-
Urithi wa UpapaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Mitume, kwa sababu fundisho lake ndilo imani iliyofunuliwa kwa Mitume wakati mmoja, imani ambayo linalinda na kueleza, bila kuiongezea neno wala kuiondolea neno.” (London, 1957, W. E. Addis na T. Arnold, uku. 176) Je, mambo ya uhakika yanathibitisha hilo?
Mungu alivyo
“Utatu ndilo neno linalotumiwa kuonyesha fundisho kuu la dini ya Kikristo.”—The Catholic Encyclopedia (1912), Buku la 15, uku. 47.
“Neno Utatu, wala fundisho la wazi kama hilo, halionekani katika Agano Jipya . . . Fundisho hilo lilisitawishwa hatua kwa hatua kwa muda wa karne kadhaa na kwa mabishano mengi.”—The New Encyclopædia Britannica (1976), Macropædia, Buku la 10, uku. 126.
“Wafafanuzi na wanatheolojia wa Biblia, kutia ndani idadi inayoongezeka ya Wakatoliki, wanatambua kwamba haimpasi mtu kusema juu ya Utatu katika Agano Jipya bila ufafanuzi mzito. Pia, wanahistoria wa mafundisho ya kidini na wanatheolojia wanatambua kwamba mtu anaposema juu ya Utatu usiohitaji kufafanuliwa, huwa ameondoka katika kipindi cha mwanzo wa Ukristo akaingia, tuseme, kwenye ile robo ya mwisho ya karne ya 4.”—New Catholic Encyclopedia (1967), Buku la 14, uku. 295.
Useja wa makasisi
Papa Paulo wa Sita, katika waraka wake Sacerdotalis Caelibatus (Useja wa Makasisi, 1967), aliidhinisha useja kuwa takwa kwa makasisi, lakini alikiri kwamba “Agano Jipya linalohifadhi mafundisho ya Kristo na ya Mitume . . . halidai waziwazi useja wa wahudumu watakatifu . . . Yesu Mwenyewe hakuufanya uwe takwa Alipokuwa akiwachagua wale Kumi na Wawili, wala Mitume hawakudai wale waliosimamia jumuiya za kwanza za Kikristo wawe waseja.”—The Papal Encyclicals 1958-1981 (Falls Church, Va.; 1981), uku. 204.
1 Kor. 9:5, UV: “Hatuna uwezo kuchukua pamoja nasi mke aliye ndugu, kama wao mitume wengine, na ndugu wa Bwana, na Kefa?” (“Kefa” ni jina la Kiaramu alilopewa Petro; ona Yohana 1:42. Ona pia Marko 1:29-31, ambapo mama-mkewe wa Simoni, au Petro, anatajwa.)
1 Tim. 3:2, UV: “Basi imempasa askofu awe . . . mume wa mke mmoja [“ameoa mara moja tu,” NAB].”
Kabla ya enzi ya Ukristo, dini ya Ubudha iliwataka makasisi na watawa wake wa kiume wawe waseja. (History of Sacerdotal Celibacy in the Christian Church, London, 1932, chapa ya nne, iliyosahihishwa, Henry C. Lea, uku. 6) Hata mapema zaidi, makasisi wakuu wa Kibabiloni walitakiwa wawe waseja, kulingana na The Two Babylons cha A. Hislop.—(New York, 1943), uku. 219.
1 Tim. 4:1-3, UV: “Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; . . . wakiwazuia watu wasioe.”
Kujitenga na ulimwengu
Papa Paulo wa Sita, alipokuwa akihutubia Umoja wa Mataifa katika mwaka wa 1965, alisema hivi: “Watu wa dunia wanageukia Umoja wa Mataifa kuwa tumaini la mwisho la upatano na amani; Tunatoa sifa yao ya heshima na ya tumaini, pamoja na Yetu wenyewe.”—The Pope’s Visit (New York, 1965), Time-Life Special Report, uku. 26.
Yoh. 15:19, UV: “[Yesu Kristo akasema:] Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.”
Yak. 4:4, UV: “Hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu?”
Kutumia silaha za vita
Mwanahistoria Mkatoliki E. I. Watkin aliandika hivi: “Ingawa ni vigumu kukubali, hatuwezi kukataa wala kupuuza uhakika wa kihistoria kwamba nyakati zote Maaskofu wameunga mkono vita vyote vinavyopiganwa na serikali ya nchi yao ili kuendeleza mafundisho ya uwongo au ushikamanifu usio wa kweli. Kwa hakika, sijui kisa chochote ambapo makasisi wa taifa walishutumu vikali vita vyovyote kuwa si vya haki . . . Hata nadharia rasmi iwe gani, kwa matendo, wakati wa vita Maaskofu wa Wakatoliki wamefuata kanuni ya kwamba ‘nchi yangu ni sawa sikuzote.’”—Morals and Missiles (London, 1959), kilichohaririwa na Charles S. Thompson, uku. 57, 58.
Mt. 26:52, UV: “Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga.”
1 Yoh. 3:10-12, BHN: “Asiyempenda ndugu yake, huyo si mtoto wa Mungu. Hiyo ndiyo tofauti iliyoko kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi. . . . Tunapaswa kupendana! Tusiwe kama Kaini ambaye, kwa kuongozwa na yule Mwovu, alimwua ndugu yake.”
Kutokana na yaliyotangulia, je, kwa kweli wale wanaodai kuwa warithi wa mitume wamefundisha na kutenda yale ambayo Kristo na mitume wake walitenda?
-
-
UtatuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Utatu
Maana: Fundisho kuu la dini za Jumuiya ya Wakristo. Kulingana na Imani ya Athanasia, kuna Watu watatu wa kimungu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu), inasemekana kwamba kila mmoja ni wa milele, kila mmoja ni mweza-yote, hakuna aliye mkubwa au mdogo kuliko mwingine, kila mmoja ni Mungu, na hata hivyo wote pamoja ni Mungu mmoja tu. Maelezo mengine kuhusu fundisho hilo hukazia kwamba hao “Watu” watatu si watu mbalimbali bali ni maumbo matatu ambayo Mungu hukaa ndani yake. Kwa hiyo Wana-Utatu fulani hukazia imani yao kwamba Yesu Kristo ni Mungu, au kwamba Yesu na Roho Mtakatifu ni Yehova. Hilo si fundisho la Biblia.
Fundisho la Utatu lilitoka wapi?
The New Encyclopædia Britannica husema: “Neno Utatu, wala fundisho la wazi kama hilo, halipatikani katika Agano Jipya, wala Yesu na wafuasi wake hawakukusudia kupinga ile Shema katika Agano la Kale: ‘Sikiliza, Ee Israeli; BWANA, Mungu wetu, BWANA, ndiye mmoja’ (Kum. 6:4). . . . Fundisho hilo lilisitawi hatua kwa hatua kwa muda wa karne kadhaa na kupitia mabishano mengi. . . . Kufikia mwisho wa karne ya 4 . . . fundisho la Utatu likawa jinsi lilivyo leo hii.”—(1976), Micropædia, Buku la 10, uku. 126.
New Catholic Encyclopedia hueleza hivi: “Maneno ‘Mungu mmoja katika Watu watatu’ hayakuthibitishwa imara, nayo hayakuwa sehemu kamili ya maisha ya Wakristo na imani yao, kabla ya mwisho wa karne ya 4. Lakini ni maneno hayo hasa ambayo yalianza kuitwa kwanza fundisho la Utatu. Kati ya Mababa wa Kimitume, hakukuwa na jambo lolote linalokaribia hata kidogo mawazo au maoni hayo.”—(1967), Buku la 14, uku. 299.
Katika The Encyclopedia Americana tunasoma hivi: “Ukristo ulitokana na dini ya Kiyahudi na dini ya Kiyahudi iliamini kabisa Umoja [waliamini kwamba Mungu ni mtu mmoja tu]. Imani ya Utatu ya karne ya nne haikuonyesha kwa usahihi fundisho la kwanza la Kikristo kuhusu umbo la Mungu; badala ya hivyo, ilikuwa imepotoka kutoka katika fundisho hili.”—(1956), Buku la 27, uku. 294L.
Kulingana na kichapo Nouveau Dictionnaire Universel, “Utatu wa Plato, ambao wenyewe ulikuwa ni kupangwa upya tu kwa miungu mitatu-mitatu ya watu wa zamani, unaonekana kuwa ndio utatu unaopatana na akili ya kifalsafa ya sifa zilizotokeza yale maumbo matatu au watu wa kimungu ambao makanisa ya Kikristo hufundisha. . . . Wazo hili la mwanafalsafa Mgiriki [Plato, karne ya nne K.W.K.] la utatu wa kimungu . . . linapatikana katika dini zote za kale [za kipagani].”—(Paris, 1865-1870), kilichohaririwa na M. Lachâtre, Buku la 2, uku. 1467.
John L. McKenzie, S.J., katika kitabu chake Dictionary of the Bible, anasema: “Utatu wa watu katika umoja wa asili hufafanuliwa katika maneno ya ‘mtu’ na ‘asili’ ambayo ni maneno ya kifalsafa ya Kigiriki; kwa hakika maneno hayo hayapatikani katika Biblia. Mafafanuzi ya utatu yalitokana na mabishano ya muda mrefu ambapo maneno hayo na mengine kama vile ‘asili iliyoko ya vitu vyote’ na ‘asili kuu,’ yalitumiwa kimakosa na wanatheolojia fulani kumhusu Mungu.”—(New York, 1965), uku. 899.
Hata ingawa, kama vile Wana-Utatu wanavyokubali, neno “Utatu” wala fundisho la Utatu halipatikani katika Biblia, je, mawazo yanayotiwa katika fundisho hilo yanapatikana humo?
Je, Biblia hufundisha kwamba “Roho Mtakatifu” ni mtu?
Maandiko fulani yanayotaja roho takatifu (“Roho Mtakatifu,” UV) huenda yakaonekana kumaanisha mtu. Kwa mfano, roho takatifu huitwa msaidizi (Kigiriki, pa·raʹkle·tos; “Mtulizaji,” VB) ambaye ‘hufundisha,’ ‘hutoa ushahidi,’ ‘husema’ na ‘husikia.’ (Yoh. 14:16, 17, 26; 15:26; 16:13) Lakini maandiko mengine husema kwamba watu ‘walijazwa’ roho takatifu, kwamba wengine ‘walibatizwa’ nayo au ‘walipakwa mafuta’ nayo. (Luka 1:41; Mt. 3:11; Mdo. 10:38) Bila shaka maandiko hayo ya mwisho yanayoitaja roho hayawezi kurejelea mtu. Ili kuelewa yale ambayo Biblia hufundisha kwa ujumla, ni lazima maandiko hayo yote yafikiriwe. Ni jambo gani linalopatana na akili? Kwamba maandiko ya kwanza yaliyotajwa hapa yanatumia maneno ya mfano, yanayoifanya roho takatifu ya Mungu au nguvu zake za utendaji, zionekane kuwa kama mtu. Biblia hufanya vivyo hivyo kuhusu maneno kama vile hekima, dhambi, kifo, maji, na damu. (Ona pia ukurasa wa 242, 243, chini ya kichwa “Roho.”)
Maandiko Matakatifu hutuambia jina la Baba—Yehova. Yanatuambia kwamba Mwana ni Yesu Kristo. Lakini hakuna popote katika Maandiko ambapo jina la kibinafsi linatumiwa kuhusu roho takatifu.
Andiko la Matendo 7:55, 56 husema kwamba Stefano alionyeshwa maono ya mbinguni ambapo alimwona “Yesu akiwa amesimama kwenye mkono wa kuume wa Mungu.” Lakini yeye hakusema lolote kuhusu kuiona roho takatifu. (Ona pia Ufunuo 7:10; 22:1, 3.)
New Catholic Encyclopedia hukubali hivi: “Maandiko mengi ya A[gano] J[ipya] huonyesha roho ya Mungu kuwa kitu, wala si mtu; jambo hilo linaonekana hasa kutokana na ulinganifu uliopo kati ya roho na nguvu za Mungu.” (1967, Buku la 13, uku. 575) Pia inasema hivi: “Watetea-Imani [waandikaji Wakristo wa Kigiriki wa karne ya pili] walisema kwa kusita-sita mno juu ya Roho; kwa kufikiria mambo yaliyotukia baadaye, mtu anaweza kusema kwamba walisema bila kuonyesha ni mtu.”—Buku la 14, uku. 296.
Je, Biblia inakubaliana na wale wanaofundisha kwamba Baba na Mwana si watu tofauti?
Mt. 26:39, UV: “Akaendelea mbele kidogo, [Yesu Kristo] akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; lakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.” (Ikiwa Baba na
-