Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 7/15 kur. 15-20
  • Toa Uangalifu Daima kwa Fundisho Lako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Toa Uangalifu Daima kwa Fundisho Lako
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kusitawisha Eneo “Jipya”
  • Toa Ushuhuda Kikamili
  • Wale Wanaolalamika
  • Kushinda Tatizo la Ubaridi
  • Ione Ikimalizika
  • Usichoke Kutenda Yaliyo Mema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Uwe Mwenye Matokeo Katika Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Kutoa Habari Njema—Katika Eneo Lenye Kufanyiwa Kazi Mara Nyingi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Tumia Ile Kanuni Bora Katika Huduma Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 7/15 kur. 15-20

Toa Uangalifu Daima kwa Fundisho Lako

“Toa uangalifu daima kwa wewe mwenyewe na kwa fundisho lako. Endelea katika vitu hivyo, kwa kuwa kwa kufanya hivyo utaokoa wote wawili wewe mwenyewe na wale wanaosikiliza wewe.”​—TIMOTHEO 4:16, NW

1 Kwa nini huu sio wakati wa sisi kupunguza mwendo katika kazi yetu ya kuhubiri Ufalme?

SASA Yehova anaharakisha kukusanywa kwa watu wa aina ya kondoo. Kwa kweli, basi, huu si wakati wa watu wake kupunguza mwendo katika kazi yao ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi. (Isaya 60:8, 22; Mathayo 24:14; 28:19, 20) Tunahitaji kutenda kulingana na kusudi ya yale ambayo Mungu anafanya katika wakati wetu. Mwisho unapokaribia zaidi, tutakuwa tunawarudia majirani zetu mara nyingi zaidi. Kweli kweli, utendaji wa ushuhuda ulioongezeka unaofanywa na wahubiri na mapainia wengi zaidi sasa unaamsha shamba la ulimwengu. Na mwendo wa kukusanya huku kwa shangwe utakua.​—Isaya 60:11; linganisha Zaburi 126:5, 6.

2. (a) Kulingana na Isaya 40:28-31, ni chanzo kipi cha nishati ambacho sisi tunaweza kuchota uthabiti unaohitajiwa ili kumaliza kazi ya kuhubiri Ufalme? (b) Kuna sababu nzuri gani ya kutoa uangalifu zaidi kuelekea huduma yetu wakati huu?

2 Badala ya kuanguka katika hisia yo yote ya ‘kuchoka’ kwa sababu eneo fulani linaenezwa mara kwa mara, tunapaswa kung’amua kwamba huu ndio wakati wetu sisi kusali kwa Yehova kwa ajili ya “nishati msukumo” inayohitajiwa kumaliza kazi hii. (Isaya 40:28-31; 1 Yohana 5:14, NW) Kweli, mamilioni ya “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” tayari wamekusanywa. Lakini kitu fulani ambacho wakati mmoja kilikuwa chenye mafanikio katika kuwasaidia watu fulani huenda kisiwe tena chenye matokeo katika kuwasaidia watu wengine ambao wangali katika maeneo yetu. (Ufunuo 7:9, 10; Yohana 10:16) Kwa sababu hiyo, ubora wa huduma yetu unahitaji uangalifu zaidi.

3. Idili mpya inawezaje kuingizwa katika huduma yetu ya shambani?

3 Kwa kupiga moyo konde tena, tunaweza kukaza fikira kufanyia maendeleo matokeo yetu katika huduma. Hilo linaweza kuupa utumishi wetu wa shambani idili mpya. Lakini jambo hilo linaweza kufanywa kwa jinsi gani? Kwa ‘kutoa uangalifu daima kwetu wenyewe na kwa fundisho letu,’ si kwa kufanya huduma yetu kama kawaida tu. (1 Timotheo 4:16, NW) Midomo yetu inapasa kutoa zaidi ya “dhabihu ya sifa” ya haraka haraka tu. (Waebrania 13:15) Tunapaswa kuwa stadi katika kazi yetu. (Mithali 22:29) Basi, kinachohitajiwa ni kufanyia eneo letu kazi kwa ustadi. Hapa pana pande fulani za huduma yetu ambazo tunahitaji ‘kutoa uangalifu daima.’

