Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kifo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • wangekuwa wakichukua maumbo ya watu waliokufa na kuwapotosha wanadamu kwa kutia katika akili zao maoni ambayo yanaendeleza uwongo, je, halingekuwa jambo la upendo kwa Mungu kuwalinda watumishi wake dhidi ya udanganyifu huo?—Efe. 6:11, 12.

      Kwa nini Mashahidi wa Yehova hawashiriki katika desturi za kimapokeo za kuwaomboleza wafu?

      Mpendwa wetu anapokufa, ni jambo la kawaida kuwa na huzuni, na si kosa kuonyesha huzuni

      Baada ya kifo cha rafiki yake mkubwa Lazaro, ‘Yesu alitokwa na machozi.’ (Yoh. 11:35) Mara nyingine watumishi wa Mungu hupatwa na huzuni nyingi kwa sababu ya kifo.—2 Sam. 1:11, 12.

      Lakini kwa sababu ya tumaini la ufufuo, Wakristo wanaambiwa hivi: “Hatutaki mkose kujua kuhusu wale walalao usingizi katika kifo; ili msiwe na huzuni kama wale watu wengine wasio na tumaini.”—1 The. 4:13.

      Watumishi wa Yehova hawakatai desturi zote zinazohusiana na kifo

      Mwa. 50:2, 3: “Yosefu akawaamuru watumishi wake, matabibu, wampake baba yake dawa ya kumfanya asioze . . . nao wakatumia siku 40 kamili kwa ajili yake, kwa maana hiyo ndiyo hesabu ya siku ambazo kwa desturi wao hutumia kupaka dawa ya kumfanya mtu asioze.”

      Yoh. 19:40: “Wakauchukua mwili wa Yesu na kuufunga kwa vitambaa pamoja na manukato, sawa na jinsi Wayahudi walivyo na desturi ya kutayarisha kwa ajili ya maziko.”

      Watu wanaotaka kumpendeza Mungu huepuka desturi ambazo hazipatani na Neno lake

      Desturi fulani huonyesha waziwazi huzuni ya mtu. Lakini Yesu alisema: “Wakati mnapofunga [kwa sababu ya huzuni], msiwe na nyuso zenye huzuni kama wanafiki, kwa maana wao hukunja nyuso zao ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Kwa kweli ninawaambia ninyi, Wanapata thawabu yao kwa ukamili. Lakini wewe, unapofunga, paka kichwa chako mafuta na unawe uso wako, ili uonekane kuwa unafunga, si na wanadamu, bali na Baba yako aliye mahali pa siri; ndipo Baba yako anayetazama akiwa mahali pa siri atakulipa.”—Mt. 6:16-18.

      Desturi fulani zinatokana na imani ya kwamba mtu ana nafsi isiyoweza kufa ambayo huendelea kuishi baada ya mwili kufa na, kwa hiyo, inajua yale ambayo walio hai wanafanya. Lakini Biblia inasema hivi: “Wafu . . . hawajui lolote kamwe.” (Mhu. 9:5) Pia, “Nafsi inayotenda dhambi—hiyo yenyewe itakufa.”—Eze. 18:4.

      Desturi nyingi hutokana na imani ya kwamba wafu wanahitaji msaada wa walio hai au hutokana na kuogopa kwamba huenda wafu wakawadhuru walio hai ikiwa hawatatulizwa. Lakini Neno la Mungu linaonyesha kwamba wafu hawahisi maumivu wala raha. “Roho yake hutoka, naye hurudi kwenye udongo wake; siku hiyo mawazo yake hupotea.” (Zab. 146:4; ona pia 2 Sam. 12:22, 23.) “Upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari zimepotea, na mpaka wakati usio na kipimo hawana fungu lolote tena katika chochote ambacho kitafanywa chini ya jua.”—Mhu. 9:6.

      Mtu Akisema—

      ‘Ni mapenzi ya Mungu’

      Unaweza kujibu: ‘Watu wengi huamini hivyo. Lakini nimeona ni muhimu kuchunguza yale ambayo Mungu anasema kuhusu jambo hilo.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘(Soma Mwanzo 2:17.) Baba akimwonya mwanawe kwamba kufanya jambo fulani kutahatarisha uhai wake, je, ungesema kwamba baba huyo anataka mwanawe afanye jambo hilo?’ (2) ‘Basi mapenzi ya Mungu kuwahusu wanadamu ni nini? Yesu alisema hivi: “Haya ndiyo mapenzi ya Baba yangu, kwamba kila mtu ambaye humtazama Mwana [yaani, anatambua na kukiri kwamba Yesu kwa kweli ndiye Mwana wa Mungu] na kumwamini awe na uzima wa milele, nami nitamfufua katika siku ya mwisho.” (Yoh. 6:40)’

      ‘Watu wataendelea kufa sikuzote’

      Unaweza kujibu: ‘Wanadamu wamekuwa wakifa mpaka leo hii, sivyo?’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Lakini ona ahadi hii nzuri ajabu ambayo Mungu anatoa katika Ufunuo 21:3, 4 (au Isaya 25:8).’

      ‘Mtu hufa wakati wake unapofika’

      Unaweza kujibu: ‘Watu wengi wana maoni kama yako. Je, unajua kwamba Wagiriki wengi wa kale walikuwa na maoni hayohayo? Waliamini kwamba kulikuwa na miungu mitatu ya kike iliyoamua muda ambao kila mwanadamu angeishi. Lakini Biblia ina maoni tofauti kabisa kuhusu maisha.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘(Soma Mhubiri 9:11.) Mfano: Jiwe linaweza kuvunjika kutoka kwenye nyumba na kumwangukia mpita-njia. Je, Mungu ndiye aliyesababisha jambo hilo? Ikiwa hivyo ndivyo ilivyo, je, ni haki kumshtaki mwenye nyumba kwa sababu ya uzembe? . . . Kama Biblia inavyosema, kwa mpita-njia huyo, tukio hilo halikuwa limepangwa mapema wala halikuwa limetarajiwa, bali alikuwa papo hapo wakati jiwe hilo lilipoanguka.’ (2) ‘Biblia inatuambia kwamba tukiepuka mwenendo mbaya, tutaulinda uhai wetu. (Met. 16:17) Ikiwa wewe ni mzazi, nina hakika kwamba unatumia kanuni hiyohiyo unapowafundisha watoto wako. Unawaonya juu ya mambo ambayo yanaweza kusababisha kifo. Yehova anawafanyia wanadamu wote jambo hilohilo leo.’ (3) ‘Yehova anajua yatakayotokea wakati ujao. Kupitia Biblia yeye anatuambia jinsi tunavyoweza kufurahia maisha marefu zaidi kuliko yale ya watu wanaopuuza maneno yake. (Yoh. 17:3; Met. 12:28)’ (Ona pia kichwa, “Majaliwa.”)

  • Kitia-Moyo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kitia-Moyo

      Maana: Jambo linalomtia mtu moyo au kumpa tumaini. Kila mtu anahitaji kutiwa moyo. Mtu anaweza kumtia mwingine moyo kwa kumsaidia au kwa kumshukuru. Mara nyingi huhusisha kumsaidia mtu aone jinsi ya kukabiliana na hali ngumu au kuzungumzia sababu za kuwa na hakika katika wakati ujao ulio bora. Biblia ina msingi bora zaidi wa kitia-moyo hicho, na maandiko yaliyonukuliwa hapa yanaweza kukusaidia unapowatia moyo watu wanaokabili matatizo mbalimbali. Wakati mwingine, mtu anaweza kumsaidia sana mwingine kwa kumsikitikia tu.—Rom. 12:15.

      Kwa wale wanaoteseka kwa sababu ya UGONJWA—

      Ufu. 21:4, 5: “‘[Mungu] atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki