Mkatoliki Akifurahia
Mmoja wa Mashahidi wa Yehova akiwa katika eneo moja la mashambani la Virginia, U.S.A., alitobokewa na mpira wa gurudumu la gari lake. Nyumba moja ilikuwa karibu, na dada huyo akapiga hodi mlangoni. Bibi mwenye nyumba alimruhusu aingie apigie simu wenye kutoa utumishi wa barabarani. Baadaye Shahidi yule alimpelekea bibi yule barua ya kusema asante, akaambatanisha na barua hiyo nakala-zawadi ya kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Linalofuata, kwa sehemu, ndilo jibu alilopokea:
“Mimi nitakueleza mambo bila kukuficha hata kidogo. Mimi ni Mkatoliki. Na wakati wo wote mtu ye yote anapokuja mlangoni kwangu akiwa na Mnara wa Mlinzi au trakti nyingine zo zote, mimi najaribu kuzikataa. Nikilazimishwa nizichukue, nazitupa katika pipa ya takataka. Ukatoliki umeingizwa ndani yangu sana tangu nilipokuwa mtoto mdogo.
“Ijapokuwa hivyo, nilivutiwa na kitabu chenu kwa sababu kilikuwa na neno ‘Paradiso’ ndani ya kichwa chacho na kwa sababu maneno yacho yalifanya usomaji uwe wazi na rahisi. Maulizo yaliyo katika sehemu za chini za kurasa hizo yalinitia moyo kusoma, na picha zilinivutia. Nilipenda hasa ukurasa 11 kwa sababu mimi ninajaribu kutengeneza paradiso kama hiyo hapa, ikiwa ni ya ndege na wanyama. Mimi nina paa, sungura, kindi-milia, kindi wa kawaida, bata-mizinga mwitu na ndege wa aina zote. . . .
“Kweli wewe ulitimiza jambo kubwa sana kwa kumfanya Mkatoliki asome kitabu cha dini nyingine. Wapi! mimi nina shaka kama nitakuja kugeuka kamwe nifuate dini nyingine. Lakini nilikisoma kitabu, na mume wangu sasa anakisoma. Kwa mara nyingine, asante!”
Kichapo hiki kizuri sana kina kurasa 256, na ukubwa wacho ni sawa na gazeti hili, nacho kimejawa na picha zaidi ya 150, nyingi zazo zikiwa katika rangi ya kupendeza sana. Utupelekee Kshs. 40 (Tshs. 110; RWF 250) tu. Au ili upokee chenye ukubwa uliopunguzwa, peleka Kshs. 20.00 (Tshs. 55.00)
Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, kile kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Onyesha kwa kutia alama katika visanduku unataka chapa ile kubwa kwa Kshs. 40 (Tshs. 110) [ ] au ile ndogo kwa Kshs. 20.00 (Tshs. 55.00) [ ] na utupelekee pesa zinazolingana na kile unachotaka.