Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Har–Magedoni
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Ni nini au ni nani watakaoharibiwa kwenye Har–Magedoni?

      Dan. 2:44: “Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme. . . . Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo.”

      Ufu. 19:17, 18: “Nikaona pia malaika amesimama katika jua, naye akapaaza kilio kwa sauti kubwa na kuwaambia ndege wote wanaoruka katikati ya mbingu: ‘Njooni hapa, mkusanyike pamoja kwenye mlo mkubwa wa jioni wa Mungu, ili mpate kula sehemu zenye nyama za wafalme na sehemu zenye nyama za viongozi wa kijeshi na sehemu zenye nyama za watu wenye nguvu na sehemu zenye nyama za farasi na za wale wanaoketi juu yao, na sehemu zenye nyama za wote, za watu huru na vilevile za watumwa na za wadogo na wakubwa.’”

      1 Yoh. 2:16, 17: “Kila kitu kilicho katika ulimwengu—tamaa ya mwili na tamaa ya macho na mtu kujionyesha mali yake maishani—hakitokani na Baba, bali hutokana na ulimwengu. Zaidi ya hayo, ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake, lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”

      Ufu. 21:8: “Lakini kwa habari ya waoga na wale wasio na imani na wale wenye kuchukiza katika uchafu wao na wauaji na waasherati na wale wanaozoea kuwasiliana na pepo na waabudu-sanamu na waongo wote, fungu lao litakuwa ndani ya lile  ziwa linalowaka moto na kiberiti. Hili linamaanisha kifo cha pili.”

      Je, uharibifu huo utakuwa wa milele?

      Mt. 25:46: “Na hawa [waliokataa kuwatendea “ndugu” za Kristo mema] watakatiliwa mbali milele, lakini waadilifu wataingia katika uzima wa milele.”

      2 The. 1:8, 9: “Wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu . . . watahukumiwa adhabu ya uharibifu wa milele.”

      Je, kutakuwako waokokaji?

      Sef. 2:3: “Mtafuteni Yehova, ninyi nyote mlio wapole wa dunia, ambao mmetenda uamuzi Wake wa hukumu. Utafuteni uadilifu, utafuteni upole. Huenda mkafichwa katika siku ya hasira ya Yehova.”

      Rom. 10:13: “Kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa.”

      Zab. 37:34: “Mtumaini Yehova na kuishika njia yake, naye atakuinua uimiliki dunia. Watu waovu watakapokatiliwa mbali, wewe utaona hilo.”

      Yoh. 3:16: “Mungu . . . akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee, ili kila mtu anayemwamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.”

      Ufu. 7:9, 10, 14: “Nikaona, na, tazama! umati mkubwa, ambao hakuna mtu aliyeweza kuuhesabu, kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha, wamesimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wamevikwa kanzu nyeupe; na kulikuwa na matawi ya mitende mikononi mwao. Nao wanaendelea kupaaza sauti kubwa, wakisema: ‘Wokovu unatoka kwa Mungu wetu, anayeketi juu ya kiti cha ufalme, na Mwana-Kondoo.’ . . . ‘Hawa ndio wale wanaotoka katika ile dhiki kuu.’”

      Ni nini kitakachowapata watoto wachanga kwenye Har–Magedoni?

      Biblia haijibu swali hilo moja kwa moja, wala sisi si waamuzi. Hata hivyo, Biblia inaonyesha kwamba Mungu anawaona watoto wachanga wa Wakristo wa kweli kuwa “watakatifu.” (1 Kor. 7:14) Inafunua pia kwamba katika nyakati za zamani Mungu alipowaharibu waovu aliwaharibu watoto wao pia. (Hes. 16:27, 32; Eze. 9:6) Mungu hataki mtu yeyote aharibiwe, hivyo anafanya onyo litolewe sasa ili kunufaisha wazazi na watoto pia. Je, halingekuwa jambo la hekima kwa wazazi kuishi maisha ambayo yatawafanya watoto wao wapate kibali cha Mungu sasa na wakati wa Har–Magedoni?

      Je, kuharibiwa kwa waovu kunaonyesha kwamba Mungu hana upendo?

      2 Pet. 3:9: “Yehova . . . ni mwenye subira kwenu kwa sababu hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.”

      Luka 18:7, 8: “Je, Mungu hatasababisha haki ifanywe kwa ajili ya watu wake waliochaguliwa ambao wanampaazia sauti mchana na usiku, hata ingawa ana ustahimilivu kwao? Ninawaambia ninyi, Yeye atasababisha watendewe haki upesi?”

      2 The. 1:6: “Ni jambo la uadilifu kwa upande wa Mungu kuwalipa dhiki wale wanaowafanyia ninyi [watumishi wake] dhiki.”

      Je, inawezekana kutounga mkono upande wowote?

      2 The. 1:8: “Anapoleta kisasi juu ya wale wasiomjua Mungu [kwa kuchagua] na wale wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.”

      Mt. 24:37-39: “Kama vile siku za Noa zilivyokuwa . . . hawakujali mpaka gharika ikaja na kuwafagilia mbali wote, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa.”

      Mt. 12:30: “Yeye asiyekuwa upande wangu ananipinga, naye asiyekusanya pamoja nami anatawanya.”

      Linganisha na Kumbukumbu la Torati 30:19, 20.

      Ni nani anayeyachochea mataifa kwenye hali ya ulimwengu itakayotokeza vita dhidi ya Mungu?

      Ufu. 16:13, 14; 12:9: “Nikaona maneno machafu matatu yaliyoongozwa na roho ambayo yalionekana kama vyura yakitoka katika kinywa cha yule joka mkubwa [Shetani Ibilisi; Ufu. 12:9] na kutoka katika kinywa cha yule mnyama-mwitu na kutoka katika kinywa cha yule nabii wa uwongo. Hayo, kwa kweli, ni maneno yanayoongozwa na roho waovu nayo yanafanya ishara, nayo yanakwenda kwa wafalme wa dunia nzima inayokaliwa, ili kuwakusanya pamoja kwa vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.”

      Linganisha na Luka 4:5, 6; 1 Yohana 5:19; pia Matendo 5:38, 39; 2 Mambo ya Nyakati 32:1, 16, 17.

  • Ibada ya Mababu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Ibada ya Mababu

      Maana: Zoea la kuwaheshimu na kuwaabudu mababu waliokufa (kwa kufanya sherehe au kwa njia nyingine) kwa sababu wanaamini kwamba mababu hao wanaishi katika makao yasiyoonekana na wanaweza kuwasaidia au kuwadhuru walio hai na kwa hiyo wanapaswa kutulizwa. Hilo si fundisho la Biblia.

      Je, mababu waliokufa wanajua mambo ambayo walio hai wanafanya, na je, mababu hao wanaweza kuwasaidia watu walio hai?

      Mhu. 9:5: “Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe.”

      Ayu. 14:10, 21: “Mtu wa udongo hukata pumzi, naye yuko wapi? Wanawe hupewa heshima, lakini yeye hajui hilo.”

      Zab. 49:10, 17-19: “Hata wenye hekima wanakufa, mjinga na asiyetumia akili huangamia wote pamoja, nao hulazimika kuwaachia wengine mali yao. . . . Anapokufa hawezi kuchukua kitu chochote; utukufu wake hautashuka chini pamoja naye. . . . Nafsi yake mwishowe inafikia tu kwenye kizazi cha mababu zake. Hawataona nuru tena kamwe.”

      Je, si kweli kwamba chakula kinachowekwa juu ya madhabahu au juu ya kaburi huwa hakiliwi? Je, hilo halionyeshi kwamba wafu hawawezi kukila?

      Ona pia kichwa, “Kuwasiliana na Pepo.”

      Je, kuna sababu ya kuogopa kwamba mababu zetu waliokufa watatudhuru?

      Mhu. 9:5, 6: “Lakini wafu, . . . upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari zimepotea, na mpaka wakati usio na kipimo hawana fungu lolote tena katika chochote ambacho kitafanywa chini ya jua.”

      Je, mtu ana roho inayoendelea kuishi baada ya mwili kufa?

      Eze. 18:4: “Tazama! Nafsi zote—ni zangu. Kama ilivyo nafsi ya baba ndivyo ilivyo nafsi ya mwana—ni zangu. Nafsi inayotenda dhambi—hiyo yenyewe itakufa.” (Ona pia mstari wa 20.)

      Zab. 146:3, 4: “Msiweke tegemeo lenu katika watu wenye vyeo, wala katika mtu wa udongo, . . . Roho yake hutoka, naye hurudi kwenye udongo wake; siku hiyo mawazo yake hupotea.”

      Wanasayansi na madaktari wa upasuaji hawajaona uthibitisho wa kuwapo kwa sehemu yoyote ya mwanadamu iliyo na ufahamu na inayoendelea kuishi baada ya mwili kufa.

      Ona pia ukurasa wa 102-104, chini ya kichwa, “Kifo.”

      Je, wewe ungependa watoto wako na wajukuu wako wakuheshimu na kukupenda wakati ungali hai au wafanye matambiko kwenye kaburi lako ukisha kufa?

      Efe. 6:2, 3: “‘Mheshimu baba yako na mama yako’; ambayo ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi: ‘Ili mambo yakuendee vema nawe ukae muda mrefu duniani.’” (Watoto waliofundishwa kanuni za Biblia wanaonyesha heshima hiyo inayofurahisha mioyo ya wazazi wao wakiwa wangali hai.)

      Met. 23:22: “Msikilize baba yako aliyekuzaa, wala usimdharau mama yako kwa sababu tu amezeeka.”

      1 Tim. 5:4: “Ikiwa mjane yeyote ana watoto au wajukuu, acha hao wajifunze kwanza kuzoea ujitoaji-kimungu nyumbani kwao wenyewe na kuendelea kuwalipa wazazi na wazazi wa wazazi wao malipo yanayowastahili, kwa maana hilo linakubalika machoni pa Mungu.”

      Watu wanaowasiliana na pepo wanapodai kuleta ujumbe kutoka kwa wafu, ujumbe huo unatoka wapi hasa?

      Isa. 8:19: “Nao wakiwaambia ninyi: ‘Toeni maombi kwa wenye kuwasiliana na pepo au kwa wale wenye roho ya kubashiri wanaonong’oneza na kusema maneno kwa sauti za chini,’ je, kundi lolote la watu halipaswi kutoa maombi kwa Mungu wake? Je, maombi yatolewe kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?” (Je, Mungu angetuonya tujiepushe na zoea hilo ikiwa kwa kweli linatuwezesha kuwasiliana na wapendwa wetu?)

      Mdo. 16:16: “Tulipokuwa tukienda pale mahali pa sala, kijakazi fulani mwenye roho, roho mwovu wa uaguzi, akakutana nasi. Yeye alikuwa akiwapatia mabwana zake faida nyingi kwa kufanya ufundi wa kubashiri.”

      Ona pia ukurasa wa 140, 141, chini ya kichwa, “Kuwasiliana na Pepo.”

      Ni nani tunayepaswa kumwabudu?

      Luka 4:8: “Yesu akajibu akamwambia: ‘Imeandikwa, “Yehova Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu, na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.”’”

      Yoh. 4:23, 24: “Saa inakuja, nayo ipo sasa, wakati ambapo waabudu wa kweli watamwabudu Baba kwa roho na kweli, kwa maana, kwa kweli, Baba anawatafuta watu wa namna hiyo wamwabudu. Mungu ni Roho, na wale wanaomwabudu lazima wamwabudu kwa roho na kweli.”

      Je, kuna tumaini kwamba wakati ujao washiriki wa familia, kutia ndani wale waliokufa, wataungana pamoja?

      Yoh. 5:28, 29: “Msistaajabie jambo hili, kwa sababu saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake na kutoka, wale waliotenda mambo mema kwenye ufufuo wa uzima, wale waliokuwa na zoea la kutenda mambo maovu kwenye ufufuo wa hukumu.”

  • Imani
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Imani

      Maana: “Imani ni tarajio lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa, uthibitisho ulio wazi wa mambo halisi ingawa hayaonekani.” (Ebr. 11:1) Imani ya kweli si kuamini jambo haraka-haraka bila uthibitisho mzuri au kwa sababu tu mtu anataka iwe hivyo. Ili mtu awe na imani ya kweli, anahitaji kuwa na ujuzi wa msingi, kujua uthibitisho, na pia kuthamini kutoka moyoni yale ambayo uthibitisho huo unaonyesha. Kwa hiyo, ijapokuwa haiwezekani kuwa na imani ya kweli bila ujuzi sahihi, Biblia inasema kwamba mtu huamini “kwa moyo.”—Rom. 10:10.

      Kwa nini watu wengi hawana imani?

      Imani ni tunda la roho ya Mungu, na kwa upendo Mungu huwapa roho yake wale wanaoitafuta. (Gal. 5:22; Luka 11:13) Basi watu wasio na imani hawaitafuti roho hiyo, au wanafanya hivyo kwa kusudi baya au wanapinga utendaji wa roho hiyo maishani mwao. Mambo mengi husababisha hali hiyo:

      Kutokuwa na ujuzi sahihi wa Biblia: Biblia imeandikwa kwa uongozi wa roho ya Mungu. (2 Tim. 3:16, 17; 2 Sam. 23:2) Mtu asipojifunza Biblia, hawezi kusitawisha imani ya kweli. Ijapokuwa huenda wanadini wakawa na Biblia, ikiwa

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki