Ilikuwa Lazima Ajue
Msichana wa miaka 15 kutoka Mobile, Alabama, anaandika hivi: “Mlipotokeza kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtu U Karibu! mimi nilijua kwamba baada muda fulani ningekisoma.
“Usiku mmoja nilipokuwa nikikosa usingizi, nilichukua kitabu hicho nikazitazama picha tu. Katika kurasa 75, 78, na 86, nilipata picha zilizonivutia sana. Sikujua zilimaanisha nini, na ilikuwa lazima nijue. Nisingeweza kupata mwanzo mzuri sana kwa kuanza katikati kwa sababu nisingeelewa kitu nikifanya hivyo. Kwa hiyo usiku huo huo nilisoma sura ya kwanza.
“Usiku uliofuata nilisoma sura iliyofuata nikawa sitaki kamwe kukiweka chini. Kwa hiyo nikaendelea na kuisoma ile iliyofuata pia.
“Hiki ni kimoja cha vitabu vya kusisimua zaidi ambavyo nimepata kusoma! Sasa mimi nina zoea la ukawaida la kusoma angalau sura moja kila usiku. Nyakati fulani nimekaa macho mpaka saa saba ya usiku nikisoma tu! . . . Naona ingekuwa vizuri vijana wote wakisoma kitabu hiki.”
Sisi tunahisi kwamba wewe utasisimuliwa na mambo utakayojifunza katika Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Kitabu hiki chenye jalada gumu kina ukubwa unaolingana na ukurasa wa gazeti hili. Kinatoa ufikirio wa mstari-kwa-mstari wa kitabu kizima cha Ufunuo, kikiandaa elezo lenye kueleweka wazi juu ya njozi na vifananisho vyao vingi. Peleka ombi leo ili ukipate kitabu hicho. Ni Kshs. 50/= tu, kikiwa kimelipiwa malipo ya posta.
Tafadhali mnipelekee kile kitabu chenye kurasa 320, Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Mimi ninawapelekea Kshs. 50/=.
Pokea ensaiklopedia hii ya mabuku mawili iliyo na thamani kubwa kwa kujaza hati yenye anwani iliyoambatanishwa na uipeleke pamoja na Kshs. 225/= (Tshs. 1,125/=; RWF 1,350).