Wimbo 214
Kufuata Njia ya Mungu ya Uzima
1. Uzima mali bora, kupitia
Yesu Kristo! Tutumie vema.
Kwako Yehova tunakiri hivi:
Njia yako inatupendeza.
2. Yehova ni wewe tunaogopa.
Twapata hekima na ujuzi.
Sheria yako yatufurahisha;
Tunatembea katika hiyo.
3. Uzima una kusudi, u mwema.
Twajifunza kuishi kwa Yesu.
Sisi tusiupende ulimwengu.
Furahi zaidi kwa kutoa.
4. Tuishi katika mafunzo yako,
Sababu Ufalme ni karibu.
Tuwahubirie wapole wote,
Kristo arudishapo ibada.