Wimbo 139
Zisikilizeni Habari za Ufalme
1. Habari za Ufalme sikilizeni
Yesu asema: ‘Ninatawala.
Karibuni adui ataondoshwa;
Sasa mufumo wake ukimbieni.’
(Korasi)
2. Kwa mashahidi Yehova anaita:
“Enyi wapole, Shangilieni.
Yesu kuonyesha nguvu karibuni.
Zitoweke shida, uchungu, huzuni.”
(Korasi)
3. Wasikilizao ni wenye furaha
Wenye kusema: ‘Nitamutii’
Mungu huwahifadhi waaminifu
Ufalme wake wanatafuta kwanza.
(KORASI)
Waovu waache njia mbaya,
Na wenye madhara mawazo yao.
Warudi kwa Mungu wa rehema,
Ambaye husamehe sana.