Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/92 uku. 8
  • Ninaweza Kusema Nini Ili Nichochee Kupendezwa Zaidi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ninaweza Kusema Nini Ili Nichochee Kupendezwa Zaidi?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Kupiga Mbiu ya ‘Maneno ya Unabii’
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Wasaidie Waelewe
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Ufunuo—Mafumbo Yafumbuliwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1992
km 3/92 uku. 8

Ninaweza Kusema Nini Ili Nichochee Kupendezwa Zaidi?

1 Sehemu ya maana ya kusudi letu la kuhubiri habari njema ni kufanya wanafunzi, si kuangusha fasihi tu. Kwa hiyo, baada ya kupendezwa kuonekana, tunahitaji kusitawisha na kulisha mbegu zilizopandwa, tukifanya sehemu yetu ya kuendeleza hali nzuri ambayo kwayo Yehova anaweza kumsaidia mtu huyo akue kiroho. (1 Kor. 3:6) Unaweza kusema nini kufuatia utoaji mbalimbali ulioonyeshwa hapo juu? Hapa pana madokezo fulani kwa ajili ya hali mbalimbali unazoweza kukabili.

2 Kusitawisha Kupendezwa Kunakopatikana: “Tulipozungumza kifupi hapo mbeleni, ulikuwa mwenye shughuli sana, lakini ulichukua wakati wako kueleza hangaiko lako kuhusu wakati ujao. Kama ukumbukavyo, tulisoma katika Biblia kwenye Ufunuo 1:3 kwamba ‘wakati uliowekwa u karibu.’ Hilo lina tokeo la moja kwa moja kwa wakati wetu ujao. Angalia yale ambayo kitabu hiki kinasema kuhusu andiko hilo. [Soma kutoka fungu 11 ukurasa 17 wa kitabu Upeo wa Ufunuo.] Kichapo hiki hupitia unabii wote wa kitabu cha Biblia cha Ufunuo na huonyesha jinsi sisi tunavyoweza kufaidika kibinafsi. Je! ungependezwa kujifunza mengi zaidi?”

3 Kutumia Kitabu Upeo wa Ufunuo Kuanzisha Funzo la Biblia: “Ni vizuri kukuona tena. Kuna jambo la ziada ningependa kushiriki nawe linalopatikana kwenye kile kitabu nilichokuachia, na ni lenye kutia moyo sana. Biblia husema juu ya ‘hati-kunjo ya uhai’ kuhusiana na wale watakaoishi milele. Je! ungependa kujua ni majina gani yaliyo katika hati-kunjo hiyo?” Fungua ukurasa 298 wa kitabu Upeo wa Ufunuo. Soma fungu 11, halafu uulize maswali ya fungu hilo. Baada ya kupitia mafungu kadhaa, sema kwamba ungependa kurudi na kuendelea na mazungumzo.

4 Kutumia Kichapo Kingine Kuanzisha Funzo la Biblia: “Ninafurahi kukupata nyumbani leo. Tulipozungumza wakati uliopita, tulisoma pamoja ahadi ya Biblia kwenye Ufunuo 1:3. [Soma tena.] Ona kwamba furaha inayozungumzwa hapo haiji kivivi hivi tu. Mambo mawili yanatakiwa: Ni lazima tusome yale ambayo Biblia husema halafu tuyashike, au kujizoeza, yale yaliyoandikwa. Broshua hii ‘Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya’ itafanya usomaji wako wa fasihi niliokuachia uwe wenye kufurahisha zaidi kwa sababu inaeleza kwa njia rahisi matakwa ya Mungu ni nini hasa. Katika ukurasa 30 kuna orodha ya maswali 12 yanayoulizwa na watu wengi. Ni lipi kati yayo ungependa ujibiwe?” Baada ya mwenye nyumba kuitikia, unaweza kufungua kwenye broshua mahali ambapo swali hilo linajibiwa na kuanza funzo la Biblia.

5 Tumia Picha Ili Uchochee Kupendezwa: Kitabu Upeo wa Ufunuo kina vielezi vingi vya wazi. Hivyo vyaweza kuonyeshwa ili kuchochea kupendezwa. Kwa mfano, tunapofanya rudio, tunaweza kufungua ukurasa 7. Onyesha picha ya Yohana akiwa kwenye kisiwa cha Patmosi. Ufunuo 1:3 huonyesha kwamba ufunuo kwa Yohana ulikuwa ujumbe wa furaha. Hilo lingewezaje kuwa hivyo hali Ufunuo huelezea wanyama wenye kuhofisha na uharibifu? Zungumzia mafungu 1 na 2 katika ukurasa 6 wa kitabu hicho. Vielezi vya upande wa ndani wa majalada vyaweza kutumiwa, pamoja na mandhari zinazoonyesha Dunia-Paradiso katika kurasa 302, 308, na 309.

6 Kuhusu ziara za kurudia, tunapaswa kujenga juu ya msingi uliowekwa wakati wa ziara ya kwanza. Kutoa uangalifu wa makini kwa upande huu wa huduma yetu kutaleta baraka nyingi kutoka kwa Yehova kwetu sisi na kwa wale watusikiao pia.—1 Tim. 4:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki