Wimbo 182
“Zeri Katika Gileadi”
1. Kuna zeri Gileadi;
Biblia husema.
Huifariji mioyo
Hutoa huzuni.
Hutufariji tukiwa
Tunajaribiwa,
Au mupenzi kulala
’Singizi wa kifo.
2. Kumbuka ‘Mungu ni pendo,’
Hekima na kweli.
Chochote anachotoa
Kinakufaidi.
Mwombe Mungu wa faraja
Pasipo kukoma,
Ya moyoni; sema yote
Ya kukusumbua.
3. Ukumbuke ya zamani,
Yaliyotendeka,
Yaliandikwa kusudi
Tupate faraja.
Kubali musaada wa
Waliokomaa,
Na watakusaidia
Ukavumilie.
4. Umefikiri wengine,
Wanahuzunika?
Na ukamilifu wao
Unajaribiwa?
Watafute, wafariji,
Changamusha moyo.
Hivyo utajua nguvu
Za dawa ya zeri.