Jinsi ya Kusitawisha Eneo “Jipya”

4. Ni katika njia gani tunaweza kusitawisha eneo “jipya” katika ule mgawo wetu wa kundi?

4 Acheni tuangalie hali hii katika njia yenye mafaa. Katika sehemu nyingi, hakuna eneo jipya wala lisilofanyiwa kazi mara nyingi. Kwa hivyo basi mbona msisitawishe eneo “jipya” katika mgawo wa kundi? Jinsi gani? Basi, tunapotembea mara kwa mara, hatuwezi kutenda kana kwamba hatujawahi kutembelea maskani hayo wakati mwingine kwa kusema tu yale ambayo tumesema kwa kawaida milangoni. Yaelekea, kwa vyo vyote mwenye nyumba atatung’amua ikiwa tumeeneza eneo hilo kwa kurudia-rudia. Kitabu Reasoning From the Scriptures kinatoa zaidi ya matangulizi 40 ambayo tunaweza kutumia katika huduma yetu. Lazima tuyatayarishe vizuri kama kitu kipya na chenye kuvutia kwa kuyaunganisha na mambo yanayopendeza ya karibuni na ya mahali petu. Badala ya kuhisi sikitiko kuhusu kutembea kwetu mara kwa mara, tunahitaji kuwa na mwelekeo chanya na kufanya eneo letu liwe “jipya” kwa kutoa utoaji ulio bora. Lakini je! hili litasaidia ikiwa wenye nyumba si wenye urafiki?

5. (a) Tunaweza kufanyaje mwelekeo usio wa kirafiki uliotangulia kuonyeshwa utufaidi? (b) Wewe umepata mambo gani yanayotokeza matokeo mazuri mahali penu? (c) Kwa nini kusikiliza na kusifu kwa kufuata haki kunasaidia?

5 Kujua mwelekeo wa wakati uliopita wa mwenye nyumba unaweza kufanya tuwe na hisia hasi kuhusu kutembelea tena. Lakini mbona usifanye maarifa hayo yakufaidi? Jinsi gani? Labda kwa kuyataja kijuu-juu kwanza kisha kuendeleza yale yaliyosemwa wakati wa ziara iliyopita. Huenda ukasema: “Habari ya asubuhi, Bw. Harris!” Ikiwa linaonekana kuwa jambo linalofaa unaweza kuongezea hivi: “Umeshindaje?” Kisha unaweza kusema: “Nilipokuwa hapa juma lililopita, uliniambia kwamba kanisa lako lilishughulikia mahitaji yako yote ya kiroho na kwamba wewe ni mshiriki anayejihusisha sana nalo. Nikiwa jirani ambaye anachukua dini kwa uzito pia ebu niulize kanisa lako linasema nini juu ya tumaini la kuokolewa katika kizazi hiki cha nyukilia?” Kisha acha akueleze. Msifu mwenye nyumba mahali ambapo unaona unaweza kufanya hivyo kwa ufuataji haki. Kumsikiliza na kumsifu huenda kukabadili mwelekeo wake. Mara nyingi, watu watakubali kutembelewa tena ikiwa wao wenyewe wanaweza kuzungumza. Bila shaka, utataka kurekebisha ujumbe wako kulingana na yale ambayo mwenye nyumba anasema.

6. (a) Tunaweza kuwazoezaje wenye nyumba watutazamie tuzuru kwa ukawaida? (b) Ni maneno gani ya msingi yanayoweza kutusaidia tufanikiwe? (c) Ni mambo gani yanayotokeza matokeo mazuri mahali penu?

6 Kwa yale ambayo unasema, unaweza kuwazoeza wenye nyumba watutazamie tuzuru kwa ukawaida. Jaribu kusema: “Habari, Bi. Fredericks! U hali gani leo? Katika ziara hii kwa majirani wetu, tunazungumzia . . .” Au unaweza kusema: “Habari ya asubuhi! Tunafanya ziara zetu za kila juma. Ni vizuri kuwa hapa tena. Majirani wako wamefurahia habari mpya ambayo tunazungumza katika ziara hii.” Kisha endelea. Jambo hilo linafanya eneo liwe “jipya” kwako pia. Maneno yenyewe yanaweza kutofautiana kidogo katika bara lako, Iakini hii inatoa wazo kuu. Mbona usiitumie kadiri uwezavyo kwa faida yako?

7. (a) Wakati wa kuondoka, Mashahidi fulani fulani wanatayarishaje mwenye nyumba kwa ajili ya ziara nyingine? (b) Kwa habari hii, ni mambo gani yanayotokeza matokeo mazuri mahali penu?

7 Ili kumtayarisha mwenye nyumba kwa ajili ya ziara itakayofuata, Mashahidi fulani wana mafanikio kwa kumalizia hivi: “Tunatazamia kukutembelea tena karibuni.” Kwa wale ambao hawakutaka kuzungumza nawe mara ya kwanza, unaweza kusema hivi: “Nimefurahia mazungumzo yetu. Kwa kweli ulisema maneno fulani mazuri. Hii ilichukua dakika chache, lakini angalau hatukuongea habari mbaya, ambazo tunaweza kusikia wakati wo wote. Hakika mazungumzo yalikuwa yenye kujenga.” Bila shaka, utasitawisha njia nyingine zinazofaa za kuzungumza na wenye nyumba. Kwa vyo vyote, kwa maneno yanayofaa, utoaji ulio bora, na urafiki, jitahidi kusaidia halaiki wasichukizwe na ziara zetu za kawaida.

Toa Ushuhuda Kikamili

8, 9. Ni madokezo gani yanayotolewa kwa kutafuta-tafuta wanaostahili kwa ukamili?

8 Jambo jingine ambalo tunaweza kutoa uangalifu kwalo ambalo litaendeleza idili yetu ni kutafuta-tafuta kwa ukamili zaidi wale wanaostahili. (Matendo 8:25; 20:24) Mathalani, huenda ndugu akaomba mume wa nyumba aje ikiwa mke au mtoto anakuja mlangoni wakati wa miisho juma au jioni. Pengine mke ndiye tumezungumza naye mara nyingi. Kwa hiyo tunaweza kuanza upya na jamaa kwa kuzungumza na kichwa cha jamaa. Tunaweza kurekebisha ujumbe umfae yeye, tukisema mambo kama vile, “Unafikiri ni nini kitakachohakikishia jamaa yako wakati ujao wenye furaha?” au, “Angalia jinsi Biblia inavyoendeleza umoja wa jamaa.” Sifu mwanamume huyo kwa maoni mazuri ambayo huenda akatoa.

9 Njia nyingine ya kupata eneo “jipya” ni kutafuta washiriki wengine wa jamaa wanaoishi katika nyumba ile ile​—nyanya, mpwa au binamu anayeenda shule, shemeji wa kike anayefanya kazi wakati wa juma. Limekuwa jambo lenye mafaa pia kuangalia ni mita ngapi za stima au sanduku za posta zilizopo katika makao. Hii inaweza kuonyesha mahali ambapo watu wametengeneza upya orofa ya chini, orofa ya juu kabisa, au sehemu nyingine ya kupangisha. Jaribu kuwafikia wale ambao wamepanga​—wanafunzi, wafanya kazi waseja, wajane, na wengine. Jambo hili pia linasaidia kupanua eneo linalopatikana.

10. Ni njia gani nyingine ya kupanua eneo letu la nyumba kwa nyumba, na wengine wamefanya nini ili kuwafikia wafanya kazi wa usiku?

10 Njia nyingine zaidi ya kupanua eneo la nyumba kwa nyumba ni kwa kuliacha lipumzike nyakati nyingine tunaposhiriki katika sehemu nyingine za huduma yetu. Kwa mambo mbalimbali, tunaweza kufanyia eneo kazi tukitoa moja kwa moja funzo la nyumbani la jamaa la Biblia bure. Watu fulani ambao hawapatikani nyumbani tunapozuru wanaweza kupatikana mahali pao pa biashara au pa kazi. Na kutoa ushuhuda katika maeneo ya kibiashara kunaweza kuwa kwenye matokeo sana. Wengine wa watu hawa wanaweza kufikiwa ikiwa tunatoa ushuhuda barabarani wakati unaofaa, masaa yenye matokeo. Katika Kanada, mapainia wamekuwa na matokeo mazuri kutokana na kuwatembelea wafanya kazi wanaofanya kazi usiku wote kwenye vituo vya petroli, maduka, na mahoteli ambapo karani hawana kazi nyingi wakati huo na mara nyingi wanathamini kuwa na kitu cha kusoma. Bila shaka, akina dada wangehitaji kuepuka sehemu fulani-fulani saa za usiku-usiku.

11. (a) Mashahidi fulani wanafanya nini mahali ambapo wengi hawapatikani nyumbani wakati wa ziara ya kwanza? (b) Juhudi katika kurudia wasiopatikana nyumbani inaweza kuathirije eneo letu na kukiwa na matokeo gani katika huduma?

11 Namna gani wale ambao hawako nyumbani tunapozuru? Hapa tena, lazima tuwe kamili. Mashahidi fulani wanatumia maandishi yao ya mlango kwa mlango yaliyotunzwa vizuri baada tu ya kazi yao ya nyumba kwa nyumba na kurudia sehemu ambazo watu hawakupatikana nyumbani mapema siku hiyo. Mara nyingi, wenye nyumba wamerudi nyumbani au wafanya kazi wa usiku wameamka kufikia wakati huo. Katika sehemu nyingi, asilimia 50 au zaidi hawamo manyumbani wakati wa mchana. Kwa hiyo kwa kweli tunaweza, kwa matokeo mazuri, kuzidisha maradufu eneo hilo kwa kufanya ziara za wasiopatikana nyumbani saa tofauti-tofauti mpaka tupate mtu fulani nyumbani. Mapainia na wahubiri wenye ujuzi wanakubali kwamba juhudi katika kufanyia kazi nyumba zisizopatikana watu mara nyingi inatokeza matokeo mazuri kuliko kueneza eneo mara ya kwanza. Kwa kutoa uangalifu kwa upande huu wa huduma yetu inaelekea tutavuna baraka nyingi.​—Mithali 10:22.

Wale Wanaolalamika

12. Tunapaswa kujibizaje wakati watu wanapolalamika kwamba sisi tunazuru mara nyingi mno? Kwa nini?

12 Ni jambo gani linaloweza kuambiwa watu ambao wanalalamika kwamba sisi tunazuru mara nyingi sana? Zaidi ya yote, lazima tuonyeshe ufahamivu. (Mathayo 7:12) Kwao inaonekana kwamba tumerudi haraka sana. Lakini ni vizuri kukumbuka kwamba hata miaka mingi iliyopita watu walikuwa wakisema, ‘Mlikuwa hapa juma lililopita’ hali tulijua vizuri kabisa kwamba ilikuwa miezi sita au zaidi tangu tulipozuru. Mbali na hilo, ziara za mara kwa mara zinaweza kuamsha kupendezwa. Katika Guadeloupe, mwanamume mmoja alimkimbilia Shahidi ili amwambie: “Mimi nimekuchunguza kwa majuma mengi sasa. Kwa kawaida, mimi sisikilizi Mashahidi, lakini ninataka kujua kwa nini mnatembelea watu mara nyingi sana!” Funzo la Biblia jipya lilianzishwa.

13, 14. Wengine wa waitikadi wenzetu wanashughulikiaje mambo wakati wenye nyumba wanapolalamika?

13 Akina ndugu fulani wamewaambia walalamikaji kwa fadhili tarehe yenyewe ya zaira yao ya mwisho na wakatoa magazeti ya karibuni, wakionyesha wazi kwamba makala zinatofautiana na zile zilizokuwa katika majarida ambayo tulikuwa nao wakati wa mwisho tulipozuru. Kwa kusababu pamoja na wenye nyumba hao, tunaweza kusema kwamba pengine wamepokea karatasi-habari na magazeti mengi tangu tulipozuru mara ya mwisho, lakini si sikuzote hayo yamekuwa na habari njema. Tunaweza kueleza kwamba tunaleta habari njema na kwamba ziara zetu si ndefu. Lakini ikiwa mwenye nyumba ana shughuli nyingi, tungeweza kusema: “Ikiwa huu sio wakati unaofaa kusema nawe, nitakuona tutakapozuru tena baada ya juma moja hivi.”

14 Ni jambo gani lingine tunaloweza kusema? Hii inategemea mwelekeo wa mwenye nyumba na heshima ya kawaida inayotazamiwa mahali tunapoishi. Dada mmoja katika Japani anaeleza juu ya ziara zetu za mara kwa mara katika njia hii: ‘Habari za televisheni zitaripoti juu ya mwendo wa kimbunga tena na tena, zikirudia habari hiyo mara kwa mara kwa manufaa ya wale ambao huenda wakawa wamezikosa wakati wa matangazo yaliyotangulia. Jambo hilo linafanywa kwa sababu uhai unahusika. Kurudia ripoti hizo mara kwa mara kunaongezeka tufani hiyo inapokaribia. Kwa hiyo, tufani ya Har–Magedoni inapokaribia, lazima ujumbe wa kuonya utangazwe mara nyingi iwezekanavyo ili kuokoa uhai.’ Bila shaka, tungesema maneno hayo kwa fadhili na kwa weupe wa moyo, tukitumaini kufikia moyo wa msikilizaji.

Kushinda Tatizo la Ubaridi

15. (a) Ni tatizo gani lenye kukua linaloweza kutokea wakati tunapolifanyia eneo letu kazi mara kwa mara? (b) Kwa sababu gani watu fulani ni wenye ubaridi?

15 Ziara zetu zinapoongezeka, tatizo linaloongezeka ni ubaridi ambao tunakabiliana nao mara kwa mara. Lakini tunapochunguza sababu nyingine za ubaridi, inaweza kututia moyo kuona kwamba bado inawezekana kufikia mioyo ya wengine wa watu hawa. Ubaridi wao unaweza kuonyesha kuvurugika akili na kukosa kwao tumaini. Huenda wakahisi kwamba hakuna njia ya kutoka katika hali iliyopo ya ulimwengu huu, wakisababu kwamba wataishi tu maisha zao katika njia nzuri wanayoweza. Wengine wanaona kinyaa kwa sababu viongozi fulani wa kidini wanahusika katika siasa, wana hatia ya mwenendo usio wa adili, au wanashindwa kuchukua msimamo imara dhidi ya ukosefu wa adili katika ngono. Kwa hiyo wenye nyumba hawa wamezinduka na wanaishi kwa ajili ya leo tu.

16. Moyo wa mtu mwenye ubaridi unawezaje kufikiwa?

16 Tunajua kwamba wahudumu Wakristo wa mapema walikabili mwelekeo huo huo kwa mafanikio, kwa kuwa wakati huo watu fulani walisema, “Na tule, na tunywe, maana kesho tutakufa.” (1 Wakorintho 15:32) Kwa sababu hiyo, tunajua kwamba tuna kile ambacho watu hao wanahitaji kusikia. Bado, tunawezaje kufikia moyo wao? Njia moja ni kuweka kando kichapo chetu cha Biblia kwa wakati huo, ukiwaacha waone wewe ukifanya hivyo. Kisha tunaweza kuwauliza maswali yaliyofikiriwa vizuri kama haya: “Je! wewe unafikiri kuna utatuzi fulani kwa matatizo yaliyopo siku hizi? Je! inaweza kuwa kwamba watu wengi hawajapata utatuzi bado? Je! unafikiri tunapaswa kuwa na mwelekeo chanya na kuendelea kutafuta?” Kwa wengine, tunaweza kusema: “Kwa kweli unakubali kwamba ni afadhali kuishi ukiwa na tumaini kuliko kutokuwa na taraja lo lote la vitu vizuri. Wewe unatumaini kuona nini?” Tunaweza kuuliza: “Wewe mwenyewe unahisi ni nini kilicho kizuizi kikubwa cha umoja na amani ya ulimwengu?” Bado wengine wanaweza kuulizwa: “Je! wewe unafikiri dini zote ziko kama vile umeeleza?” Mara nyingi maswali ya namna hiyo yatawafanya wenye nyumba kueleza rai yao. Kisha, wanapoitikia, hakikisha kwamba unasikiliza. Ndiyo, acha wakuambia kilicho moyoni mwao. Wengi wao ‘wanatweta na kupiga kite juu ya vitu vyote vyenye kukirihika vinavyofanywa sasa.’​—Ezekieli 9:4, NW.

17. Vichapo vyetu vinaweza kutumiwaje kuwafikia watu fulani hata wakati wanaposisitiza mara ya kwanza kwamba hawapendezwi?

17 Njia nyingine ya kushughulikia ubaridi ni kukumbuka neno moja au kipingamizi ambacho mwenye nyumba anatokeza na kurudi ukiwa na gazeti au kichapo cha Mnara wa Mlinzi kinachoshughulikia habari hiyo. Kwanza, huenda hata ikawa si habari ya kidini, kama vile makala yenye kuzungumzia kifo cha ghafula cha mtoto au kumalizika kwa misitu. Eleza kwamba ulikuwa ukifikiria jambo lililopendeza mwenye nyumba na ukakumbuka makala hiyo. Kisha onyesha mambo ya msingi katika habari hiyo. Mwanamke mmoja ambaye alikuwa amekataa kichapo chetu alikubali gazeti sekunde chache baadaye. Kwa nini? Kwa kuwa Shahidi aliuliza ikiwa mwanamke huyo alijua kwamba kulikuwa na utoaji mimba milioni 55 kila mwaka. Kwa kugutuka kujua hilo, aliomba gazeti lenye habari hizo.

Ione Ikimalizika

18, 19. (a) Tunapaswa ‘kutoa uangalifu’ kwa mambo gani ya kuongezea tunapofanya huduma yetu? (b) Watu fulani wana maoni gani ya kuchukia sisi na itikadi zetu bila sababu, nasi tunaweza kuwajibuje?

18 Zaidi ya yote, tunahitaji kuwaonyesha watu subira. Zungumza kwa polepole, kwa uchangamfu. Onyesha upendo na fadhili. (Wagalatia 5:22, 23) Kabla ya kwenda kwenye mlango unaofuata, fikiria kilichotokea kwenye mlango uliotangulia ili uone mahali ambapo maendeleo yanaweza kufanywa. Uwe mwenye kufahamu, kwa kuwa watu wengi wana maoni mabaya juu ya Mashahidi wa Yehova. Huenda wakasema: ‘Ninyi mnakataa siasa na kazi za kiserikali,’ ‘Ninyi mnakataa utumishi wa kijeshi,’ au ‘Ninyi mnavunja jamaa.’ Lakini mwelekeo huu ni kama ule wa ulimwengu kuelekea waitikadi wenzetu wa karne ya kwanza. Waonyeshe wenye nyumba hilo, labda ukitumia manukuu yaliyo chini ya kichwa “Kutokuwamo” katika kitabu Reasoning.

19 Kwa habari ya Wakristo wa mapema, mwanahistoria Will Durant aliandika hivi: “Kwa Mkristo dini yake ilikuwa kitu fulani zaidi ya na kikubwa kuliko jamii ya kisiasa; utii wake ulio mkubwa ulikuwa kwa Kristo si kwa Kaisari. . . . Mtengano wa Mkristo kutoka kwa shughuli za kidunia ulionekana kwa wapagani kuwa kukimbia kazi ya kiserikali, kudhoofika kwa uzi na mapenzi ya kitaifa. Tertullian alishauri Wakristo wakatae utumishi wa kijeshi;... Wakristo walisihiwa na viongozi wao wawaepuke watu wasio Wakristo, wajiepushe na karamu zao za michezo ya kishenzi, na mahali pao pa maneno ya matusi. Ukristo [ulipokuwa ukifanya waongofu] ulishtakiwa kuwa unavunja nyumba.”​—Caesar and Christ, uku. 647.

20, 21. (a) Tunataka kuhakikisha nini watu wasipoitikia? (b) Kwa nini hatupaswi ‘kuchoka’ bali tuendelee na kazi yetu nzuri ya kuhubiri Ufalme?

20 Watu fulani fulani hawatasikiliza, hata tuseme nini. Lakini hiyo inapasa kuwa kwa sababu ya kukataa kwao ujumbe wa Ufalme si kwa sababu ya kushindwa kwetu kutoa utoaji ulio bora katika huduma yetu. (Luka 10:8-11; Matendo 17:32; Ezekieli 3:17-19) Tunapaswa kufanya vizuri tuwezavyo kwa msaada wa Mungu, naye Yehova ataimaliza kazi.​—Linganisha Wafilipi 1:6.

21 Basi, mkiwa na utumainifu kamili, endeleeni kuwa na “mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi yenu yenye bidii si ya bure kuhusiana na Bwana.” (1 Wakorintho 15:58, NW) “Toa uangalifu daima kwa wewe mwenyewe na kwa fundisho lako. Endelea katika vitu hivyo, kwa kuwa kwa kufanya hivyo utaokoa wote wawili wewe mwenyewe na wale wanaosikiliza wewe.” (1 Timotheo 4:16, NW) Zaidi ya yote, “tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.”​—Wagalatia 6:9.

Je! Unaweza Kukumbuka?

◻ Ni njia fulani zipi za kudumisha mwelekeo chanya katika eneo linalofanyiwa kazi kwa ukawaida?

◻ Tunawezaje kutafuta-tafuta wanaostahili kwa ukamili zaidi?

◻ Tunaweza kujaribu kushughulikaje na wale ambao wanalalamika kwamba tunazuru mara nyingi?

◻ Ni katika njia gani tunaweza kushughulikia tatizo la ubaridi?

◻ Ni nini kitakachofanyia maendeleo ubora wa huduma yetu?

[Sanduku katika ukurasa wa 20]

MWENEZO WA ENEO UNAPOONGEZEKA,

“Toa uangalifu daima” kwa:

◻ Njia na utoaji chanya

◻ Kutafuta-tafuta wanaostahili kwa ukamili zaidi

◻ Kushughulika na wanaolalamika kwa subira

◻ Kukabiliana na matatizo ya ubaridi na kutoelewana

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki