Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuteseka
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • juu ya yaliyo mabaya; wanazungumza juu ya upunjaji kwa majivuno. Tazama! Hao ndio waovu waliostarehe mpaka wakati usio na kipimo. Wameongeza mali yao.”—Zab. 73:3, 5, 8, 12.

      Siku ya Mungu ya kutoza hesabu itafika. Wakati huo atawaadhibu waovu, na kuwaharibu milele. Andiko la Methali 2:21, 22 linasema hivi: “Wanyoofu ndio watakaokaa duniani, na wasio na lawama ndio watakaobaki ndani yake. Nao waovu, watakatiliwa mbali kutoka duniani; nao wenye hila, watang’olewa kutoka ndani yake.” Hapo ndipo wanyoofu, ambao wengi wao wameteseka, watakapopata afya kamilifu na kufurahia mazao mengi ya dunia.

      Mtu Akisema—

      ‘Kwa nini Mungu anaruhusu kuteseka?’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Hilo ni jambo linalotuhangaisha sana sisi sote. Hebu nikuulize, Kwa nini umeuliza swali hilo leo?’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘(Tumia habari katika ukurasa wa 124-128.)’ (2) ‘(Tumia maandiko mengine yanayoonyesha kwamba hali fulani hususa ambayo imemfanya mtu huyo binafsi ateseke itaondolewa.)’

      Au unaweza kusema: (ikiwa wanahangaishwa na ukosefu wa haki ulimwenguni): ‘Biblia inaonyesha kwa nini hali hizi zipo leo. (Mhu. 4:1; 8:9) Je, unajua kwamba inaonyesha pia mambo ambayo Mungu atafanya ili atuletee kitulizo? (Zab. 72:12, 14; Dan. 2:44)’

      Pia unaweza kusema: ‘Inaonekana wewe unamwamini Mungu. Je, unaamini kwamba Mungu ni upendo? . . . Je, unaamini kwamba yeye ni mwenye hekima na kwamba yeye ni mweza-yote? . . . Basi ni lazima awe ana sababu fulani nzuri za kuruhusu kuteseka. Biblia inaonyesha sababu hizo. (Ona ukurasa wa 124-128.)’

  • Kutoa Mimba
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kutoa Mimba

      Maana: Kutoa mimba ni kuondoa tumboni kiini-tete au kitoto ambacho kwa kawaida hakiwezi kuishi nje ya tumbo la uzazi. Huenda mimba ikatoka yenyewe kwa sababu ya kutokamilika kwa kibinadamu au kwa sababu ya msiba. Kutoa mimba kimakusudi ili kuepuka tu kuzaa mtoto asiyetakiwa ni sawa na kumwua binadamu kimakusudi.

      Kumfikiria yule aliye Chanzo cha uhai wa kibinadamu kunapaswa kutufanya tuwe na maoni gani juu ya jambo hili?

      Mdo. 17:28: “Kupitia kwake [Mungu] tuna uhai na tunaenda na kuwako.”

      Zab. 36:9: “Kwako wewe [Yehova Mungu] iko chemchemi ya uzima.”

      Rom. 14:12: “Kila mmoja wetu atatoa hesabu kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe.”

      Je, Yehova anauona uhai wa mtoto kuwa wenye thamani hata wakati wa hatua za kwanza za ukuzi baada ya mimba kutungwa?

      Zab. 139:13-16: “Wewe [Yehova] uliniweka nikiwa nimekingwa katika tumbo la mama yangu. . . . Macho yako yalikiona kiini-tete changu, na katika kitabu chako sehemu zake zote zilikuwa zimeandikwa.”

      Je, Mungu amewahi kusema kwamba mtu atatozwa hesabu kwa kumdhuru mtoto ambaye hajazaliwa bado?

      Kut. 21:22, 23: “Ikiwa watu watapambana nao kwa kweli wamuumize sana mwanamke mwenye mimba nao watoto wake watoke lakini kifo kisitokee, atadaiwa alipie hasara kulingana na kile ambacho mume wa mwanamke huyo atamdai; naye atakitoa kupitia kwa waamuzi. Lakini kifo kikitokea, basi utatoa nafsi kwa nafsi.” (Tafsiri fulani zinafanya ionekane kana kwamba katika sheria hii kwa Israeli jambo la maana hapa lilikuwa kile kilichompata mama, wala si kitoto. Hata hivyo, maandishi ya kwanza ya Kiebrania yanarejezea msiba ambao ungeweza kusababisha kifo cha mama au mtoto.)

      Kumwua binadamu kimakusudi bila ruhusa ya Mungu ni jambo zito kadiri gani?

      Mwa. 9:6: “Yeyote anayemwaga damu ya mwanadamu, damu yake nayo itamwagwa na mwanadamu, kwa maana kwa mfano wa Mungu alimfanya mwanadamu.”

      1 Yoh. 3:15: “Hakuna muuaji aliye na uzima wa milele ukikaa ndani yake.”

      Kut. 20:13: “Usiue.”

      Je, maoni ya daktari ya kwamba kuruhusu mimba ikue kutadhuru afya ya mama ni sababu inayofaa ya kutoa mimba?

      Wakati mwingine madaktari hukosea. Je, ingefaa mtu auawe kwa sababu huenda mtu huyo akamdhuru mwenzake? Ikiwa wakati wa kuzaa kuna uhitaji wa kuchagua kati ya uhai wa mama na ule wa mtoto, ni juu ya watu wanaohusika kufanya uamuzi huo. Hata hivyo, maendeleo ya kitiba katika nchi nyingi yamepunguza sana uwezekano wa hali hizo kutokea.

      Mtu Akisema—

      ‘Lakini nina haki ya kuamua mambo yanayohusu mwili wangu mwenyewe.’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Ninaelewa maoni yako. Siku hizi, watu wengine huvunja haki zetu mara nyingi; wengi hata hawajali yanayowapata watu wengine. Lakini Biblia inatoa miongozo inayoweza kutulinda. Hata hivyo, ili tufaidike, ni lazima pia tukubali wajibu.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Akina mama wengi wameachwa na baba za watoto wao. Lakini katika nyumba ambamo mume na mke wanafuata viwango vya Biblia, mume atampenda sana mke na watoto wake na kukaa nao kwa ushikamanifu na kuwaandalia mahitaji yao. (1 Tim. 5:8; Efe. 5:28-31)’ (2) ‘Ili sisi binafsi tupokee aina hiyo ya upendo na heshima, tunapaswa pia kutumia viwango vya Biblia kuhusu maoni yetu kuwaelekea washiriki wa familia yetu. Biblia inasema tunapaswa kuwa na maoni gani kuwahusu watoto tunaowazaa? (Zab. 127:3; linganisha na Isaya 49:15.)’

  • Kutounga Mkono Upande Wowote
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Kutounga Mkono Upande Wowote

      Maana: Msimamo wa wale wasiounga mkono upande wowote wala kusaidia upande wowote kati ya pande mbili au zaidi zinazoshindana. Ni wazi kwamba tangu zamani na hata leo, katika

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki