‘Wao Walikuwa Wakicheka’
Mwanamume mmoja anayetumikia katika jeshi huko Hungary asema kwamba si muda mrefu uliopita watu walikuwa wakicheka wale waliokuwa wakisema juu ya Biblia. Lakini nyakati zimebadilika. Hivi karibuni askari-jeshi huyo aliandikia ofisi ya Watch Tower Society katika Budapest, akisema hivi:
“Siku chache zilizopita, nilisoma kichapo chenu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Mtu fulani alikuwa ameniazimia kitabu hicho mpaka nilipomaliza kukisoma. Yale ambayo yameandikwa katika kitabu hicho yamenigusa sana moyoni na kunifanya nifikiri.” Askari-jeshi huyo alitaka Biblia na habari zaidi. Itikio la jinsi hiyo si jambo lisilo la kawaida tena katika Ulaya Mashariki.
Barua nyingine iliyopokewa katika ofisi ya Budapest yasema hivi: “Nimekisoma kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Kitabu hicho kimenivutia sana, nami nawaandikia nyinyi kuomba Shahidi anitembelee nyumbani kwangu ili niweze kuwa na funzo la Biblia la kawaida.”
Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani ni kitabu kinachotoa tumaini kwa kukuelekeza kwenye majibu ya Biblia. Kimekuwa na uvutano mkubwa katika kubadili maisha mengi. Ikiwa ungependa kupokea nakala, tafadhali jaza na kupeleka hati-anwani hii yenye kuandama.
Ningependa kupokea kile kitabu cha kurasa 256 chenye jalada gumu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani.
[Picha katika ukurasa wa 32]
Akiwa na sababu nzuri, mzazi ataruhusu mtoto wake mpendwa apate upasuaji wenye maumivu. Vilevile Mungu ana sababu nzuri za kuruhusu kwa muda wanadamu wateseke