Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kifo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • ‘Mtu hufa wakati wake unapofika’

      Unaweza kujibu: ‘Watu wengi wana maoni kama yako. Je, unajua kwamba Wagiriki wengi wa kale walikuwa na maoni hayohayo? Waliamini kwamba kulikuwa na miungu mitatu ya kike iliyoamua muda ambao kila mwanadamu angeishi. Lakini Biblia ina maoni tofauti kabisa kuhusu maisha.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘(Soma Mhubiri 9:11.) Mfano: Jiwe linaweza kuvunjika kutoka kwenye nyumba na kumwangukia mpita-njia. Je, Mungu ndiye aliyesababisha jambo hilo? Ikiwa hivyo ndivyo ilivyo, je, ni haki kumshtaki mwenye nyumba kwa sababu ya uzembe? . . . Kama Biblia inavyosema, kwa mpita-njia huyo, tukio hilo halikuwa limepangwa mapema wala halikuwa limetarajiwa, bali alikuwa papo hapo wakati jiwe hilo lilipoanguka.’ (2) ‘Biblia inatuambia kwamba tukiepuka mwenendo mbaya, tutaulinda uhai wetu. (Met. 16:17) Ikiwa wewe ni mzazi, nina hakika kwamba unatumia kanuni hiyohiyo unapowafundisha watoto wako. Unawaonya juu ya mambo ambayo yanaweza kusababisha kifo. Yehova anawafanyia wanadamu wote jambo hilohilo leo.’ (3) ‘Yehova anajua yatakayotokea wakati ujao. Kupitia Biblia yeye anatuambia jinsi tunavyoweza kufurahia maisha marefu zaidi kuliko yale ya watu wanaopuuza maneno yake. (Yoh. 17:3; Met. 12:28)’ (Ona pia kichwa, “Majaliwa.”)

  • Kitia-Moyo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kitia-Moyo

      Maana: Jambo linalomtia mtu moyo au kumpa tumaini. Kila mtu anahitaji kutiwa moyo. Mtu anaweza kumtia mwingine moyo kwa kumsaidia au kwa kumshukuru. Mara nyingi huhusisha kumsaidia mtu aone jinsi ya kukabiliana na hali ngumu au kuzungumzia sababu za kuwa na hakika katika wakati ujao ulio bora. Biblia ina msingi bora zaidi wa kitia-moyo hicho, na maandiko yaliyonukuliwa hapa yanaweza kukusaidia unapowatia moyo watu wanaokabili matatizo mbalimbali. Wakati mwingine, mtu anaweza kumsaidia sana mwingine kwa kumsikitikia tu.—Rom. 12:15.

      Kwa wale wanaoteseka kwa sababu ya UGONJWA—

      Ufu. 21:4, 5: “‘[Mungu] atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.’ Na Yule aliyeketi juu ya kiti cha ufalme akasema: ‘Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.’ Pia, anasema: ‘Andika, kwa sababu maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.’”

      Mt. 9:35: “Yesu akaondoka ili kutembelea majiji na vijiji vyote, akifundisha . . . na kuhubiri habari njema ya ufalme na kuponya kila namna ya magonjwa na kila namna ya udhaifu.” (Kwa kuhusianisha uponyaji huo na mahubiri yake juu ya Ufalme, Yesu alionyesha mambo mazuri atakayowafanyia wanadamu wakati wa Utawala wake wa Miaka Elfu.)

      2 Kor. 4:13, 16: “Sisi pia tunaonyesha imani . . . Kwa hiyo hatufi moyo, lakini hata ikiwa mtu tuliye kwa nje [mwili wetu] anachakaa, hakika mtu tuliye kwa ndani anafanywa upya [au tunapewa nguvu mpya] siku baada ya siku.” (Huenda tukawa tunadhoofika kimwili, lakini kiroho tunafanywa upya tunapoendelea kujilisha ahadi nzuri za Mungu.)

      Ona pia Luka 7:20-23.

      Kwa wale ambao wapendwa wao WAMEKUFA—

      Isa. 25:8, 9: “Yeye kwa kweli atameza kifo milele, na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote. . . . Na katika siku hiyo hakika mtu atasema: ‘Tazama! Huyu ndiye Mungu wetu. Tumemtumaini yeye, naye atatuokoa. Huyu ndiye Yehova. Tumemtumaini yeye. Na tuwe na shangwe na kushangilia katika wokovu wake.’”

      Yoh. 5:28, 29: “Msistaajabie jambo hili, kwa sababu saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake na kutoka, wale waliotenda mambo mema kwenye ufufuo wa uzima, wale waliokuwa na zoea la kutenda mambo maovu kwenye ufufuo wa hukumu.”

      Yoh. 11:25, 26: “Yesu akamwambia: ‘Mimi ndiye ufufuo na uzima. Yule anayeniamini, hata akifa, atarudi kwenye uzima; na kila mtu aliye hai na ananiamini hatakufa kamwe. Je, unaamini hilo?’”

      Zab. 146:5, 9: “Mwenye furaha ni yule . . . ambaye tumaini lake liko katika Yehova Mungu wake. . . . Humtuliza mvulana asiye na baba na mjane.” (Sasa hivi Mungu anawahangaikia kwa upendo wale waliofiwa.)

      Ona pia Luka 7:11-16; 8:49-56.

      Kwa wale WANAOTESWA kwa sababu wanafanya mapenzi ya Mungu—

      Zab. 27:10: “Hata ikiwa baba yangu na mama yangu wangeniacha, Yehova mwenyewe angenichukua.”

      1 Pet. 4:16: “Akiteseka kwa sababu yeye ni Mkristo, asione aibu, bali na aendelee kumtukuza Mungu katika jina hili.”

      Met. 27:11: “Uwe na hekima, mwanangu, na kuufanya moyo wangu ushangilie, ili nipate kumjibu anayenidhihaki.” (Tunapokuwa waaminifu, sisi tunatoa jibu kwa shtaka la uwongo la Shetani kwamba hakuna mtu yeyote anayeteseka ambaye anaweza kuendelea kumtumikia Mungu.)

      Mt. 5:10-12: “Wenye furaha ni wale ambao wameteswa kwa ajili ya uadilifu, kwa kuwa ufalme wa mbinguni ni wao. Wenye furaha ni ninyi wakati watu wanapowashutumu na kuwatesa na kusema kwa uwongo kila namna ya jambo baya juu yenu kwa ajili yangu. Shangilieni na kuruka kwa shangwe, kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana hivyo ndivyo walivyowatesa manabii waliokuwa kabla yenu.”

      Mdo. 5:41, 42: “Kwa hiyo, [mitume] wakatoka mbele ya Sanhedrini, wakishangilia kwa sababu walikuwa wamehesabiwa kuwa wenye kustahili kuvunjiwa heshima kwa ajili ya jina lake. Na kila siku katika hekalu na nyumba kwa nyumba wakaendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema juu ya Kristo, Yesu.”

      Flp. 1:27-29: “Ila tu jiendesheni kwa namna inayostahili habari njema juu ya Kristo . . . nanyi msiwaogope hata kidogo wapinzani wenu. Jambo hili ni uthibitisho wa uharibifu kwao, lakini wa wokovu kwenu; na ishara hii inatokana na Mungu, kwa sababu ninyi mlipewa pendeleo kwa ajili ya Kristo, si muwe tu na imani katika yeye, bali pia mteseke kwa ajili yake.”

      Kwa wale waliovunjika moyo kwa sababu ya UKOSEFU WA HAKI—

      Zab. 37:10, 11: “Bado muda kidogo tu, na mtu mwovu hatakuwako tena; nawe hakika utapaangalia mahali pake, naye hatakuwapo. Bali wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.”

      Isa. 9:6, 7: “Kuna mtoto ambaye amezaliwa kwetu, kuna mwana ambaye tumepewa; na utawala wa ukuu utakuwa juu ya bega lake. Naye ataitwa jina Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mkuu wa Amani. Hakutakuwa na mwisho kwa habari ya wingi wa huo utawala wa kifalme na kwa amani, juu ya kiti cha ufalme cha Daudi na juu ya ufalme wake ili kuufanya imara na kuutegemeza kwa njia ya haki na kwa njia ya uadilifu, kuanzia sasa na kuendelea mpaka wakati usio na kipimo. Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.”

      Dan. 2:44: “Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo.”

      Ona pia Isaya 32:1, 2; 2 Petro 3:13.

      Kwa wale wanaokazwa sana na MATATIZO YA KIUCHUMI—

      Isa. 65:21, 22: “Watajenga nyumba na kukaa ndani yake; na hakika wao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. Hawatajenga na mtu mwingine akae ndani yake; hawatapanda na mtu mwingine ale. . . . Watu wangu waliochaguliwa wataitumia kazi ya mikono yao wenyewe kikamilifu.”

      Zab. 72:8, 16: “Naye [Mfalme Masihi] atakuwa na raia kutoka bahari mpaka bahari na kutoka ule Mto mpaka miisho ya dunia. Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani; juu ya milima kutakuwa na mafuriko.”

      Mt. 6:33: “Basi, endeleeni kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake, nanyi mtaongezewa hivi vitu [mahitaji ya kimwili ya maisha] vingine vyote.”

      Rom. 8:35, 38, 39: “Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je, ni dhiki au taabu au mateso au njaa au uchi au hatari au upanga? Kwa maana nimesadiki kwamba wala kifo wala uzima wala malaika wala serikali wala mambo yaliyopo sasa wala mambo yatakayokuja wala nguvu wala kimo wala kina wala uumbaji mwingine wowote havitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.”

      Ona pia Waebrania 13:5, 6.

      Kwa watu ambao wamevunjika moyo kwa sababu ya MAKOSA yao wenyewe—

      Zab. 34:18: “Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo; naye huwaokoa wale waliopondwa roho.”

      Zab. 103:13, 14: “Kama vile baba anavyowaonyesha wanawe rehema, ndivyo ambavyo Yehova amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa. Kwa maana yeye mwenyewe analijua vema umbo letu, akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.”

      Neh. 9:17: “Wewe ni Mungu wa matendo ya kusamehe, mwenye neema na rehema, si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fadhili zenye upendo.”

      2 Pet. 3:9, 15: “Yehova hakawii kuhusiana na ahadi yake, kama watu fulani wanavyoona kukawia, bali yeye ni mwenye subira kwenu kwa sababu hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba. Zaidi ya hayo, ioneni subira ya Bwana wetu kuwa wokovu.”

  • Kunyakuliwa
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kunyakuliwa

      Maana: Imani ya kwamba Wakristo waaminifu watachukuliwa kimwili kutoka duniani, waondolewe ghafula kutoka katika ulimwengu, ili waende kuungana pamoja na Bwana “hewani.” Watu fulani huamini kwamba andiko la 1 Wathesalonike 4:17 linazungumzia “kunyakuliwa” huko.

      Mtume Paulo aliposema kwamba Wakristo ‘watanyakuliwa’ wakawe pamoja na Bwana, alikuwa akizungumza juu ya nini?

      1 The. 4:13-18, UV: “Hatutaki msijue habari zao waliolala mauti [“wale wanaokufa,” NAJ], msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini. Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye. Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. Basi, farijianeni kwa maneno hayo.” (Inaonekana kwamba washiriki fulani wa kutaniko

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki