Wimbo 59
Kuthamini Vikumbusho vya Mungu
1. Wa furaha wenye vikumbusho,
Mungu wamutafutao,
Kutimiza sheria upesi,
Wasiziache sheria.
Amuri zake wathamini,
Fadhili wanasimulia.
Sheria zake wazipendao,
Wamefunzwa kumungoja.
2. Fadhilize hazina kifani;
Zapenya sana angani!
Maamuzi yake yatulinda,
Ijapo tusingiziwe.
Wapenda sheria; amani.
Watabakia barakani.
Afurahivyo muteka nyara,
Furaha yetu ’tazidi.
3. Maombi tuweke kwa Yehova
Tufahamu Neno lake.
Asikie sala zetu ili
Tuokolewe na yeye.
Moyo wetu uaminike,
Tutende atuambiayo.
Mushikamanifu ni Yehova.
Hurudisha nguvu zetu.