Wimbo 156
“Nataka”
1. Yesu alituonyesha,
Upendo akaja chini,
Aishi na watu, Awape ukweli.
Na aliusema daima.
Na alifariji watu,
Aliwaponya wagonjwa.
Aliitimiza kazi yake,
Yeye alisema: “Nataka.”
2. Mungu alisaidia
Kutoa “mutumwa” wake
Tunayetumika Pamoja na yeye,
Tuponye wenye mahitaji!
Wao wanajua sisi
Tunapowapenda sana.
Wajane nao yatima pia,
Utawaambia: “Nataka”?
3. Kupenda Mungu kwafanya
Tuhubiri, tufundishe.
Wanaougua Na walioachwa;
Na tuwasaidie wao.
Ni shangwe wakifahamu
Kweli nzuri za Biblia,
Wafanye utumishi wa Mungu!
Kwani tumesema: “Nataka.”