Fuatia Kupendezwa kwa Utambuzi Wakati wa Majira ya Sikukuu
1 Desemba ni mwezi ambao wengi wa wale ambao wameonyesha kupendezwa katika ujumbe wetu wataelekea kuwa wenye shughuli na utendaji wa sikukuu. Kwa hiyo, tunapofuatia kupendezwa, tutahitaji kuwa wenye utambuzi na labda kuwa tayari kutaja jambo kuu kwa haraka, isipokuwa kama mwenye nyumba anaonyesha tamaa ya kuwa na mazungumzo marefu zaidi.
2 Fikiria Kimbele Yale Tutakayosema: Twapaswa sikuzote tujue vizuri yale tunayotaka kusema. Hilo lataka turejezee maandishi yetu juu ya ziara iliyopita na kujikumbusha kuhusu mambo yaliyoenezwa katika mazungumzo na swali lolote ambalo halikujibiwa lililoachwa na mwenye nyumba.
3 Ikiwa lile dokezo katika fungu la 5 la makala iliyo juu lilitumiwa, tunaporudi tungeweza kusema hivi:
◼ “Katika wakati huu wa mwaka, watu wengi wanafikiri juu ya kuzaliwa kwa Kristo. Mara ya mwisho tulipozungumza, niliahidi kushiriki pamoja na wewe jambo la hakika lenye kupendeza kuhusu jiji ambako Yesu alizaliwa. Je! ulijua kwamba Biblia ilitabiri miaka 700 kimbele kwamba Yesu angezaliwa Bethlehemu?” Ruhusu jibu. Halafu, baada ya kusoma Mika 5:2, ungeweza kusema hivi: “Huo ni unabii wenye kushangaza, sivyo? Ingawa hilo ni jambo la hakika la Kibiblia, je, ulijua ya kwamba unabii mwingi wa Biblia unatimizwa katika siku yetu?” Ikiwa mtu ana wakati, tungeweza kuendelea na mazungumzo, au ikiwa ana shughuli, twaweza kumtolea kurudi na kuzungumza zaidi juu ya hilo.
4 Kutoa Funzo la Biblia Nyumbani: Tukimwachia mwenye nyumba kitabu Mtu Mkuu Zaidi au ikiwa tayari ana nakala moja, ingekuwa vema kutoa wonyesho wa funzo la Biblia nyumbani kwa kutumia sura 111. Utaongozaje funzo hilo? Ungeweza kusoma habari yote iliyo chini ya kichwa kidogo (au sura nzima) na kisha kuuliza maswali yaliyo mwishoni mwa sura hiyo yanayolingana na sehemu iliyotoka kusomwa. Kumbuka kwamba majibu hayafuatani moja kwa moja katika sura sikuzote. Funzo likiendelea kufanya maendeleo, tungeweza kubadilisha na kujifunza mojayapo broshua au kwenda moja kwa moja kwenye kitabu Kuishi Milele.
5 Acheni tuwe tayari sikuzote kufuatia kupendezwa kwote. Ni lazima tuwe wenye utambuzi na kujitahidi sikuzote kufungulia njia ziara nyingine kwa kutokeza maswali yenye kupendeza mwishoni mwa kila mazungumzo. Hilo litatusaidia ‘tuwe tayari kabisa kwa kila kazi njema.’—2 Tim. 3:17, NW.