Wimbo 162
“Lihubiri Neno”!
1. “Lihubiri neno,” sasa
Ni amuri ya Mungu.
Tuna wakati tutii
Amuri ya Kimungu.
‘Hubiri Neno’ fundisha;
Elewesha wapole.
Bila hofu, kuhubiri
Barabarani kote.
2. ‘Hubiri’ kila wakati,
Uwe tayari kupa
Kila anayeuliza
Unayotumaini.
‘Hubiri,’ japo kupinga
Muda usiofaa.
Mwaminifu kwa agizo;
Mutumaini Mungu.
3. “Lihubiri Neno” bila
Kukoma, wasikie!
Uovu waongezeka.
Na mwisho u karibu.
‘Hubiri Neno,’ wokovu
Kwako na kwa wengine.
‘Hubiri Neno,’ karibu
Yehova atetewe.