Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Nguvu Ipitayo Iliyo ya Kawaida”
    Mnara wa Mlinzi—1992 | Februari 1
    • “Nguvu Ipitayo Iliyo ya Kawaida”

      MKRISTO aweza kuvumilia mateso ya kadiri gani? Leo, Wakristo ulimwenguni pote wanakabiliana na umaskini, farakano za familia, shtuo la kihisia-moyo, ugonjwa, vita, na minyanyaso. Je! ni jambo lifaalo kuwatazamia washikilie uaminifu wao wa kimaadili yajapokuwa hayo yote? Mtume Paulo alisema ingewezekana. Aliandika: “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.”—Wafilipi 4:13.

      Historia imeonyesha kwamba nguvu kutoka kwa Yehova inatosha kwelikweli kwa mambo yote. Kwa mfano, wakati wa utawala wa Nazi katika Ujerumani, Mashahidi wa Yehova walipatwa na minyanyaso mikali. Je! walivumilia? Kitabu Les Bibelforscher et le nazisme (Wanafunzi wa Biblia na Unazi) chasema: “Yajapokuwa mapigo yote yale, vitisho, marufuku, ujapokuwa udhilifu wa hadharani, vifungo na vizuizi katika kambi za mateso, Wanafunzi wa Biblia [Mashahidi wa Yehova] hawakujiruhusu ‘wafunzwe tena.’”

      Kwenye kambi za mateso, Mashahidi wa Yehova walitambulishwa kwa vialama vya zambarau kwenye mikono ya mavazi yao na waliwekwa kando kwa ajili ya ukatili wa kipekee. Je! hilo liliwavunja? Mwanasaikolojia Bruno Bettelheim aliandika kwamba “si kwamba tu walionyesha viwango visivyo vya kawaida vya kibinadamu na adili za mwenendo, bali walionekana kana kwamba wamekinzwa na hali ile ile ya kambi iliyoharibu upesi watu waliofikiriwa kuwa wenye usawaziko wa kiakili na marafiki wangu wa kisaikoanali na mimi mwenyewe.”

      Ndiyo, walikuwa na ‘nguvu kwa mambo yote.’ Kwa nini? kwa sababu walimtegemea Yehova. Paulo alisema: “Sisi tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili nguvu ipitayo iliyo ya kawaida ipate kuwa ya Mungu wala si ile ya kutoka kwetu wenyewe.” (2 Wakorintho 4:7 NW) Ikiwa utapatwa na hali yenye kujaribu, mtegemee Yehova kwa uhakika kwa ajili ya msaada. Kwa kuimarishwa na nguvu ipitayo iliyo ya kawaida anayotoa, utaweza kuvumilia.—Luka 11:13.

  • Je! Wewe Ungekaribisha Ziara?
    Mnara wa Mlinzi—1992 | Februari 1
    • Je! Wewe Ungekaribisha Ziara?

      Hata katika ulimwengu huu wenye matatizo, wewe waweza kupata furaha kutokana na maarifa sahihi ya Biblia kuhusu Mungu, Ufalme wake, na kusudi lake zuri ajabu kwa ainabinadamu. Ikiwa ungependa habari zaidi au kutembelewa na mtu fulani ili aongoze funzo la Biblia nyumbani na wewe bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki