-
Sikukuu ya Kupitwa Iliyo ya Mwisho kwa Yesu YakaribiaYule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
-
-
Sura 112
Sikukuu ya Kupitwa Iliyo ya Mwisho kwa Yesu Yakaribia
JUMANNE, Nisani 11, ikaribiapo, Yesu amaliza kufundisha mitume juu ya Mlima wa Mizeituni. Lo, imekuwa siku yenye mikazo na shughuli kama nini! Sasa, labda akiwa anarudi Bethania akakae huko usiku huo, awaambia hivi mitume wake: “Nyinyi mwajua kwamba siku mbili kuanzia sasa sikukuu ya Kupitwa yatukia, na Mwana wa binadamu atatolewa atundikwe.”
Siku inayofuata, Jumatano, Nisani 12, yaonekana Yesu ajitenga ili kwa utulivu awe na mitume wake. Siku iliyotangulia, alikuwa amewakemea peupe viongozi wa kidini, naye ang’amua kwamba wanatafuta kumwua. Kwa hiyo siku ya Jumatano hajionyeshi waziwazi, kwa kuwa hataki kitu chochote kikatize kuadhimisha kwake Sikukuu ya Kupitwa pamoja na mitume wake jioni inayofuata.
Wakati uo huo, makuhani wakuu na wanaume wazee wa watu wamekusanyika katika ua wa kuhani wa juu, Kayafa. Wakiwa na udhia wa kushambuliwa na Yesu siku iliyotangulia, wanafanya mipango ya kumbamba kwa mbinu ya ujanja na kufanya auawe. Na bado wanafuliza kusema hivi: “Si kwenye ule msherehekeo, ili kwamba zahama yoyote isitokee miongoni mwa watu.” Wanawahofu watu, ambao Yesu huonea shangwe ya kibali chao.
Huku viongozi wa kidini wakitunga kwa uovu njama ya kumwua Yesu, wapokea mgeni. Wao washangazwa na jambo la kwamba ni mmoja wa mitume wa Yesu mwenyewe, Yuda Iskariote, mmoja ambaye Shetani amepanda ndani yake lile wazo bovu la kusaliti Bwana-Mkubwa wake! Wao wapendezwa kama nini Yuda aulizapo hivi: “Nyinyi mtanipa nini nikimsaliti yeye kwenu?” Wao waafikiana kwa mteremo kumlipa vipande 30 vya fedha, bei ya mtumwa kulingana na agano la Sheria ya Musa. Tangu hapo na kuendelea, Yuda atafuta fursa nzuri ya kumsaliti Yesu kwao wakati pasipokuwa na umati karibu.
Nisani 13 yaanza kwenye mshuko-jua wa Jumatano. Yesu aliwasili kutoka Yeriko siku ya Ijumaa, kwa hiyo huu ndio usiku wa sita na wa mwisho ambao atumia akiwa Bethania. Siku inayofuata, Alhamisi, matayarisho ya mwisho yatahitaji kufanywa kwa ajili ya Sikukuu ya Kupitwa, ambayo yaanza kwenye mshuko-jua. Huo ndio wakati ambapo ni lazima mwana-kondoo wa Sikukuu ya Kupitwa achinjwe halafu achomwe akiwa mzima. Wataadhimisha wapi karamu hiyo, na ni nani atafanya matayarisho?
Yesu hajaandaa maelezo hayo, labda ili kumzuia Yuda asiwapashe habari makuhani wakuu ili waweze kumkamata Yesu wakati wa mwadhimisho wa Sikukuu ya Kupitwa. Lakini sasa, labda ikiwa ni mapema alasiri ya Alhamisi, Yesu awatuma Petro na Yohana kutoka Bethania, akisema: “Endeni mkatutayarishie sikukuu ya kupitwa ili tule.”
“Wataka tuitayarishe wapi?” wao wauliza.
“Mwingiapo jijini,” Yesu aeleza, “mwanamume mmoja mwenye kubeba nyungu ya maji atawalaki. Mfuateni ndani ya nyumba ambamo yeye aingia. Nanyi ni lazima mseme kwa mmiliki-ardhi wa ile nyumba, ‘Mwalimu asema kwako hivi: “Kiko wapi chumba cha mgeni ambamo mimi naweza kula sikukuu ya kupitwa pamoja na wanafunzi wangu?”’ Na mwanamume huyo atawaonyesha chumba cha juu kikubwa chenye vifaa. Itayarisheni humo.”
Bila shaka mmiliki-ardhi huyo ni mwanafunzi wa Yesu ambaye labda atazamia ombi la Yesu kutumia nyumba yake kwa pindi hii maalumu. Vyovyote vile, Petro na Yohana wawasilipo katika Yerusalemu, wakuta kila kitu kama vile Yesu alivyotabiri. Kwa hiyo wao wawili wahakikisha kwamba mwana-kondoo yuko tayari na kwamba mipango mingine yote yafanywa ili kutimiza mahitaji ya waadhimishi wale 13 wa Sikukuu ya Kupitwa, Yesu na mitume wake 12. Mathayo 26:1-5, 14-19; Marko 14:1, 2, 10-16; Luka 22:1-13; Kutoka 21:32, NW.
▪ Yaonekana Yesu afanya nini Jumatano, na kwa nini?
▪ Ni mkutano gani ambao wafanywa nyumbani kwa kuhani wa juu, na Yuda awazuru viongozi wa kidini kwa kusudi gani?
▪ Yesu atuma nani wakaingie Yerusalemu Alhamisi, na kwa kusudi gani?
▪ Hawa waliotumwa wakuta nini ambacho kwa mara nyingine tena chafunua nguvu za kimwujiza za Yesu?
-
-
Unyenyekevu Kwenye Sikukuu ya Kupitwa ya MwishoYule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
-
-
Sura 113
Unyenyekevu Kwenye Sikukuu ya Kupitwa ya Mwisho
PETRO na Yohana, kwa kuagizwa na Yesu, tayari wamewasili katika Yerusalemu kufanya matayarisho kwa ajili ya Sikukuu ya Kupitwa. Yesu awasili baadaye alasiri, yaonekana akiwa na wale mitume wengine kumi. Jua linazama chini kwenye upeo wa macho huku Yesu na kikundi chake wakiteremka chini ya Mlima wa Mizeituni. Hii ndiyo mara ya mwisho ya Yesu kuliona jiji wakati wa mchana kutoka mlima huu mpaka baada ya ufufuo wake.
Muda si muda Yesu na kikundi chake wawasili katika jiji na kushika njia kwenda kwenye nyumba ambamo wataadhimisha Sikukuu ya Kupitwa. Wazipanda ngazi kwenda kwenye chumba kikubwa cha juu, ambamo wapata matayarisho yote yamefanywa kwa ajili ya mwadhimisho wao wa faragha wa Sikukuu ya Kupitwa. Yesu ameitazamia pindi hii, kwa vile asema: “Mimi nimetamani sana kuila sikukuu ya kupitwa hii pamoja na nyinyi kabla sijateseka.”
Kimapokeo, vikombe vinne vya divai hunywewa na washiriki wa Sikukuu ya Kupitwa. Baada ya kupokea kile ambacho yaonekana ndicho kikombe cha tatu, Yesu ashukuru na kusema: “Chukueni hiki na mkipitishe kutoka kwa mmoja hadi kwa mwingine miongoni mwenu wenyewe; kwa maana mimi nawaambia nyinyi, Kuanzia sasa na kuendelea sitakunywa tena kutoka zao la mzabibu mpaka ufalme wa Mungu uwasili.”
Wakati fulani katika mlo huo, Yesu ainuka, aweka kando mavazi yake ya nje, achukua taulo, na kujaza karai maji. Kwa kawaida, mwenye kupokea wageni ndiye angehakikisha kwamba nyayo za mgeni zimeoshwa. Lakini kwa kuwa katika pindi hii hakuna mwenye kupokea wageni, Yesu afanya utumishi huu wa kibinafsi. Yeyote wa mitume angaliweza kuwa amebamba fursa hiyo ili kufanya hivyo; na bado, yaonekana kwa sababu ushindani fulani ungali miongoni mwao, hakuna afanyaye hivyo. Sasa wao waaibika Yesu aanzapo kuosha nyayo zao.
Yesu amjiapo, Petro ateta akisema: “Kwa hakika wewe hutaosha kamwe nyayo zangu.”
“Mimi nisipokuosha wewe, wewe huna sehemu pamoja na mimi,” Yesu asema.
“Bwana,” Petro aitikia, “si nyayo zangu tu, bali pia mikono yangu na kichwa changu.”
“Yeye ambaye ameoga,” Yesu ajibu, “hahitaji kuoshwa zaidi ya nyayo zake, bali ni safi kabisa. Na nyinyi watu ni safi, lakini si nyote.” Asema hivyo kwa sababu ajua kwamba Yuda Iskariote anapanga kumsaliti.
Yesu akiisha kuosha nyayo za wote 12, kutia na nyayo za msaliti wake, Yuda, avaa mavazi yake ya nje na kuegemea mezani tena. Halafu auliza: “Je! nyinyi mwajua lile ambalo mimi nimewafanyia nyinyi? Nyinyi huniita, ‘Mwalimu,’ na, ‘Bwana,’ na mwasema ifaavyo, kwa maana ndivyo nilivyo. Kwa hiyo, ikiwa mimi, ijapokuwa ni Bwana na Mwalimu, nimeosha nyayo zenu, nyinyi pia mwapaswa kuosha nyayo za mmoja na mwenzake. Kwa maana mimi niliwawekea nyinyi kigezo, kwamba, kama vile mimi nilivyowafanyia nyinyi, nyinyi mwapaswa kufanya hivyo pia. Kwa kweli kabisa mimi nasema kwenu nyinyi, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana-mkubwa wake, wala mwenye kutumwa si mkubwa kuliko mwenye kumtuma. Ikiwa mwajua mambo haya, wenye furaha ni nyinyi ikiwa mwayafanya.”
Lo, somo zuri kama nini la utumishi wa unyenyekevu! Mitume hawapaswi kuwa wakitafuta mahali pa kwanza, wakifikiri kwamba wao ni wa maana sana hivi kwamba wengine wapaswa kuwatumikia wao sikuzote. Wao wahitaji kufuata kigezo kilichowekwa na Yesu. Hicho si kigezo cha uoshaji nyayo kidesturi tu. Sivyo, bali ni cha nia ya kutumikia bila upendeleo, hata kama kazi ile ni ya umaana mdogo au isiyopendeza kwa kadiri gani. Mathayo 26:20, 21; Marko 14:17, 18; Luka 22:14-18; 7:44; Yohana 13:1-17, NW.
▪ Ni jambo gani lisilo na kifani juu ya Yesu kuona Yerusalemu aingiapo ili kuadhimisha Sikukuu ya Kupitwa?
▪ Wakati wa Sikukuu ya Kupitwa, yaonekana ni kikombe gani ambacho Yesu apitisha kwa wale mitume 12 baada ya kusema baraka?
▪ Ni utumishi gani wa kibinafsi ulioandaliwa wageni kidesturi Yesu alipokuwa duniani, na kwa nini haukuandaliwa wakati wa Sikukuu ya Kupitwa iliyoadhimishwa na Yesu na mitume?
▪ Kusudi la Yesu lilikuwa nini katika kufanya utumishi huo wenye umaana mdogo wa kuosha nyayo za mitume wake?
-
-
Kijio cha UkumbushoYule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
-
-
Sura 114
Kijio cha Ukumbusho
BAADA ya Yesu kuosha miguu ya mitume wake, yeye anukuu andiko lililo kwenye Zaburi 41:9, NW, akisema: “Yeye aliyekuwa akila mkate wangu ameinua kisigino chake dhidi yangu.” Halafu, akifadhaika katika roho, aeleza hivi: “Mmoja wenu nyinyi atanisaliti.”
Mitume waanza kuwa na kihoro na kumwambia Yesu hivi mmoja baada ya mwingine: “Si mimi, au sivyo?” Hata Yuda Iskariote ajiunga katika kuuliza. Yohana, ambaye amejinyoosha karibu na Yesu mezani, aegemea nyuma kwenye kifua cha Yesu na kuuliza: “Bwana, ni nani?”
“Ni mmoja wa wale kumi na wawili, ambaye anachovya pamoja nami ndani ya bakuli la ujumla,” Yesu ajibu. “Kweli, Mwana wa binadamu anaenda zake, kama vile imeandikwa kuhusu yeye, lakini ole wake mtu huyo ambaye kupitia yeye Mwana wa binadamu asalitiwa! Ingalikuwa vizuri zaidi kwa mtu huyo kama asingalizaliwa.” Baada ya hapo, Shetani amwingia Yuda tena, akitumia kwa faida yake ile nafasi wazi iliyo katika moyo wake, ambao umekuwa mwovu. Baadaye usiku huo, kwa kufaa Yesu amwita Yuda “mwana wa uharibifu.”
Sasa Yesu amwambia Yuda: “Unalolifanya lifanyishe kwa haraka zaidi.” Hakuna yeyote wa wale mitume wengine aelewa Yesu amaanisha nini. Baadhi yao wawazia kwamba kwa kuwa Yuda ndiye mwenye sanduku la pesa, Yesu anamwambia: “Nunua vitu ambavyo twahitaji kwa ajili ya msherehekeo,” au kwamba apaswa kwenda na kuwapa maskini kitu fulani.
Baada ya Yuda kuondoka, Yesu aanzisha mwadhimisho mpya kabisa, au ukumbuko, pamoja na mitume wake waaminifu. Achukua mkate, asema sala ya shukrani, aumega, na kuwapa, akisema: “Chukueni, mle.” Aeleza hivi: “Huu wamaanisha mwili wangu ambao utatolewa kwa ajili yenu. Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.”
Kila mmoja aishapo kula kutokana na mkate huo, Yesu achukua kikombe cha divai, ambacho kwa wazi ndicho kikombe cha nne chenye kutumiwa katika sherehe ya Sikukuu ya Kupitwa. Pia asema sala ya shukrani juu yacho, awapitishia, awaomba wanywe kutokana nacho, na kutaarifu hivi: “Kikombe hiki chamaanisha agano jipya kwa nguvu ya damu yangu, ambayo itamwagwa kwa ajili yenu.”
Kwa hiyo, kwa uhakika, huu ni ukumbusho wa kifo cha Yesu. Kila mwaka siku ya Nisani 14 wapasa kurudiwa, kama vile Yesu alivyosema, kwa ukumbusho wake. Utakumbusha waadhimishaji mambo ambayo Yesu na Baba yake wa kimbingu wamefanya kuandalia ainabinadamu mponyoko wa kutoka kwenye laana ya kifo. Kwa Wayahudi ambao huwa wafuasi wa Kristo, mwadhimisho huo utachukua mahali pa Sikukuu ya Kupitwa.
Agano jipya, ambalo hutendeshwa kazi na damu ya Yesu iliyomwagwa, huchukua mahali pa agano la kale la Sheria (Torati). Hilo hupatanishwa na Yesu Kristo kati ya vikundi viwili—kwa upande mmoja, Yehova Mungu, na kwa upande mwingine, Wakristo 144,000 waliozaliwa kwa roho. Zaidi ya kuandaa msamaha wa dhambi, agano hilo huruhusu kufanyizwa kwa taifa la kimbingu la wafalme-makuhani. Mathayo 26:21-29; Marko 14:18-25; Luka 22:19-23; Yohana 13:18-30; 17:12; 1 Wakorintho 5:7, NW.
▪ Yesu anukuu unabii gani wa Biblia kuhusu mwandamani fulani, naye aufanyia utumizi gani?
▪ Kwa nini mitume waingiwa na kihoro kingi, na kila mmoja wao auliza nini?
▪ Yesu amwambia Yuda afanye nini, lakini mitume wale wengine wafasirije maagizo hayo?
▪ Yesu aanzisha mwadhimisho gani baada ya Yuda kuondoka, nao una kusudi gani?
▪ Ni vikundi gani vilivyo katika agano jipya, na agano hilo latimiza nini?
-
-
Bishano LafokaYule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
-
-
Sura 115
Bishano Lafoka
MAPEMA kidogo jioni, Yesu alifundisha somo zuri la utumishi wa unyenyekevu kwa kuosha miguu ya mitume wake. Baadaye, alianzisha Ukumbusho wa kifo chake kinachokaribia. Sasa, hasa kwa sababu ya kile ambacho kimetendeka sasa hivi, tukio la kushangaza latukia. Mitume wake wahusika katika bishano kali juu ya ni yupi kati yao aonekana kuwa mkubwa kupita wote! Yaonekana kwamba hii ni sehemu ya ugomvi wenye kuendelea.
Kumbuka kwamba baada ya Yesu kugeuzwa sura mlimani, mitume walibishana juu ya nani miongoni mwao alikuwa mkubwa kupita wote. Zaidi ya hilo, Yakobo na Yohana waliomba vyeo vya umashuhuri katika Ufalme, hiyo ikitokeza ushindani zaidi miongoni mwa mitume. Sasa, katika usiku wake wa mwisho wa kuwa pamoja nao, ni lazima Yesu awe ahuzunika kama nini kuwaona wakizozana tena! Yeye afanya nini?
Badala ya kuwagombeza mitume kwa mwenendo wao, kwa mara nyingine tena Yesu asababu pamoja nao kwa subira: “Wafalme wa mataifa hupiga ubwana juu yao, na wale walio na mamlaka juu yao huitwa Wafadhili. Ingawa hivyo, nyinyi hamtakuwa hivyo. . . . Kwa maana ni yupi aliye mkubwa zaidi, yule anayeegemea kwenye meza au yule anayehudumia? Je! si yule anayeegemea kwenye meza?” Halafu, akiwakumbusha juu ya kielelezo chake, asema hivi: “Lakini mimi niko kati yenu kama yule anayehudumia.”
Wajapokuwa na hali zao za kutokamilika, mitume wameshikamana na Yesu wakati wa majaribu yake. Kwa hiyo yeye asema: “Mimi nafanya agano pamoja nanyi, kama vile Baba yangu amefanya agano pamoja na mimi, kwa ajili ya ufalme.” Agano hili la kibinafsi kati ya Yesu na wafuasi wake waaminifu-washikamanifu huwaunga wao kwake ili washiriki umiliki wake wa kifalme. Ni hesabu ndogo tu ya 144,000 ambao mwishowe hutiwa ndani ya agano hili kwa ajili ya Ufalme.
Ingawa mitume wametokezewa tazamio hili zuri sana la kushiriki pamoja na Kristo katika utawala wa Ufalme, kwa sasa wao ni dhaifu kiroho. “Nyinyi nyote mtajikwaa kuhusiana na mimi usiku huu,” Yesu asema. Hata hivyo, akimwambia Petro kwamba Yeye amesali kwa ajili yake, Yesu ahimiza hivi: “Mara ukiisha kurudi, waimarishe ndugu zako.”
“Watoto wadogo,” Yesu aeleza, “mimi niko pamoja nanyi kitambo kidogo zaidi. Nyinyi mtanitafuta mimi; na kama vile nilivyosema kwa Wayahudi, ‘Niendako nyinyi hamwezi kuja,’ nasema kwenu nyinyi pia kwa sasa. Mimi nawapa nyinyi amri mpya, kwamba mpendane; kama vile mimi nimewapenda nyinyi, ili kwamba nyinyi pia mpendane. Kwa hili wote watajua kwamba nyinyi ni wanafunzi wangu, mkiwa na upendo miongoni mwa nyinyi wenyewe.”
“Bwana, wewe unaenda wapi?” Petro auliza.
“Niendako huwezi wewe kunifuata sasa,” Yesu ajibu, “lakini utafuata baadaye.”
“Bwana, kwa nini mimi siwezi kukufuata wewe kwa sasa?” Petro ataka kujua. “Mimi nitaitoa nafsi yangu kwa ajili yako.”
“Je! wewe utaitoa nafsi yako kwa ajili yangu?” Yesu auliza. “Kwa kweli mimi nasema kwako wewe, Wewe leo, naam, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, hata wewe utanikana mimi mara tatu.”
“Hata ikinipasa mimi kufa pamoja na wewe,” Petro ateta, “kwa vyovyote mimi sitakukana.” Na ingawa mitume wale wengine wajiunga katika kusema hilo hilo, Petro ajisifu hivi: “Ingawa wengine wote wajikwae kuhusiana na wewe, mimi sitajikwaa kamwe!”
Akirejezea wakati ambao aliwatuma mitume nje kwenye safari ya kuhubiri Galilaya bila kibeti na kifuko cha chakula, Yesu auliza hivi: “Nyinyi hamkukosa kitu chochote, je! mlikosa?”
“La!” wao wajibu.
“Lakini sasa acheni yule mwenye kibeti akichukue, vivyo hivyo pia kifuko cha chakula,” yeye asema, “na acheni yule asiye na upanga auze vazi lake la nje anunue mmoja. Kwa maana mimi nasema kwenu nyinyi kwamba hili ambalo limeandikwa ni lazima litimizwe katika mimi, yaani, ‘Na yeye alihesabiwa pamoja na wasiofuata sheria.’ Kwa maana lile ambalo lanihusu mimi linatimizwa.”
Yesu anaelekeza kwenye wakati ambapo atatundikwa pamoja na watenda maovu, au wasiofuata sheria. Pia anaonyesha kwamba baada ya hapo wafuasi wake watakabili mnyanyaso mkali. “Bwana, tazama! panga mbili hizi,” wao wasema.
“Imetosha,” yeye ajibu. Kama tutakavyoona, kuwa kwao na panga hizo kutaruhusu Yesu karibuni afundishe somo jingine muhimu. Mathayo 26:31-35; Marko 14:27-31; Luka 22:24-38; Yohana 13:31-38; Ufunuo 14:1-3, NW.
▪ Kwa nini bishano la mitume linashangaza sana?
▪ Yesu ashughulikiaje bishano hilo?
▪ Ni nini kitimizwacho na agano ambalo Yesu afanya na wanafunzi wake?
▪ Yesu atoa amri gani mpya, nayo ni ya maana kadiri gani?
▪ Petro aonyesha uhakika gani wa kupita kiasi, na Yesu asema nini?
▪ Kwa nini maagizo ya Yesu juu ya kuchukua kibeti na kifuko cha chakula ni tofauti na yale aliyotoa mapema kidogo?
-
-
Kuwatayarisha Mitume kwa Ajili ya Kuondoka KwakeYule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
-
-
Sura 116
Kuwatayarisha Mitume kwa Ajili ya Kuondoka Kwake
MLO wa ukumbusho umemalizika, lakini Yesu na mitume wake wangali katika chumba cha juu ghorofani. Ingawa hivi karibuni Yesu atakuwa hayupo, bado yeye ana mambo mengi ya kusema. “Msifadhaike mioyoni mwenu,” yeye awafariji. “Mnamwamini Mungu.” Lakini yeye aongeza: “Niaminini na mimi.”
“Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi,” Yesu aendelea kusema. “Naenda kuwaandalia mahali . . . ili nilipo mimi, nanyi mwepo. Nami niendako mwaijua njia.” Mitume hawafahamu kwamba Yesu aongea juu ya kwenda zake mbinguni, kwa hiyo Tomaso auliza: “Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia?”
“Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima,” Yesu ajibu. Ndiyo, kukubali na kuiga mwendo wake wa maisha ndiyo njia ya pekee tu ambayo kwayo yeyote aweza kuingia katika nyumba ya kimbingu ya Baba kwa sababu, kama vile Yesu asemavyo: “Mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.”
“Bwana, utuonyeshe Baba,” Filipo aomba, ‘na yatutosha.’ Yaonekana Filipo ataka Yesu aandae udhihirisho wenye kuonekana kuhusu Mungu, kama ule uliotolewa nyakati za kale katika njozi kwa Musa, Eliya, na Isaya. Lakini, kwa kweli, mitume wana kitu fulani kilicho bora sana kuliko njozi za namna hiyo, kama vile Yesu aoneleavyo: “Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba [pia, NW].”
Yesu aonyesha utu wa Baba yake kwa ukamilifu sana hivi kwamba kuishi pamoja naye na kumchunguza ni kama kumwona Baba kikweli. Hata hivyo, Baba ni mkuu kuliko Mwana, kama vile Yesu akirivyo: “Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu.” Kwa kufaa Yesu ampa Baba yake wa kimbingu sifa yote kwa mafundisho yake.
Ni lazima iwe yawatia mitume moyo kama nini kumsikia Yesu sasa akiwaambia: “Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya”! Yesu hamaanishi kwamba wafuasi wake watatumia nguvu za kimuujiza zilizo kubwa kuliko zile ambazo yeye alitumia. Sivyo, bali amaanisha kwamba wataendesha huduma kwa muda mrefu zaidi, katika eneo kubwa zaidi, na kwa watu wengi zaidi.
Yesu hatawaacha wanafunzi wake baada ya kuondoka kwake. “Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu,” yeye aahidi, “nitalifanya.” Zaidi ya hilo, asema hivi: “Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli [roho ya kweli, NW].” Baadaye, akiisha kupaa mbinguni, Yesu amimina juu ya wanafunzi wake ile roho takatifu, msaidiaji huyu mwingine.
Kuondoka kwa Yesu ku karibu, kama asemavyo: “Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena.” Yesu atakuwa kiumbe wa roho asiyeweza kuonwa na binadamu yeyote. Lakini Yesu awaahidi tena mitume wake waaminifu hivi: “Ninyi mnaniona [mtaniona, NW] . . . kwa sababu mimi ni hai [na] ninyi nanyi mtakuwa hai.” Ndiyo, si kwamba tu Yesu atawatokea kwa umbo la kibinadamu baada ya ufufuo wake bali pia atawafufua wakati uwadiapo ili wawe pamoja naye kwenye uhai mbinguni wakiwa viumbe wa roho.
Sasa Yesu ataarifu ile kanuni sahili: “Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.”
Hapo mtume Yuda, yule aitwaye pia Thadayo, akatiza mazungumzo hivi: “Bwana, imekuwaje ya kwamba wataka kujidhihirisha kwetu, wala si kwa ulimwengu?”
“Mtu [yeyote, NW] akinipenda,” Yesu ajibu, “atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda . . . Mtu asiyenipenda, yeye hayashiki maneno yangu.” Tofauti na wafuasi wake watiifu, ulimwengu hupuuza mafundisho ya Kristo. Kwa hiyo yeye hajifunui kwao.
Wakati wa huduma yake ya kidunia, Yesu amefundisha mitume wake mambo mengi. Watayakumbukaje yote, hasa kwa kuwa hata kufikia sasa washindwa kushika mengi sana? Kwa furaha Yesu aahidi hivi: “Huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu [roho takatifu, NW], ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.”
Akiwafariji tena, Yesu asema hivi: “Amani nawaachieni; amani yangu nawapa . . . Msifadhaike mioyoni mwenu.” Kweli Yesu anaondoka, lakini aeleza hivi: “Kama mngalinipenda, mngalifurahi kwa sababu naenda kwa Baba; kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi.”
Wakati wa Yesu unaobaki wa kuwa pamoja nao ni mfupi. “Mimi sitasema nanyi maneno mengi tena,” yeye asema, “kwa maana yuaja mkuu wa ulimwengu huu, wala hana kitu kwangu.” Shetani Ibilisi, yeye aliyeweza kumwingia Yuda na kumwongoza, ndiye mtawala wa ulimwengu. Lakini katika Yesu hamna udhaifu wowote wenye dhambi ambao Shetani aweza kutumia ili amgeuze asitumikie Mungu.
Kuonea Shangwe Uhusiano wa Karibu
Kufuatia mlo wa ukumbusho, Yesu amekuwa akiwatia moyo mitume wake kwa hotuba isiyo rasmi ya kufunuliana yaliyomo moyoni. Yaweza kuwa ni baada ya katikati ya usiku. Kwa hiyo Yesu ahimiza hivi: “Ondokeni, twendeni zetu.” Hata hivyo, kabla hawajaondoka, Yesu, kwa kusukumwa na upendo wake kwa ajili yao, aendelea kunena, akiandaa kielezi chenye kuchochea.
“Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima,” aanza. Mkulima Mkuu, Yehova Mungu, alipanda mzabibu huo wa mfano alipompaka mafuta Yesu kwa roho takatifu wakati wa ubatizo wake katika vuli ya 29 W.K. Lakini Yesu aendelea kuonyesha kwamba mzabibu huo wafananisha zaidi ya yeye tu, akionelea hivi: “Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa. . . . Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu. Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi.”
Wakati wa Pentekoste, siku 51 baadaye, mitume na wengine wakawa matawi ya mzabibu huo wakati roho takatifu inapomiminwa juu yao. Hatimaye, watu 144,000 wakawa matawi ya mzabibu wa kitamathali. Pamoja na shina la mzabibu, Yesu Kristo, wao wajumlika kuwa mzabibu wa ufananisho ambao huzaa matunda ya Ufalme wa Mungu.
Yesu afafanua ufunguo wa kuzaa matunda: “Akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.” Hata hivyo, ikiwa mtu ashindwa kuzaa matunda, Yesu asema, “hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni yakateketea.” Kwa upande mwingine, Yesu aahidi hivi: “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.”
Yesu azidi kusema kwa mitume wake: “Hivyo hutukuzwa Baba yangu, kwa vile mzaavyo sana; nanyi mtakuwa wanafunzi wangu.” Matunda anayotamani Mungu kutoka kwa matawi hayo ni udhihirisho wao wa sifa kama za Kristo, hasa upendo. Zaidi ya hayo, kwa kuwa Kristo alikuwa mpiga mbiu ya Ufalme wa Mungu, tunda lenye kutamanika latia ndani pia utendaji wao wa kufanya wanafunzi sawa na alivyofanya yeye.
“Kaeni katika pendo langu,” sasa Yesu awahimiza. Hata hivyo, mitume wake wawezaje kufanya hivyo? “Mkizishika amri zangu,” yeye asema, “mtakaa katika pendo langu.” Akiendelea, Yesu aeleza hivi: “Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi. Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”
Baada ya saa chache, Yesu atadhihirisha upendo huu unaozidi kwa kuutoa uhai wake kwa ajili ya mitume wake, na pia kwa ajili ya wengine wote watakaozoea imani katika yeye. Kielelezo chake chapasa kusukuma wafuasi wake wawe na upendo uo huo wa kujidhabihu kwa ajili ya mmoja na mwenzake. Upendo huo utawatambulisha, kama alivyosema Yesu mapema kidogo: “Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.”
Akitambulisha rafiki zake, Yesu asema: “Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo. Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.”
Huo ni uhusiano ulio na thamani kama nini kuwa nao—kuwa rafiki za karibu za Yesu! Lakini ili kuendelea kuonea shangwe uhusiano huo, wafuasi wake wapaswa kuendelea ‘kuzaa matunda.’ Wakifanya hivyo, Yesu asema, “lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu a[ta]wapeni.” Hakika, hiyo ni thawabu tukufu kwa ajili ya kuzaa matunda ya Ufalme! Baada ya kuwahimiza tena mitume wake ‘wapendane,’ Yesu aeleza kwamba ulimwengu utawachukia. Hata hivyo, yeye awafariji hivi: “Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.” Kisha Yesu afunua ni kwa nini ulimwengu huchukia wafuasi wake, akisema hivi: “Kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.”
Akiendelea kufafanua sababu ya chuki ya ulimwengu, Yesu aendelea kusema hivi: “Haya yote watawatenda kwa ajili ya jina langu, kwa kuwa hawamjui yeye [Yehova Mungu] aliyenipeleka.” Kazi za kimuujiza za Yesu, kwa kweli, zawahukumu wale wanaomchukia yeye, kama asemavyo: “Kama nisingalitenda kwao kazi asizozitenda mtu mwingine, wasingalikuwa na dhambi; lakini sasa wametuona mimi na Baba yangu na kutuchukia.” Kwa hiyo, kama asemavyo Yesu, andiko limetimizwa: “Walinichukia bure.”
Kama alivyofanya mapema kidogo, kwa mara nyingine tena Yesu awafariji kwa kuahidi kupeleka msaidizi, roho takatifu, ambayo ni kani ya utendaji ya Mungu yenye uwezo. “Yeye atanishuhudia [hiyo itatoa ushahidi juu yangu mimi, NW]. Nanyi pia mnashuhudia.”
Onyo Zaidi la Upole Wakati wa Kuachana
Yesu na mitume wake wamejiandaa kuondoka kwenye chumba cha juu. “Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa [mkakwazwa, NW],” yeye aendelea. Halafu atoa onyo hili zito: “Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada.”
Kwa wazi mitume wafadhaishwa kwa kina kirefu na onyo hilo. Ingawa mapema kidogo Yesu alikuwa amesema kwamba ulimwengu ungewachukia, hakuwa amefunua moja kwa moja jinsi hiyo kwamba wangeuawa. “Sikuwaambia hayo tangu mwanzo,” Yesu aeleza, “kwa sababu nalikuwapo pamoja nanyi.” Hata hivyo, ni vizuri kama nini kutangulia kuwatahadharisha kwa habari hiyo kabla hajaondoka!
“Lakini sasa,” Yesu aendelea kusema, “naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka, wala hakuna mmoja wenu aniulizaye, Unakwendapi?” Mapema kidogo jioni hiyo, walikuwa wameuliza anaenda wapi, lakini sasa wameshtushwa sana na lile ambalo amewaambia hivi kwamba washindwa kuuliza zaidi juu ya jambo hilo. Kama asemavyo Yesu: “Kwa sababu nimewaambia hayo huzuni imejaa mioyoni mwenu.” Mitume wana kihoro si kwa sababu tu wamejifunza kwamba watapatwa na mnyanyaso mbaya sana na kuuawa bali pia kwa sababu Bwana wao anawaacha.
Hivyo basi Yesu aeleza hivi: “Yawafaa ninyi mimi niondoke; kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu.” Akiwa binadamu, Yesu aweza kuwa mahali pamoja tu kwa wakati mmoja, lakini awapo mbinguni, aweza kupeleka msaidizi, roho takatifu ya Mungu, kwa wafuasi wake popote walipo duniani. Hivyo basi kuondoka kwa Yesu kutakuwa na manufaa.
Roho takatifu hiyo, Yesu asema, ‘itahakikishia ulimwengu habari ya dhambi, na haki, na hukumu.’ Dhambi ya ulimwengu, kushindwa kwao kujizoeza imani katika Mwana wa Mungu, itafichuliwa. Kwa kuongezea, ithibati yenye kusadikisha juu ya uadilifu wa Yesu itaonyeshwa kwa kupaa kwake kwenda kwa Baba. Na kushindwa kwa Shetani na ulimwengu wake mwovu kuvunja ukamilifu-maadili wa Yesu ni uthibitisho wenye kusadikisha kwamba mtawala wa ulimwengu amehukumiwa vikali.
“Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia,” Yesu aendelea kusema, “lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa.” Kwa hiyo Yesu aahidi kwamba wakati amiminapo roho takatifu, ambayo ni kani ya utendaji ya Mungu, itawaongoza katika uelewevu wa mambo hayo kwa kulingana na uwezo wao wa kushika mambo.
Mitume washindwa hasa kuelewa kwamba Yesu atakufa halafu awatokee baada ya yeye kufufuliwa. Kwa hiyo wao waulizana hivi: “Neno gani hilo asemalo, Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni, na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona? na hilo, Kwa sababu naenda zangu kwa Baba?”
Yesu ang’amua kwamba wao wataka kumwuliza swali, kwa hiyo aeleza hivi: “Amin, amin, nawaambia, Ninyi mtalia na kuomboleza, bali ulimwengu utafurahi; ninyi mtahuzunishwa, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.” Baadaye siku hiyo, wakati wa alasiri, Yesu anapouawa, viongozi wa kidini walimwengu washangilia, lakini wanafunzi wana kihoro. Hata hivyo, kihoro chao chabadilika kuwa shangwe, Yesu afufuliwapo! Na shangwe yao yaendelea awatiapo nguvu wakati wa Pentekoste ili wawe mashahidi wake kwa kumimina roho takatifu ya Mungu juu yao!
Akilinganisha hali ya mitume na ile ya mwanamke wakati wa maumivu ya kuzaa, Yesu asema: “Mwanamke azaapo, yuna huzuni kwa kuwa saa yake imefika.” Lakini Yesu aonelea kwamba yeye hakumbuki tena dhiki yake mtoto wake akiisha kuzaliwa, naye awatia moyo mitume wake, akisema: “Basi ninyi hivi sasa mna huzuni; lakini mimi nitawaona tena [nifufuliwapo]; na mioyo yenu itafurahi, na furaha yenu hakuna awaondoleaye.”
Kufikia wakati huu, mitume hawajapata kamwe kuomba mambo kwa jina la Yesu. Lakini sasa yeye asema: “Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu. . . . Kwa maana Baba mwenyewe awapenda kwa kuwa ninyi mmenipenda mimi, na kusadiki ya kwamba mimi nalitoka kwa Baba [nilitoka nikiwa mwakilishi wa Baba, NW]. Nalitoka kwa Baba, nami nimekuja hapa ulimwenguni; tena nauacha ulimwengu; na kwenda kwa Baba.”
Maneno ya Yesu ni kitia-moyo kikubwa kwa mitume. “Kwa hiyo twasadiki ya kwamba ulitoka kwa Mungu,” wao wasema. “Je! mnasadiki sasa?” Yesu auliza. “Tazama, saa yaja, naam, imekwisha kuja, ambapo mtatawanyika kila mtu kwao kwao, na kuniacha mimi peke yangu.” Hata lionekane kuwa jambo lisilosadikika kama nini, latukia kabla ya usiku huo kwisha!
“Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu [kwa njia yangu mimi, NW].” Yesu amalizia: “Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.” Yesu aliushinda ulimwengu kwa kutimiza mapenzi ya Mungu kwa uaminifu japo kila jambo ambalo Shetani na ulimwengu wake walijaribu kufanya ili wavunje ukamilifu wa Yesu.
Sala ya Kumalizia Katika Chumba cha Juu
Kwa kusukumwa na upendo wa kina kirefu kwa mitume wake, Yesu amekuwa akiwatayarisha kwa ajili ya kuondoka kwake kuliko karibu. Sasa, baada ya kuwaonya kwa upole na kuwafariji kirefu, ainua macho yake mbinguni na kumwomba Baba yake dua kwa bidii hivi: “Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe; kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele.”
Lo, ni kichwa chenye kuchochea kama nini ambacho Yesu atanguliza—uzima wa milele! Akiisha kupewa “mamlaka juu ya wote wenye mwili,” Yesu aweza kuipa aina ya kibinadamu yote yenye kufa manufaa za dhabihu yake ya ukombozi. Hata hivyo yeye huwapa “uzima wa milele” wale tu ambao Baba awakubali. Akikuza kichwa hiki cha uzima wa milele, Yesu aendelea na sala yake hivi:
“Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.” Ndiyo, wokovu wategemea kutwaa kwetu maarifa juu ya wote wawili, Mungu na Mwana wake. Lakini mengi zaidi yahitajiwa kuliko maarifa ya kichwani tu.
Ni lazima mtu apate kuwajua kindani, akisitawisha urafiki wenye uelewano pamoja nao. Ni lazima mtu ahisi kama vile wao huhisi juu ya mambo na ayaone kupitia macho yao. Na juu ya yote, ni lazima mtu ajitahidi kuiga sifa zao zisizo na kifani katika kushughulika na wengine.
Halafu, Yesu asali hivi: “Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.” Akiwa ametimiza mgawo wake hivyo kufikia hapo na kuwa mwenye uhakika juu ya mafanikio yake ya wakati ujao, aomba dua hivi: “Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.” Naam, sasa aomba kwamba kwa njia ya ufufuo aurudishwe kwenye utukufu wa kimbingu aliokuwa nao hapo kwanza.
