Wimbo 70
Uwe Kama Yeremia
1. Kutumikia Mungu
Kwatokeza furaha.
Mungu anatulinda,
Tumutumikiapo.
Biblia hutuonya
—Nayo husema kweli—
Tutazipata furaha
Hata taabu nazo.
2. Kumbuka Yeremia,
Alikuwa kijana
Alipoanza kazi;
Alifanywa shujaa.
‘Hata wapige vita
Kwa nguvu zao zote,
Hawatakushinda wewe,
Utakuwa munara.’
3. Miaka ikapita
Akiwa mwaminifu.
Na alifanikiwa,
Ajapotaabishwa.
Tumwige Yeremia;
Tutumaini Mungu.
Tuhubiri enzi kuu
Ya Mungu bila woga.