Halikuwa jina la muda tu la kutumiwa kwa wakati fulani kisha mtajo kama vile “Bwana” utumiwe badala yalo. Yehova mwenyewe alimwambia Musa hivi: “Jehova . . . hili ndilo jina langu milele, nalo la kunikumbukia hata vizazi vyote ni hilo.”—Kutoka 3:15, OTSWMSA.

Hata ajaribu namna gani, mwanadamu hataliondoa kabisa kamwe litoke katika dunia. “‘Tangu kupanda kwa jua hata kwenye kushuka kwalo jina langu litakuwa kuu kati ya mataifa, na katika kila mahali moshi wa dhabihu utafanywa, toleo litafanywa kwa jina langu, hata zawadi safi; kwa sababu jina langu litakuwa kuu kati ya mataifa,’ Yehova wa majeshi amesema.”—Malaki 1:11; Kutoka 9:16; Ezekieli 36:23, NW.

Kwa sababu hiyo, kutakaswa kwa jina la Mungu ni kwa maana zaidi sana kupita na suala jinginelo lote. Makusudi yote ya Mungu yanahusianishwa na jina lake. Matatizo ya wanadamu yalianza wakati Shetani alipochafua mara ya kwanza jina la Yehova kwa kumwita Yeye mwongo na asiyefaa kutawala jamii ya kibinadamu. (Mwanzo 3:1-6; Yohana 8:44) Jina la Mungu litakapoondolewa lawama vya kufaa ndiyo hapo tu wanadamu watakapofurahia kikamili kitulizo cha matokeo yenye msiba ya uwongo wa Shetani. Ndiyo sababu Wakristo wanasali kwa bidii sana jina la Mungu litakaswe. Lakini kuna mambo wanayoweza kufanya, pia, ili walitakase.

Sisi Tunaweza Kulitakasa Jina la Mungu Namna Gani?

Njia moja ni kuzungumza na wengine juu ya Yehova na kuelekeza kwenye Ufalme wake mikononi mwa Kristo Yesu kuwa ndio tumaini pekee la wanadamu. (Ufunuo 12:10) Wengi wanafanya hivyo, kwa utimizo wa kisasa wa maneno haya ya unabii wa Isaya: “Katika siku hiyo mtasema, Mshukuruni Jehova, linganani jina lakwe, tangazani habari za vitendo vyakwe katika hizo kabila za watu, semani ya kwamba jina lakwe limetukuka sana. Mwimbieni Jehova; kwani amevitenda vitendo vikuu mno: na habari hizi zienee katika dunia yote.”—Isaya 12:4, 5, OTSWMSA.

Njia nyingine ni kutii sheria na amri za Mungu. Yehova aliliambia taifa la Israeli hivi: “Mtayashika maagizo yangu, na kuyafanya: mimi ni Jehova. Nanywi msilitungue jina langu takatifu; lakini ntatakaswa mimi katika hao wana wa Isiraeli: mimi ni Jehova niwatakasae nyinywi.”—Mambo ya Walawi 22:31, 32, OTSWMSA.

Kushika kwa Waisraeli Torati ya Yehova kulitakasa jina lake namna gani? Torati hiyo ilitolewa kwa Waisraeli kwa kutegemea jina lake. (Kutoka 20:2-17) Kwa sababu hiyo, walipoishika Torati, walikuwa wakionyesha heshima na staha inayolifaa jina hilo. Zaidi ya hayo, jina la Yehova lilikuwa juu ya Waisraeli wakiwa taifa. (Kumbukumbu la Torati 28:10; 2 Mambo ya Nyakati 7:14) Walipotenda vya kufaa, hiyo ilimletea sifa, kama vile mtoto anayetenda kwa kufaa anavyomletea babaye heshima.

Kwa upande mwingine, Waisraeli walipokosa kushika Torati, walilichafua jina lake. Hivyo, dhambi kama vile kuzitolea sanamu dhabihu, kuapa uwongo, kudhulumu maskini na kufanya uasherati zinaelezwa katika Biblia kuwa ni ‘kulinajisi jina la Mungu.’—Mambo ya Walawi 18:21; 19:12; Yeremia 34:16; Ezekieli 43:7.

Hali moja na hiyo, Wakristo wamepewa amri katika jina la Mungu. (Yohana 8:28) Nao, pia, wanashirikiana na watu ‘kwa ajili ya jina la Yehova.’ (Matendo 15:14) Kwa sababu hiyo, Mkristo anayesali kwa unyofu wa moyo, akisema, “Jina lako litukuzwe” atalitakasa jina hilo katika maisha yake mwenyewe kwa kuzitii amri zote. (1 Yohana 5:3) Hiyo ingetia pia kuzitii amri alizotoa Yesu, Mwana wa Mungu, ambaye nyakati zote alimtukuza Baba yake.—Yohana 13:31, 34; Mathayo 24:14; 28:19, 20.

Usiku kabla ya kuuawa kwake, Yesu alikazia umaana wa jina la Mungu kwa Wakristo. Baada ya kumwambia Babaye hivi: “Nimefanya jina lako lijulikane kwao na nitalifanya lijulikane,” anaendelea kueleza, “ili kwamba ule upendo ulionipenda nao upate kuwa ndani yao na mimi katika kuungana nao.” (Yohana 17:26, NW) Kujifunza kwa wanafunzi jina la Mungu kulitia ndani kujua kwao binafsi upendo wa Mungu. Yesu alikuwa amefanya iwezekane kwao kupata kumjua sana Mungu kuwa Baba yao mwenye upendo.—Yohana 17:3.

Jinsi Linavyokuhusu Wewe

Penye mkutano wa karne ya kwanza wa mitume wa Kikristo na wanaume wazee katika Yerusalemu, mwanafunzi Yakobo alisema: “Simeoni ametueleza jinsi Mungu hapo kwanza alivyowaangalia Mataifa ili achague watu katika hao kwa ajili ya jina lake.” Ikiwa wewe unashindwa kutumia au kulichukua jina hilo, je! ungeweza kutambuliwa kuwa mmoja wa wale ambao Mungu anachagua wawe ‘watu kwa ajili ya jina lake’?—Matendo 15:14.

Ijapokuwa wengi hawataki kulitumia jina Yehova, na watafsiri wengi wa Biblia wanaliondoa katika tafsiri zao, mamilioni ya watu kuzunguka ulimwengu wamelikubali kwa furaha pendeleo la kuchukua jina la Mungu, la kulitumia si katika ibada tu bali katika usemi wa kila siku, na la kulitangaza kwa wengine. Kama mtu angesema na wewe juu ya Mungu wa Biblia, akatumia jina Yehova, ungemshirikisha na kikundi gani cha kidini? Kuna kikundi kimoja tu katika ulimwengu kinachotumia kwa ukawaida jina la Mungu katika ibada yao, kama vile waabudu wake wa nyakati za kale walivyofanya. Hao ni Mashahidi wa Yehova.

Jina lenye msingi wa Biblia Mashahidi wa Yehova linatambulisha Wakristo hao kuwa ‘watu kwa ajili ya jina la Mungu.’ Wanaona fahari ya kulichukua jina hilo, kwa maana ndilo Yehova Mungu mwenyewe aliwapa waabudu wake wa kweli. Katika Isaya 43:10, The Old Testament in Swahili (Mombasa), tunasoma hivi: “Nyinywi mu mashahidi yangu anena Jehova, na mtumishi wangu ambae nimemtagua.” Mungu alikuwa akizungumza juu ya nani hapa? Ebu angalia baadhi ya mistari inayotangulia.

Katika mistari 5 mpaka 7 ya sura iyo hiyo, Isaya anasema: “Usiogope; maana mimi ni pamoja nawe; nitaleta wazao wako toka mashariki, nitakukusanya toka magharibi; nitaiambia kaskazi, Toa; nayo kusi, Usizuie; waleteni wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia. Kila mmoja aliyeitwa kwa jina langu, niliyemwumba kwa ajili ya utukufu wangu; mimi nimemwumba, naam, mimi nimemfanya.” (Union Version) Wakati wetu huu, mistari hiyo inahusu watu wa Mungu mwenyewe ambao amekusanya kutoka mataifa yote waje wamsifu yeye na kuwa mashahidi wake. Hivyo jina la Mungu halimtambulishi yeye tu bali pia linasaidia kutambulisha watumishi wake wa kweli duniani leo.

Baraka Zinazotokana na Kulijua Jina la Mungu

Yehova analinda wale wanaolipenda jina lake. Mtunga zaburi alisema: “Kwa kuwa amekaza kunipenda nitamwokoa; na kumweka palipo juu, kwa kuwa amenijua Jina langu.” (Zaburi 91:14) Pia yeye anawakumbuka: “Ndipo hao waliokuwa wamcha Jehova wakazungumza wao kwa wao: yeye Jehova nae akatega sikio, tena chuo cha ukumbusho kiliandikwa mbele yakwe, kwa ajili ya hao waliomcha Jehova, na kulifikiri jina lakwe.”—Malaki 3:16, OTSWMSA.

Hivyo, zile faida zinazotokana na kulijua na kulipenda jina la Mungu si za maisha haya tu. Yehova amewaahidi wanadamu wenye utii uzima wa milele kwa furaha katika dunia-Paradiso. Daudi aliongozwa na roho ya Mungu kuandika hivi: “Watenda mabaya wenyewe watakatiliwa mbali, lakini wale wanaomtumainia Yehova ndio ambao wataimiliki dunia. Lakini wapole wenyewe wataimiliki dunia, nao watafurahia kikamilifu sana wingi wa amani.”—Zaburi 37:9, 11, NW.

Jambo hilo litawezekanaje? Yesu alitoa jibu. Katika Sala ya Mfano ile ile ambayo katika hiyo alitufundisha kusali, “Jina lako litakaswe,” yeye aliongeza kusema: “Ufalme wako uje. Mapenzi yako yatukie, kama mbinguni, pia duniani.” (Mathayo 6:9, 10, NW) Ndiyo, Ufalme wa Mungu mikononi mwa Yesu Kristo utalitakasa jina la Mungu na pia utaleta hali nzuri kwenye dunia hii. Utaondoa kabisa uovu na kuondoa vita, uhalifu, njaa kuu, magonjwa na kifo.—Zaburi 46:8, 9; Isaya 11:9; 25:6; 33:24; Ufunuo 21:3, 4.

Unaweza kufurahia uzima wa milele chini ya Ufalme huo. Jinsi gani? Kwa kumjua Mungu. “Hii ndiyo maana ya uzima wa milele, wapate maarifa ya kukujua wewe, Mungu wa kweli mmoja tu, na ya yeye uliyemtuma, Yesu Kristo.” (Yohana 17:3, NW) Mashahidi wa Yehova watapendezwa kukusaidia uyatwae maarifa yenye kutoa uzima.—Matendo 8:29-31.

Inatumainiwa kwamba habari iliyo katika broshua hii imekusadikisha kujua kwamba Muumba analo jina la kibinafsi ambalo ni lenye bei sana kwake. Limepaswa liwe lenye bei sana kwako pia. Na upate kuufahamu umaana wa kulijua na kulitumia jina hilo, hasa katika ibada.

Tena na uazimie kusema kama nabii Mika alivyosema kwa ujasiri karne nyingi zilizopita: “Kwani watu wa kabila zote watakwenenda killa mmoja katika jina la mngu wakwe, swiswi naswi tutakwenda katika jina la Jehova yeye Mwenyiezi Mngu wetu siku zote hata milele.”—Mika 4:5, OTSWMSA.

[Blabu katika ukurasa wa 28]

‘Kulijua jina la Mungu’ kunamaanisha zaidi ya kuwa na maarifa ya kichwani tu kwamba jina lake ni Yehova

[Blabu katika ukurasa wa 30]

Jina la Yehova ni lenye ‘utukufu mwingi, ni kuu, ni lenye kutia woga na liko juu kadiri isiyofikika.’ Makusudi yote ya Mungu yanashirikishwa na jina lake

[Sanduku katika ukurasa wa 29]

Katika makala iliyotokea katika Anglican Theological Review (Oktoba 1959), Dakt. Walter Lowrie alikazia uhitaji wa kulijua jina la Mungu. Aliandika hivi: “Katika uhusiano wa kibinadamu ni jambo la maana sana kulijua jina la kipekee, jina la kibinafsi, la mtu tunayependa, tunayesema naye, au hata juu ya mtu tunayesema juu yake. Ndivyo ilivyo sawasawa katika uhusiano wa mwanadamu na Mungu. Mwanadamu asiyemjua Mungu kwa jina hamjui yeye kweli kweli kuwa mtu, hana ujuano wa kusema naye (unaomaanishwa kwa njia ya sala), na hawezi kumpenda, ikiwa anamjua yeye kuwa msukumo tu usio na utu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki