Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nafsi
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • inayotenda dhambi—hiyo yenyewe itakufa.” (*Neno la Kiebrania ni “neʹphesh.” ZSB hulitafsiri “nafsi.” Tafsiri fulani zinasema “roho,” “yeyote,” au “yule.”)

      Mt. 10:28: “Msiwaogope wale ambao wanaua mwili lakini hawawezi kuiua nafsi [au, “uhai”]; lakini badala ya hivyo mwogopeni yeye anayeweza kuangamiza vyote viwili nafsi* na mwili katika Gehena.” (*Neno la Kigiriki hapa ni psy·kheʹ. ZSB hulitafsiri “nafsi.”)

      Mdo. 3:23: “Kwa kweli, nafsi [Kigiriki, psy·kheʹ] yoyote isiyomsikiliza Nabii huyo itaangamizwa kutoka kati ya watu.”

      Je, nafsi za wanadamu (watu) zinaweza kuishi milele?

      Ona ukurasa wa 327-331, chini ya kichwa “Uhai.”

      Je, nafsi ni sawa na roho?

      Mhu. 12:7: “Kisha mavumbi huirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho [au, nguvu za uhai; Kiebrania, ruʹach] yenyewe humrudia Mungu wa kweli aliyeitoa.” (Ona kwamba neno la Kiebrania linalotafsiriwa roho ni ruʹach; lakini neno linalotafsiriwa nafsi ni neʹphesh. Andiko hilo halimaanishi kwamba wakati wa kifo roho inasafiri moja kwa moja na kwenda katika makao ya Mungu; badala yake, tazamio lolote la mtu huyo kuishi tena linakaa kwa Mungu. Kwa mfano, tunaweza kusema kwamba, ikiwa mnunuzi wa shamba hafanyi malipo yanayohitajiwa, shamba hilo “humrudia” mwenyewe.) (UV, ZSB, BHN, na VB zote hapa zinatafsiri ruʹach kuwa “roho.”)

      Mhu. 3:19: “Kuna mwisho ambao huwafikia wana wa binadamu na mwisho ambao huwafikia wanyama, nao hufikiwa na mwisho uleule. Anavyokufa mmoja, ndivyo anavyokufa yule mwingine; nao wote wana roho [Kiebrania, ruʹach] moja.” (Kwa hiyo wanadamu na wanyama pia wanaonyeshwa kuwa wana ruʹach au roho ileile. Ili kupata maelezo kuhusu mstari wa 20 na 21, ona ukurasa wa 245.)

      Ebr. 4:12: “Neno la Mungu liko hai nalo lina nguvu na ni lenye makali zaidi kuliko upanga wowote wenye makali kuwili nalo huchoma hata kufikia kugawanya nafsi [Kigiriki, psy·khesʹ; ] na roho [Kigiriki, pneuʹma·tos], na viungo na urojorojo wake, nalo linaweza kutambua fikira na makusudio ya moyo.” (Ona kwamba neno la Kigiriki linalotafsiriwa “roho” si sawa na neno linalotafsiriwa “nafsi.”)

      Je, mtu huendelea kuwa na fahamu baada ya roho kuuacha mwili?

      Zab. 146:4: “Roho [Kiebrania, kutokana na ruʹach] yake hutoka, naye hurudi kwenye udongo wake; siku hiyo mawazo yake hupotea.” (VB [145:4] hutafsiri neno ruʹach kuwa “roho.” Tafsiri fulani husema “pumzi.”) (Ona pia Zaburi 104:29)

      Imani ya Jumuiya ya Wakristo kuhusu nafsi isiyo na mwili, isiyoweza kufa ilitoka wapi?

      “Wazo la Kikristo la nafsi ya kiroho iliyoumbwa na Mungu na kutiwa katika mwili wakati wa kutungwa kwa mimba ili kufanyiza mwanadamu kuwa mtu kamili lilitokana na falsafa ya Kikristo iliyositawi kwa muda mrefu. Ni kupitia Origen tu [aliyekufa karibu mwaka wa 254 W.K.] upande wa Mashariki na Mtakatifu Agustino [aliyekufa mwaka wa 430 W.K.] upande wa Magharibi kwamba nafsi ilithibitishwa kuwa kitu cha kiroho na wazo la kifalsafa likafanyizwa kuhusu asili yake.  . . . Fundisho lake [la Agustino] . . . lilikuwa na mambo mengi (kutia ndani makosa fulani) yaliyotoka kwa Plato.”—New Catholic Encyclopedia (1967), Buku la 13, uku. 452, 454.

      “Wazo la kutoweza kufa lilitokana na Wagiriki, lakini tumaini la ufufuo lilitokana na Wayahudi. . . . Baada ya ushindi wa Aleksanda, mwishowe dini ya Kiyahudi ilichukua mawazo ya Kigiriki.”—Dictionnaire Encyclopédique de la Bible (Valence, Ufaransa; 1935), iliyohaririwa na Alexandre Westphal, Buku la 2, uku. 557.

      “Kutoweza kufa kwa nafsi ni wazo la Kigiriki lililofanyizwa katika madhehebu ya kale ya kifumbo na kupanuliwa na Plato mwanafalsafa.”—Presbyterian Life, Mei 1, 1970, uku. 35.

      “Je, tunaamini kwamba kuna kitu kama kifo? . . . Je, kifo si kutengana kwa nafsi na mwili? Na kufa ndio ukamilisho wa hilo; wakati nafsi inapoishi peke yake, na inapofunguliwa kutoka katika mwili na mwili unapofunguliwa kutoka katika nafsi, je, hicho si kifo? . . . Na je, nafsi inakubali kifo? Hapana. Basi nafsi haiwezi kufa? Ndiyo.”—“Phaedo” ya Plato, Sehemu ya 64, 105, kama ilivyochapishwa katika Great Books of the Western World (1952), kilichohaririwa na R. M. Hutchins, Buku la 7, uku. 223, 245, 246.

      “Tumeona kwamba, lile tatizo la kutoweza kufa liliwavutia sana wanatheolojia wa Babiloni. . . . Watu wala viongozi wa mafundisho ya kidini hawakupata kamwe kuukabili uwezekano wa kutoweka kabisa kwa kile ambacho hapo kwanza kiliumbwa. Kifo kilikuwa ni njia ya kuingia katika maisha mengine.”—The Religion of Babylonia and Assyria (Boston, 1898), M. Jastrow, Jr., uku. 556.

      Ona pia ukurasa wa 102-104, chini ya kichwa “Kifo.”

  • Ndoa
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Ndoa

      Maana: Muungano wa mwanamume na mwanamke ili kuishi pamoja wakiwa mume na mke kulingana na kiwango kilichowekwa katika Maandiko Matakatifu. Ndoa ni mpango wa Mungu. Inawezesha kuwepo uhusiano wa karibu sana kati ya mume na mke pamoja na hisia ya usalama kwa sababu kuna upendo na kwa sababu ya wajibu wa kibinafsi ambao umefanywa na kila mmoja wa wenzi hao. Alipokuwa akiianzisha ndoa, Yehova alifanya hivyo ili kumwandalia mwanamume mwenzi wa karibu ambaye angekuwa kikamilisho chake na pia kuanzisha njia ambayo wanadamu wangeweza kuzaana katika mpango wa familia. Inapohitajiwa, kuandikisha kisheria ndoa inayokubalika katika kutaniko la Kikristo ni takwa.

      Je, ni muhimu kufunga ndoa kupatana na matakwa ya kisheria?

      Tito 3:1: “Endelea kuwakumbusha wajitiishe na kuzitii serikali na mamlaka zikiwa watawala.” (Watu wanapotii maagizo hayo, kila mmoja katika muungano huo hawezi kushutumiwa, nao watoto hawashutumiwi kama watoto ambao wazazi wao hawajafunga ndoa. Pia, kuandikisha ndoa kisheria hulinda haki za mali za familia, ikiwa mmoja wa wenzi hao atakufa.)

      Ebr. 13:4: “Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi, kwa maana Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.” (Kufunga ndoa kisheria hutimiza sehemu muhimu katika kuwa na ndoa inayoonwa kuwa ‘yenye kuheshimiwa.’ Tunapoeleza maana ya maneno “uasherati” na “uzinzi,” lazima tukumbuke yanayosemwa katika andiko la Tito 3:1, lililotangulia kunukuliwa.)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki