Wimbo 44
Yehova Anajali Kweli Kweli
1. Yehova anatujali
Sisi tunafarijika.
‘Ajua nywele za kichwa chetu.’
Kwa nini tusumbuke?
2. Na tujapojaribiwa,
Tusikatishwe tamaa.
Kama anajali ndege sisi,
Pia atatujali.
3. Na mateso mbalimbali
Yanawapata Wakristo.
Tunasafishwa na kuzoezwa;
Atatusaidia.
4. Kweli Mungu anajali,
Na yeye atatutunza.
Tukizidi kumwabudu yeye,
Atatuthawabisha.