-
DhambiKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Je, siku hizi kweli kuna “dhambi”?
Mfano: Mgonjwa akivunja kipima-joto, je, hilo linathibitisha kwamba yeye si mgonjwa? Mwizi akisema kwamba haamini yaliyoandikwa katika vitabu vya sheria, je, hilo litamfanya asiwe na hatia ya uhalifu? Hali kadhalika, uhakika wa kwamba watu wengi wanaamini kwamba si lazima kuishi kulingana na viwango vya Biblia haukomeshi dhambi.—Ona 1 Yohana 1:8.
Huenda watu fulani wakachagua kutenda yale ambayo Neno la Mungu linakataza. Lakini hilo halithibitishi kwamba Biblia ina makosa. Andiko la Wagalatia 6:7, 8 huonya hivi: “Msipotoshwe: Mungu si wa kudhihakiwa. Kwa maana lolote lile analopanda mtu, atavuna hilo pia; kwa sababu yeye anayepanda kwa mwili wake atavuna uharibifu kutokana na mwili wake.” Kuenea kwa magonjwa yanayotokana na ngono, familia zilizovunjika, na kadhalika, kunathibitisha ukweli wa yale ambayo Biblia inasema. Mungu alimuumba mwanadamu; Yeye anajua kitakachotuletea furaha yenye kudumu; Yeye anatuambia mambo hayo katika Biblia. Je, si jambo la busara kumsikiliza? (Ili kupata uthibitisho wa kuwako kwa Mungu, ona kichwa “Mungu.”)
Mambo mengi yanayoitwa dhambi, je, si mambo ya kawaida tu ambayo wanadamu hufanya?
Je, ngono ni dhambi? Je, Adamu na Hawa walitenda dhambi kwa kufanya ngono? Biblia haisemi hivyo. Andiko la Mwanzo 1:28 linasema kwamba Mungu mwenyewe aliwaambia Adamu na Hawa ‘wazae na kuwa wengi na kuijaza dunia.’ Ili kufanya hivyo, je, hawangekuwa na mahusiano ya ngono kati yao? Na andiko la Zaburi 127:3 linasema kwamba “wana ni urithi kutoka kwa Yehova,” kwamba wao ni “thawabu.” Kumbuka kwamba Hawa alikula kwanza tunda lililokatazwa na alifanya hivyo akiwa peke yake; ndipo baadaye akampa Adamu sehemu yake. (Mwa. 3:6) Kwa wazi, mti uliozaa lile tunda lililokatazwa ulikuwa mti halisi. Kile ambacho Biblia inakataza si mahusiano ya ngono ya kawaida kati ya mume na mke bali mambo kama vile uasherati, uzinzi, ngono kati ya watu wa jinsia moja, na ngono na mnyama. Matokeo mabaya ya matendo hayo yanaonyesha kwamba katazo hilo linathibitisha Yule anayejua jinsi tulivyoumbwa anatupenda.
Mwa. 1:27: “Mungu akamuumba mtu [Adamu] kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimuumba.” (Kwa hiyo, jambo ambalo ni sawa kwa Adamu lilikuwa kuonyesha sifa takatifu za Mungu, kukubali na kuthamini mwelekezo wa Mungu. Kukosa kufanya hivyo kulikuwa ni kukosa kuifikia alama, kufanya dhambi. Ona Waroma 3:23, pia 1 Petro 1:14-16.)
Efe. 2:1-3: “Ninyi [Wakristo] ndio ambao Mungu alifanya kuwa hai ingawa mlikuwa wafu katika makosa na dhambi zenu, ambazo wakati fulani mlitembea ndani yake kulingana na mfumo wa mambo wa ulimwengu huu, kulingana na mtawala wa mamlaka ya hewa, roho ambayo sasa hutenda katika wana wa kutotii. Ndiyo, wakati fulani sisi sote tulijiendesha katikati yao kupatana na tamaa za mwili wetu, tukifanya mambo yanayopendwa na mwili na fikira, nasi kiasili tulikuwa watoto wa ghadhabu sawa na wale wengine.” (Tukiwa wazao wa Adamu mtenda-dhambi, sisi tulizaliwa katika dhambi. Tangu kuzaliwa, moyo wetu una mwelekeo wa kutenda mabaya. Tusipozuia maelekeo hayo mabaya, huenda mwishowe tukaizoea njia hiyo ya maisha. Huenda hata ikaonekana kuwa “jambo la kawaida” kwa sababu wengine walio karibu nasi wanafanya mambo hayo. Lakini Biblia inatambulisha yaliyo mema na yaliyo mabaya kwa maoni ya Mungu, kwa sababu ya jinsi alivyomfanya mwanadamu na kusudi lake kwa wanadamu. Tukimsikiliza Muumba wetu na kumtii kwa upendo, maisha yatakuwa yenye maana sana kwa kadiri tusivyopata kujua, nasi tutakuwa na wakati ujao wa milele. Muumba wetu anatukaribisha kwa uchangamfu tuonje ili tuone jinsi maisha hayo yalivyo mazuri.—Zab. 34:8.)
Dhambi ina matokeo gani juu ya uhusiano wa mtu na Mungu?
1 Yoh. 3:4, 8: “Kila mtu aliye na mazoea ya kufanya dhambi anazoea pia kufanya uasi-sheria, na kwa hiyo dhambi ni uasi-sheria. Yeye ambaye huendelea kufanya dhambi hutokana na Ibilisi.” (Jambo hilo ni zito kama nini! Wale wanaochagua kimakusudi maisha ya dhambi, wakizoea kuitenda, Mungu anawaona kuwa wahalifu. Njia ambayo wamechagua ndiyo ile ambayo Shetani mwenyewe alichagua pale mwanzoni.)
Rom. 5:8, 10: “Tulipokuwa tungali watenda-dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu. . . . Tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kupitia kifo cha Mwana wake.” (Ona kwamba watenda-dhambi wanaitwa adui za Mungu. Basi, ni jambo la hekima kama nini kujifaidi wenyewe na uandalizi ambao Mungu amefanya ili tupatanishwe naye!)
1 Tim. 1:13: “Nilionyeshwa rehema [asema mtume Paulo], kwa sababu nilikosa ujuzi nami nilitenda kwa ukosefu wa imani.” (Lakini Bwana alipomwonyesha njia iliyo sawa, hakukataa kuifuata.)
2 Kor. 6:1, 2: “Tukifanya kazi pamoja naye, tunawasihi ninyi pia msipokee fadhili zisizostahiliwa za Mungu kisha mkose kusudi lake. Kwa maana anasema: ‘Katika wakati unaokubalika nilikusikia, na katika siku ya wokovu nilikusaidia.’ Tazama! Sasa ndio wakati unaokubalika hasa. Tazama! Sasa ndiyo siku ya wokovu.” (Sasa ndio wakati ambapo nafasi ya wokovu inapatikana. Mungu hatawaonyesha milele wanadamu wenye dhambi fadhili hizo zisizostahiliwa. Kwa hiyo, tunapaswa kuwa waangalifu ili tusikose kusudi la fadhili hizo.)
Dhambi inaweza kuondolewaje?
Ona kichwa, “Fidia.”
-
-
DiniKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Dini
Maana: Namna ya ibada. Inatia ndani maoni ya kidini, imani, na mazoea; hayo huenda yakawa ya kibinafsi, au yakaungwa mkono na tengenezo fulani. Kwa kawaida dini inatia ndani imani katika Mungu au katika miungu kadhaa; au huona wanadamu, vitu, tamaa, au nguvu fulani kuwa vitu vya kuabudiwa. Dini nyingi zinategemea uchunguzi wa wanadamu juu ya mambo ya asili; pia kuna dini iliyofunuliwa. Kuna dini ya kweli na ya uwongo.
Kwa nini kuna dini nyingi sana?
Kadirio lililofanywa karibuni lilionyesha kwamba kuna dini kubwa 10 na madhehebu 10,000. Kati ya hizo, 6,000 ziko Afrika, 1,200 ziko Marekani, na mamia katika nchi nyingine.
Mambo mengi yamesababisha kuongezeka kwa vikundi vipya vya kidini. Wengine wamesema kwamba dini hizo zote ni njia mbalimbali za kutoa kweli ya kidini. Lakini unapolinganisha mafundisho na mazoea yake pamoja na Biblia utaona kwamba kuna dini nyingi kwa sababu watu wanawafuata wanadamu badala ya kumsikiliza Mungu. Inafaa kuangaliwa kwamba, kwa kadiri kubwa, mafundisho ambayo wote wanashikilia, lakini yanayotofautiana na Biblia, yalianzia Babiloni la kale. (Ona ukurasa wa 28-30, chini ya kichwa “Babiloni Mkubwa.”)
Ni nani aliyeanzisha mvurugo huo wa kidini? Biblia inamtambulisha Shetani Ibilisi kuwa “mungu wa mfumo huu wa mambo.” (2 Kor. 4:4) Inatuonya kwamba “vitu ambavyo mataifa huvitoa dhabihu wao huvitoa dhabihu kwa roho waovu, na si kwa Mungu.” (1 Kor. 10:20) Basi ni jambo muhimu kama nini kuhakikisha kwamba tunamwabudu Mungu wa kweli, yule Muumba wa dunia na mbingu, na kwamba ibada yetu inampendeza!
Je, dini zote zinakubalika kwa Mungu?
Amu. 10:6, 7: “Wana wa Israeli wakaanza tena kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, nao wakaanza kutumikia Mabaali na sanamu za Ashtorethi na miungu ya Siria na miungu ya Sidoni na miungu ya Moabu na miungu ya wana wa Amoni na miungu ya Wafilisti. Basi wakamwacha Yehova wala hawakumtumikia yeye. Hivyo hasira ya Yehova ikawaka juu ya Israeli.” (Ikiwa mtu anaabudu kitu chochote au mtu yeyote badala ya Mungu wa kweli, Muumba wa mbingu na dunia, ni wazi kwamba ibada yake haikubaliki kwa Yehova.)
Marko 7:6, 7: “[Yesu] akawaambia [Mafarisayo na waandishi Wayahudi]: ‘Isaya kwa kufaa alitoa unabii juu yenu wanafiki, kama ilivyoandikwa, “Watu hawa huniheshimu mimi kwa midomo yao, bali mioyo yao iko mbali nami. Wao huniabudu bure, kwa sababu wao hufundisha amri za wanadamu kuwa mafundisho.”’” (Hata kikundi fulani kikidai kwamba kinamwabudu Mungu, ikiwa kinashikilia mafundisho ya wanadamu badala ya Neno la Mungu lililoongozwa na roho, ibada yake ni bure.)
Rom. 10:2, 3: “Nawatolea ushahidi kwamba wana bidii kwa ajili ya Mungu; lakini si kulingana na ujuzi sahihi; kwa maana, kwa sababu ya kukosa kujua uadilifu wa Mungu bali wakitafuta kujiwekea uadilifu wao wenyewe, hawakujitiisha kwa uadilifu wa Mungu.” (Huenda watu wakawa na Neno la Mungu lililoandikwa lakini wakakosa ujuzi sahihi wa mambo yaliyomo, kwa sababu hawakufundishwa sawasawa. Huenda wakaona kwamba wana bidii kwa ajili ya Mungu, lakini huenda hawafanyi yale anayotaka. Je, ibada yao itampendeza Mungu?)
Je, ni kweli kwamba kuna wema katika dini zote?
Dini nyingi hufundisha kwamba mtu hapaswi kusema uwongo wala kuiba, na kadhalika. Lakini hilo linatosha? Je, wewe utakubali kunywa kikombe cha maji yenye sumu kwa sababu mtu fulani amekuhakikishia kwamba katika kikombe hicho sehemu kubwa ni maji?
2 Kor. 11:14, 15: “Shetani mwenyewe huendelea kujigeuza mwenyewe kuwa malaika wa nuru. Kwa hiyo si jambo kubwa kama wahudumu wake wakiendelea pia kujigeuza wenyewe kuwa wahudumu wa uadilifu.” (Hapa tunatahadharishwa kwamba si kila kitu kinachotoka kwa Shetani kitakachoonekana kuwa kibaya sana. Moja ya njia zake kuu za kuwadanganya wanadamu ni dini za uwongo, naye huzifanya baadhi ya dini hizo zionekane kuwa zenye uadilifu.)
2 Tim. 3:2, 5: “Watu watakuwa . . . na namna ya ujitoaji-kimungu lakini wakizikana nguvu zake; nawe geukia mbali kutoka kwa hao.” (Hata watu unaoshirikiana nao katika ibada wakidai jinsi gani kwamba wanampenda Mungu lakini hawafuati kwa unyoofu Neno lake katika maisha yao, Biblia inakusihi uvunjilie mbali ushirika huo.)
Je, inafaa mtu kuiacha dini ya wazazi wake?
Ikiwa kwa kweli mambo ambayo wazazi wetu walitufundisha yanatoka katika Biblia, tunapaswa kuyashikilia. Tunastahili kuwaheshimu wazazi wetu, hata kama tunajua kwamba matendo na imani zao za kidini hazipatani na Neno la Mungu. Lakini namna gani ukijua kwamba zoea fulani la wazazi wako ni hatari kwa afya na linaweza kufupisha uhai wa mtu? Je, utawaiga na kuwatia moyo watoto wako wafanye hivyo, au je, utawaeleza kwa heshima yale uliyojifunza? Vivyo hivyo, kujua kweli ya Biblia huleta daraka. Ikiwezekana, tunapaswa kuwaeleza watu wa familia zetu mambo tunayojifunza. Ni lazima tufanye uamuzi: Je, kweli tunampenda Mungu? Je, kweli tunataka kumtii Mwana wa Mungu? Basi, huenda tukahitaji kuiacha dini ya wazazi wetu ili tufuate ibada ya kweli. Kwa hakika haingefaa kuruhusu uaminifu wetu kwa wazazi wetu uwe mkubwa kuliko upendo wetu kwa Mungu na Kristo, sivyo? Yesu alisema hivi: “Anayempenda baba au mama kuliko mimi hanistahili; naye anayempenda mwana au binti kuliko mimi hanistahili.” (Mt. 10:37).
Yos. 24:14: “Sasa mwogopeni Yehova na kumtumikia kwa njia isiyo na kosa na katika kweli, nanyi ondoeni miungu ambayo mababu zenu waliitumikia ng’ambo ile nyingine ya Mto na katika Misri, mkamtumikie Yehova.” (Hilo lilimaanisha waiache dini ya mababu zao, sivyo? Ili kumtumikia Yehova kwa njia inayokubalika, walipaswa kuondolea mbali sanamu zozote walizotumia katika dini hiyo na kusafisha mioyo yao ili kuondoa tamaa yoyote ya vitu hivyo.)
1 Pet. 1:18, 19: “Mnajua kuwa si kwa vitu vyenye kuharibika, kwa fedha au dhahabu, kwamba mlikombolewa kutoka kwenye namna ya mwenendo wenu usiozaa matunda ambao ulipokewa kwa njia ya mapokeo kutoka kwa mababu zenu. Bali ilikuwa kwa damu yenye thamani, kama ile ya mwana-kondoo asiye na dosari na asiye na doa, ile ya Kristo.” (Wakristo wa kwanza waliacha desturi hizo za mababu zao, ambazo hazingeweza kuwapa uzima wa milele. Shukrani kwa dhabihu ya Kristo iliwafanya watamani kuondoa chochote kilichofanya maisha yao yasiwe na kusudi kwa sababu desturi hizo hazikumheshimu Mungu. Je, sisi hatupaswi kuwa na mtazamo huohuo?)
Maoni ya Biblia ni nini kuhusu kuchanganya imani mbalimbali?
Yesu aliwaonaje viongozi wa kidini waliodai kuwa waadilifu lakini walimvunjia Mungu heshima? “Yesu akawaambia: ‘Kama Mungu angekuwa ndiye Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu nami nipo hapa. Wala sikuja kwa uamuzi wangu mwenyewe hata kidogo, lakini Huyo alinituma. . . . Ninyi mmetoka kwa baba yenu Ibilisi, nanyi mnataka kufanya tamaa za baba yenu. Huyo alikuwa muuaji alipoanza, naye hakusimama imara katika kweli, kwa sababu kweli haimo ndani yake. Anaposema uwongo, yeye husema kulingana na mwelekeo wake mwenyewe, kwa sababu yeye ni mwongo na ndiye baba ya uwongo. Kwa sababu mimi, kwa upande mwingine, ninawaambia ile kweli, hamniamini. . . . Ndiyo sababu hamsikilizi, kwa sababu hamtoki kwa Mungu.’”—Yoh. 8:42-47.
Je, ingekuwa ni kuonyesha ushikamanifu kwa Mungu na kwa viwango vyake vya uadilifu ikiwa watumishi wake wangeshirikiana kidini na wale ambao hutenda yale ambayo Mungu anashutumu au wanaoachilia mambo hayo yaendelee kufanywa? “Mwache kuchangamana katika ushirika pamoja na mtu yeyote anayeitwa ndugu ambaye ni mwasherati au mtu mwenye pupa au mwabudu-sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi, hata msile chakula pamoja na mtu wa namna hiyo. . . . Wala waasherati, wala waabudu-sanamu, wala wazinzi, wala wanaume wanaowekwa kwa ajili ya makusudi yasiyo ya asili, wala wanaume wanaolala na wanaume, wala wezi, wala watu wenye pupa, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi hawataurithi ufalme wa Mungu.” (1 Kor. 5:11; 6:9, 10) “Yeyote anayetaka kuwa rafiki ya ulimwengu anajifanya kuwa adui ya Mungu.” (Yak. 4:4) “Enyi mnaompenda Yehova, chukieni yaliyo mabaya. Yeye anazilinda nafsi za washikamanifu wake.”—Zab. 97:10.
2 Kor. 6:14-17: “Msifungwe nira isivyo sawa pamoja na wasio waamini. Kwa maana kuna ushirika gani kati ya uadilifu na uasi-sheria? Au nuru ina ushirika gani na giza? Na zaidi, kuna upatano gani kati ya Kristo na Beliali? Au mtu mwaminifu ana fungu gani na asiye mwamini? Na hekalu la Mungu lina upatano gani na sanamu? . . . ‘“Kwa hiyo tokeni katikati yao, na mjitenge,” asema Yehova, “na mwache kugusa kitu kilicho najisi”’; ‘“nami nitawakaribisha ndani.”’”
Ufu. 18:4, 5: “Nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema: ‘Tokeni kwake, watu wangu, ikiwa hamtaki kushiriki pamoja naye dhambi zake, na ikiwa hamtaki kupokea sehemu ya mapigo yake. Kwa maana dhambi zake zimekusanyika pamoja mpaka mbinguni, naye Mungu amekumbuka matendo yake yasiyo ya haki.’” (Kwa maelezo zaidi, ona kichwa, “Babiloni Mkubwa.”)
Je, ni lazima kuwa mshiriki wa dini iliyopangwa kitengenezo?
Mashirika mengi ya kidini yamezaa matunda mabaya. Ubaya si kwamba vikundi hivyo vimepangwa kitengenezo. Lakini vingi vimeendeleza namna ya ibada inayotegemea mafundisho ya uwongo na kwa ujumla vinafuata desturi tu badala ya kutoa mwongozo wa kweli wa kiroho; vimetumiwa vibaya ili kutawala maisha ya watu kwa ajili ya makusudi ya kibinafsi; vimehangaikia mno ukusanyaji wa pesa na nyumba
-