Akitoa muhtasari wa kazi yake kuu duniani, Yesu asema hivi: “Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwewngu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika.” Yesu alitumia jina la Mungu, Yehova, katika huduma yake na akaonyesha tamko lalo sahihi, lakini alifanya mengi zaidi ya kudhihirisha jina la Mungu kwa mitume. Pia alipanua maarifa na uthamini wao juu ya Yehova, juu ya utu wake, na juu ya makusudi yake.
Akimpa Yehova sifa ya kuwa Mkuu kuliko yeye, Mmoja ambaye yeye hutumika chini yake, Yesu akiri kwa unyenyekevu hivi: “Maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”
Akipambanua kati ya wafuasi wake na na ile sehemu nyingine ya ainabinadamu, Yesu asali tena hivi: “Siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa . . . Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda . . . , nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu,” yaani, Yuda Iskariote. Wakati uo huo, Yuda yuko kwenye safari yake ya kudharaulika ili amsaliti Yesu. Hivyo, bila kujua Yuda anatimiza Maandiko.
“Ulimwengu umewachukia,” Yesu aendelea kusali. “Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu. Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.” Wafuasi wa Yesu wamo katika ulimwengu, jamii hii ya kibinadamu iliyopangwa kitengenezo yenye kutawalwa na Shetani, lakini wao wametengwa nao na ni lazima wabaki sikuzote wakiwa wametengwa nao na uovu wao.
“Uwatakase kwa ile kweli,” Yesu aendelea, “neno lako ndiyo kweli.” Hapa Yesu ayaita “kweli” Maandiko ya Kiebrania, ambayo kwa kuendelea yeye aliyanukuu. Lakini yale aliyowafundisha wanafunzi wake na yale waliyoyaandika baadaye chini ya uvuvio yakiwa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ni “kweli” vilevile. Ukweli huu waweza kutakasa mtu, ubadili maisha yake kabisa, na kumfanya mtu kuwa aliyetengwa na ulimwengu.
Sasa Yesu ‘haombei hao tu; lakini na wale watakaomwamini kwa sababu ya neno lao.’ Kwa hiyo Yesu asali kwa ajili ya wale watakaokuwa wafuasi wake wapakwa-mafuta na wanafunzi wengine wa wakati ujao ambao bado watakusanywa ndani ya “kundi moja.” Yeye aomba nini kwa ajili ya wote hao?
“Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu [ulivyo katika mwungano pamoja nami, NW], nami ndani yako . . . ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja [mmoja, NW].” Yesu na Baba yake si mtu mmoja kihalisi, bali wana mwafaka juu ya mambo yote. Yesu asali kwamba wafuasi wake wapate shangwe ya umoja uo huo ili “ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.”
Kwa ajili ya wale ambao wangekuwa wafuasi wake wapakwa-mafuta, sasa Yesu afanya ombi kwa Baba yake. Ombi la nini? Kwamba “wawe pamoja nami po pote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi [wa] ulimwengu,” yaani, kabla Adamu na Hawa hawajatunga mimba ya uzao wao. Muda mrefu kabla ya hapo, Mungu alimpenda Mwana wake mzaliwa-pekee, aliyepata kuwa Yesu Kristo.
Akimalizia sala yake, Yesu akazia tena hivi: “Naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; [ili] pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao [katika mwungano pamoja nao, NW].” Kwa mitume, kujifunza jina la Mungu kumetia ndani kupata kuujua kibinafsi upendo wa Mungu. Yohana 14:1–17:26; 13:27, 35, 36; 10:16; Luka 22:3, 4; Kutoka 24:10; 1 Wafalme 19:9-13; Isaya 6:1-5; Wagalatia 6:16; Zaburi 35:19; 69:4; Mithali 8:22, 30.
▪ Yesu aenda wapi, na Tomaso apokea jibu gani kuhusu njia ya kwenda huko?
▪ Kwa ombi lake, yaonekana Filipo ataka Yesu aandae nini?
▪ Kwa nini mtu ambaye amemwona Yesu amemwona Baba pia?
▪ Ni jinsi gani wafuasi wa Yesu hufanya kazi kubwa kuliko zile alizofanya yeye?
▪ Ni katika maana gani Shetani hana kitu kwa Yesu?
▪ Yehova alipanda lini mzabibu wa ufananisho, na wengine wanakuwa sehemu ya mzabibu huo lini na jinsi gani?
▪ Hatimaye, mzabibu wa ufananisho wawa na matawi mangapi?
▪ Mungu atamani matunda gani kutoka kwa matawi hayo?
▪ Twawezaje kuwa rafiki za Yesu?
▪ Ni kwa nini ulimwengu wachukia wafuasi wa Yesu?
▪ Ni onyo gani la Yesu ambalo lafadhaisha mitume wake?
▪ Kwa nini mitume washindwa kumwuliza Yesu swali juu ya anakoenda?
▪ Ni jambo gani hasa ambalo mitume washindwa kuelewa?
▪ Yesu atoaje kielezi cha kwamba hali ya mitume itabadilika iache kuwa ya kihoro iwe ya shangwe?
▪ Yesu asema mitume watafanya nini hivi karibuni?
▪ Yesu ashindaje ulimwengu?
▪ Ni katika maana gani Yesu amepewa “mamlaka juu ya wote wenye mwili”?
▪ Yamaanisha nini kutwaa maarifa juu ya Mungu na Mwana wake?
▪ Ni katika njia zipi Yesu afanya jina la Mungu lidhihirike?
▪ “Kweli” ni nini, nayo ‘yatakasaje’ Mkristo?
▪ Ni jinsi gani Mungu, Mwana wake, na waabudu wote wa kweli walivyo mmoja?
▪ “Kuwekwa msingi [wa] ulimwengu” kulikuwa wakati gani?
-