-
Usichoke Kutenda Yaliyo MemaMnara wa Mlinzi—1988 | Julai 15
-
-
Usichoke Kutenda Yaliyo Mema
“Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.”—WAGALATIA 6:9.
1. Yesu aliwapa wafuasi wake utume gani?
NI UTENDAJI mzuri jinsi gani ambao Wakristo wanafanya kama sehemu ya ibada yao! Umefungamanishwa katika amri iliyo waziwazi: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza . . . kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi. Na, tazama! mimi nipo pamoja na ninyi siku zote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 28:19, 20, NW) Yesu Kristo mwenyewe ndiye aliyewapa wanafunzi wake utume wa kufanya kazi hiyo ya kufundisha ya ulimwenguni pote.
2. (a) Kwa sababu gani tunaweza kusema kwamba kazi ya kufanya wanafunzi ilikuwa ya maana na ni nzuri? (b) Kazi ya kufanya wanafunzi inatumikia kusudi gani?
2 Kwa kuwa utume wa kufanya wanafunzi ndio uliokuwa mojapo ya taarifa za mwisho ambazo Yesu aliwaambia wanafunzi wake wa kwanza kabla ya kupaa mbinguni, je! haukuwa mgawo ulio wa maana sana? Ndiyo, kwa sababu kuutimiza kungeokoa uhai wetu. (1 Timotheo 4:16) Hilo linaufanya uwe kazi nzuri. Unaandaa elimu nzuri ya Biblia kwa wale wanaotii ujumbe wa Ufalme, na kazi ya kuhubiri inawaonya wale wasioitikia. (Luka 10:10, 11) Kwa sababu hii, kufanya kwao kazi hiyo kunawatambulisha Wakristo wa kweli kama vile kuitikia kwao mafundisho mengineyo yote ya Yesu.—Yohana 8:31.
3. (a) Wanafunzi wa Yesu waliitikiaje kielelezo na amri yake mwenyewe? (b) Yesu alikuza mwelekeo gani katika wanafunzi wake?
3 Akiwa Mwalimu Mkuu, Yesu aliwawekea wafuasi wake kielelezo kizuri sana. Alifundisha waziwazi na kufanya wanafunzi kwa “kuhubiri habari njema ya ufalme.” (Mathayo 9:35) Kwa kumwiga yeye, wafuasi wapya wenyewe wakawa wafanya-wanafunzi, kwa kuwa mwanafunzi wa kweli ni “mmoja anayekubali na kusaidia katika kueneza mafundisho ya mwingine.” Mwanzoni, kazi yao ya kufanya wanafunzi iliwekewa mpaka kwa Wayahudi na waongofu. Hata hivyo, ijapokuwa mjibizo mbaya wo wote katika kazi hiyo, je! wafuasi wa Yesu walitimiza amri yake ya “kwenda bila kukoma” ‘kutoacha’? Ndiyo, walienda kwa “kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli” mpaka wakati Wamataifa wa kwanza walipokuwa waitikadi katika 36 W.K. (Mathayo 10:5, 6; Matendo 5:42) Ilisemwa kwamba wanafunzi ‘waliijaza Yerusalemu mafundisho yao.’ (Matendo 5:28) Hawakuchoka na kazi yao nzuri. Badala yake, waliitimiza kwa imani.
“Lile Shamba Ni Ulimwengu”
4. Wafuasi wa Yesu walifuatia mgawo wao ulioongezeka wakiwa na mwelekeo gani?
4 Yesu alionyesha kwamba shamba lingetia ndani “watu wa mataifa yote.” (Mathayo 28:19 NW) Katika mfano wa maneno juu ya kupanda mbegu ya UfaIme, yeye alikuwa amesema: “Lile shamba ni ulimwengu.” (Mathayo 13:38, NW) Hivyo, Wakristo wangekuwa “mashahidi” wake wa Ufalme kila mahali. Tena wangeenda bila kukoma, wakati huu “kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” (Matendo 1:8, NW) Mtume Paulo ‘alisongwa sana na lile neno,’ na tunaweza kuwa na uhakika wa kwamba Wakristo wengine walisongwa pia.—Matendo 18:5.
5. Yesu alionyeshaje kwamba alitazamia wanafunzi wake wasongwe sana na kazi ya kutoa ushuhuda mpaka mwisho wa mfumo huu wa mambo?
5 Yesu alitazamia utendaji wa kutoa ushuhuda uwasonge Wakristo mpaka umalizio wa mfumo wa mambo uliopo. Hilo linaonyeshwa katika yale aliyotabiri juu ya huduma ya Kikristo na eneo ambayo ingeenea. Yesu alisema: “Na habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.”—Mathayo 24:14, NW.
6. Kazi ya kuhubiri Ufalme itafanywa kwa muda gani, na jambo hili linapasa kuathirije mwelekeo wetu kuielekea?
6 Yesu alipotoa amri ya kushiriki katika utendaji wa kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi duniani pote, alijua kwamba kazi nzuri hiyo ingefikia upeo siku moja, kama ilivyofikia upeo katika shamba la Kiyahudi. Lakini ingetimiza kusudi layo. “Ndipo,” kama alivyosema, “mwisho utakuja.” Hivyo, kwa utumainifu na kwa shangwe Mashahidi wa Yehova wanaendelea katika kazi waliyogawiwa mpaka mwisho uje. Jambo hilo linawasaidia waendelee katika kazi katika siku yetu mpaka imalizike.
Jinsi ya Kufanya Kazi Hiyo
7. Ni kichwa gani kilichotia alama huduma ya Yesu na ile ya wanafunzi wake?
7 Yesu aliwafundisha wanafunzi wake wa kwanza jinsi ya kufanya huduma yao ya waziwazi. Waliitikia agizo lake “Nendeni” kwa bidii. Alipokuwa akiwazoeza kwa ajili ya kazi yao ya kutoa ushuhuda, Yesu alisema: “Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.” (Mathayo 10:7) Hilo liliupa ujumbe wao kichwa kile kile cha Ufalme ambacho kilikuwa kimetia alama huduma yake. Ingekuwa habari njema kwa watu wenye moyo wa kufuata haki. Mara wanafunzi wa Yesu walipoanza kazi yao, je! yeye aliacha? La, kwa kweli, “Yesu alipokwisha kuwaagiza wanafunzi wake kumi na wawili, alitoka huko kwenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.”—Mathayo 11:1.
8. (a) Ni wapi na jinsi gani watangazaji wa Ufalme wangeenda? (b) Kwa nini inafaa kupeleka habari njema kwa nyumba ya mtu? (c) Kuna faida gani kumsalimu mwenye nyumba ifaavyo?
8 Ni wapi na jinsi gani watangazaji hao wa Ufalme wangeenda? Yesu aliwaambia: “Nanyi mkiingia katika nyumba isalimuni.” (Mathayo 10:12) Kwenda kwenye nyumba ya mtu tukiwa na habari njema kunaonyesha heshima kwa mwenye nyumba, kukimpa fursa ya kushughulikia ujumbe wa Ufalme katika maskani yake. Njia za kidesturi na zinazokubalika za kusalimu si ndio njia ya upole na yenye kuonyesha fikira tu ya kuanzisha mazungumzo, lakini pia salamu ya kirafiki na yenye uchangamfu inaweza kugeuza ziara isiyotazamiwa iwe yenye kukubalika. (Linganisha Mathayo 28:9; Luka 1:28.) Sauti na jibu la mtu anayepatikana mlangoni inakuambia mengi pia kuhusu mwelekeo wake. Unahitaji kujua hilo kabla ya kuendelea kwa kuwa kujua huko kunafanya iwe rahisi kurekebisha maelezo yako yalingane na mahitaji ya mwenye nyumba.—Linganisha Matendo 22:1, 2; 23:6.
9. Ni nini kinachoonyesha kwamba si wote ambao wangesikia ujumbe wa Ufalme kwa kuthamini, na mjibizo wa wale ambao hawangeonyesha kupendezwa ungekuwa nini?
9 Yesu aliwajulisha wanafunzi wake ya kwamba si watu wote katika eneo wangeitikia kwa upendeleo. Yeye alisema: “Ndani ya jiji lo lote au kijiji ambamo ninyi mnaingia, tafuteni-tafuteni ni nani humo anayestahili.” Ikiwa wote wangeikubali ujumbe wa Ufalme, hakungekuwa na sababu ya kutumia usemi “tafuteni-tafuteni.” Mjibizo wa wale ambao hawakuonyesha kupendezwa katika ujumbe huo ungekuwa nini? “Mahali po pote ambapo mtu ye yote hawakaribishi ndani wala kusikiliza maneno yenu, mnapotoka katika nyumba hiyo au jiji lile yakung’uteni mavumbi yatoke kwenye nyayo zenu,” kuondoka kwa amani na kuachia hukumu ya Yehova itokeze matokeo.—Mathayo 10:11, 14, NW.
Ile Hali Leo
10. Ni nini ambalo limesemwa juu ya utendaji wa kuhubiri Ufalme wa Mashahidi wa Yehova?
10 Kwa kukubali utume wa Kikristo kwa imani, Mashahidi wa Yehova wanaeneza dunia wakiwa na ujumbe wa Ufalme. Hivyo, A. P. Wisse, mwandikaji wa majarida katika Uholanzi, alieleza hivi: “Wao ni tofauti na watu wengine. Sehemu ya tofauti hiyo ni matokeo ya kueneza kwao evanjeli kwa bidii. Wao hawaoni Ukristo wa kweli kuwa dini yenye makathedro, yenye wanamitaa ambao kila mmoja ana mahali pake mwenyewe palipowekwa kando na ambaye dini yake haimtaki afanye zaidi ila kusikiliza tu. Wao wanaambia mambo waziwazi ye yote ambaye atasikiliza kama alivyofanya Paulo.” Kwa kweli bidii hiyo kwa ajili ya huduma imebarikiwa na Yehova Mungu.
11, 12. (a) Ni matokeo gani yamepatikana katika huduma katika miaka ya karibuni? (b) Tunapoongezeka katika hesabu, ni nini kinachotendeka kwa eneo la kuhubiri linalopatikana? (c) Ni maswali gani yanayozushwa?
11 Zaidi ya wahubiri wa Ufalme 3,000,000 sasa wanafanya kazi kwa bidii katika mabara 210. Tunaona ongezeko zuri la wanafunzi wapya—1,246,204 wamebatizwa katika muda wa miaka saba iliyopita. Baraka ya Yehova kwa jitihada yenye juhudi inaonekana wazi. (Isaya 60:8-10, 22) Kwani, angalau katika nchi na visiwa 40, kuna Shahidi mmoja kwa kila wakaaji 300 au chini, au mmoja kwa karibu jamaa 100! Waaidha, katika sehemu fulani fulani za nchi hizo kama vile Kanada na Guadeloupe, kila Shahidi anahubiria watu 45 au 50 katika eneo la kundi moja—karibu makao 15 tu au chini kwa kila mhubiri kutembelea! Mengi ya maeneo haya yanaenezwa kila mwezi. Hata katika mabara ambao kila mhubiri ana watu wengi wa kuhubiria, sehemu fulani za mashambani zinaenezwa kwa ukawaida katika kazi yetu ya kutoa ushuhuda. Katika Seoul, Jamhuri ya Korea, maeneo fulani ya jijini yanafanyiwa kazi baada ya kila siku tano! Tunapoongezeka katika hesabu, na Mashahidi zaidi na zaidi wanapochukua kazi ya painia na painia msaidizi, tutakuwa tunatembelea milango ya majirani wetu kwa ukawaida wenye kuongezeka. Je! hilo linatokeza matatizo?
12 Lazima ikubalike kwamba kuna matatizo katika sehemu fulani, kwa wote Mashahidi wa Yehova na wale tunaotembelea. Linaloongezea matatizo hayo ni ongezeko la ubaridi ulio miongoni mwa watu katika mabara mengi. Basi, tunapozidi kuongezeka katika hesabu, je! tunachoka polepole kufanya kazi yetu nzuri? Je! tunakata maneno kwamba kazi yetu takriban imalizike na kwamba tayari ‘tumetafuta-tafuta’ wote ambao wataitikia na kuwa wanafunzi? Je! wewe binafsi unachoka na labda hata unashindwa kuwatembelea watu wale wale wasioitikia? Ni jambo gani linaloweza kufanywa ili kuendeleza kiwango chetu bora cha utendaji?
Kudumisha Mwelekeo Unaofaa
13, 14. (a) Tunapaswa kuonaje hali inayotokea ya kufanyia eneo kazi mara kwa mara? (b) Kwa nini hatuzuiwi na wale ambao ‘hawaitikii’? (c) Tunawezaje kufuata kielelezo cha mitume katika kukabiliana na wale ambao wanachukizwa na ziara zetu?
13 Utatuzi unatia ndani hasa mwelekeo wetu tukiwa mashahidi wa Yehova. Jambo la kwanza, acheni tutazame upande mzuri sikuzote. Kueneza eneo mara nyingi zaidi kwa sababu ya hesabu kubwa ya wahubiri wanaohubiria idadi ya watu ni jambo ambalo kwa hakika lingetokea katika sehemu nyingi wakati kazi yetu inafikia upeo wake. Lakini je! hatujasali kwa ajili yalo? (2 Wathesalonike 3:1) Yale ambayo tunaona sasa yanapasa kutufanya tushangilie na yanapasa kutusadikisha kwamba tumo katika hatua za hatima katika kazi ya kufanya wanafunzi! Ufalme unahubiriwa, kama alivyotabiri Yesu. Na hata mahali ambapo watu ‘hawatasikiliza maneno yetu,’ wanaonywa kupitia kwa utendaji wetu wa kuhubiri Ufalme. Kumbuka, zaidi ya kufanya wanafunzi, tunatangaza habari njema “kwa ajili ya ushuhuda.”—Mathayo 10:14; 24:14, NW.
14 Zaidi ya hilo, ni jambo linalotazamiwa kwamba hesabu inayokua watakataa ujumbe wa Ufalme mwisho unapokaribia. Matabiri yanaonyesha wazi, na mambo yaliyoonwa na wote wawili Yesu na Paulo yanatuhakikishia kwamba kungekuwa na wale “wasioitikia’ na ambao mioyo yao ingekuwa “isiyopokea.” Kwa hiyo, wakati huu ni lazima tuwe waangalifu ili tusiwe wasioitikia utume wetu. Hata kwa wale wasioitikia, tunapaswa kwenda “tena na tena.” (Isaya 6:9-11, NW; Mathayo 13:14, 15; Mithali 10:21) Kweli, inahitaji ushujaa kuwaendea mara kwa mara watu wanaochukizwa na ziara zetu. Hata hivyo, hakuna hali ya eneo mahali po pote inayopaswa kutuambia, ‘Acha kusema.’ Bali, kama mitume, tunapaswa kusali ili tupate ujasiri ‘kuendelea kusema’—ijapokuwa chuki au uhasimu—mpaka kazi ifanywe.—Matendo 4:18-20, 24-31, NW.
15. Ni kitia-moyo kipi kinachotolewa kwenye Wagalatia 6:9, nacho kinapasa kuathirije rai yetu ya kuwatembelea majirani tukiwa na habari njema?
15 Kwa msingi, kuna aina mbili tu ya watu katika maeneo yetu yote—wale ambao kwa sasa wanapendezwa na wale ambao hawapendezwi. Basi, tunahitaji kuendelea kufanya kazi ya ‘kutafuta-tafuta wale wanaostahili.’ Kufanya hivyo ni mojapo ya kazi nyingi zilizo bora ambazo tunaweza kufanya tukiwa Wakristo kuonyesha Yehova upendo wetu na ushikamanifu wetu kwake. Basi, “tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.” (Wagalatia 6:9) Kwa kuwa sasa tunakaribia sana mwisho wa mfumo huu, huu si wakati wa kuacha au kuchoka kuwatembelea majirani zetu tukiwa na habari njema za Ufalme. Bado Yehova hajasema kwamba kazi imemalizika.
Sababu kwa Nini Tunahitaji ‘Kuendelea Kusema’
16. (a) Ni baadhi ya hali zipi zinazoweza kubadili itikio la watu katika eneo? (b) Ni vielelezo gani vya badiliko la itikio mahali penu ambavyo unaweza kutoa?
16 Tutasaidiwa pia kudumisha mwelekeo mzuri ikiwa tunakumbuka kwamba ushikamanifu kwa Yehova unaonyeshwa kwa utendaji wa kuhubiri Ufalme kwa bidii. Waaidha, maeneo yanaendelea kubadilika katika njia mbalimbali. Watu wanahama-hama, au hali huenda zao zikabadilika. Huenda ikawa hawakupendezwa mara ya mwisho tulipowatembelea, lakini kupoteza kazi, kifo cha mpendwa, badiliko kubwa sana la mng’ang’ano kati ya yale mataifa makubwa, ugonjwa mbaya sana—mabadiliko haya na mengineyo yanaweza kumaanisha kwamba wao wataitikia tunapozuru tena. Wengine, wakisha jifunze kwamba rafiki au mpendwa amekuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, huenda sasa wakataka kuzungumza nasi ili wajifunze yale ambayo tunaitikadi ambayo huenda yakawa yametokeza badiliko hilo.
17. Watu fulani sasa wanajibizaje ujumbe wa Ufalme? Toa vielelezo fulani vya mahali penu.
17 Kumbuka pia, kwamba wale ambao wamekua katika miaka ya karibuni sasa wana jamaa, wanachukua maisha kwa uzito, na wanauliza maswali ambayo Neno la Mungu tu ndilo linaloweza kujibu. Mathalani, mama mmoja kijana aliwaalika Mashahidi wawili kwenye maskani yake na akasema: ‘Nilipokuwa msichana mdogo, sikufahamu kamwe kwa nini mama yangu aliwafukuza Mashahidi na kuwaambia hakupendezwa, hali yale ambayo mlitaka kuzungumza yalikuwa juu ya Biblia. Mimi nilikata maneno kwamba nitakapokua, niolewe, na kuwa na maskani yangu mwenyewe, ningewaomba Mashahidi wa Yehova waingie na wanieleze Biblia.’
18. Mandhari ya kidini inayobadilika inaathirije eneo ambamo tunahubiri na kufundisha?
18 Je! umepata kuona kwamba watu fulani ambao hawangesema nasi kwa miaka mingi na walifikiri kwamba ‘wameokoka’ sasa wanatuuliza maswali mengi kwa weupe wa moyo? Kwa nini? Badiliko limetukia katika kufikiri kwao kwa kidini. Wanasema kwamba wamezinduka sana na kushangazwa na kufunuliwa wazi kwa mwenendo usio wa adili, utendaji wa kisiasa, na kutumiwa kwa pesa za kanisa ovyo ovyo na waeneza evanjeli fulani fulani walio mashuhuri kwenye televisheni ambao wao waliitibari wakati mmoja. Yaelekea kwamba, kutakuwa na wengi wa aina hii hali katika Babuloni Mkuu zinapoendelea kuwa mbaya kufikia mwisho wa uharibifu wake.—Ufunuo 18:1-8.
19, 20. Ni nini kinachoonyesha sababu ya kutovunjika moyo juu ya kuwaendea tena na tena watu ambao wamekataa ujumbe?
19 Kwa vyo vyote, hatupasi kuvunjika moyo wakati watu walio wengi hawawi wenye kupokea. Baada ya kuwaacha, yaelekea wangali wanatukumbuka. Katika Kanada, mwenye nyumba mmoja aliyetembelewa na Mashahidi wawili aliwaambia waziwazi kwamba hapendezwi. Baadaye, alianza kufikiria yale ambayo walikuwa wamesema na alitaka kuwatafuta ili wajibu maswali yaliyozuka akilini mwake. Aliingia kwenye gari lake na akaanza kuwatafuta katika barabara za ujirani wake lakini hakuweza kuwapata. Je! mwanamke huyo alichoka? La, alienda kwa maskani ya rafiki yake kuuliza kama walikuwa wamekuwa huko. Hawakuwa wamekuwa huko, lakini rafiki alisema kwamba angemsaidia mwanamke huyo akutane na Shahidi mmoja mahali pa kazi pa huyo rafiki yake. Matokeo yalikuwa kwamba mwanamke huyo mwenye kupendezwa alitembelewa mfululizo, naye alikaribisha marafiki, majirani, watu wa ukoo, na wafanya kazi wenzi. Nyakati nyingine watu wengi kama 15 wamekuwapo, karibu vitabu na Biblia 430 na magazeti 2,015 yameangushwa.
20 Wengi wanathamini ziara zetu. Katika barua moja iliyoandikiwa afisi ya tawi ya Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, mwanamke mmoja alisema hivi: “Asante sana kwa kuingiza kujitoa kukubwa katika mioyo ya wale wenye imani yenu. Asante kwa kutembelea . . . na kushiriki upendo wa Bwana pamoja na wengine. Tendo hilo dogo linawafanyia wengine mengi sana. . . . Ijapokuwa huenda wengine wakawa wakatili, wengine wenye ubaridi, na wengine wenye kupokea, . . . kwa kweli inasaidia sana kuwa na mtu wa kukukumbusha mambo ya kiroho. Mimi naliona jambo hilo kuwa zuri, kuzungumza juu ya Bwana mtu mmoja na mwenzake.” Katika barua nyingine, mwenye nyumba alituomba ‘tusichoshwe na watu,’ hata watutendeje. “Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozjimia roho.” (Wagalatia 6:9) Kazi hii ina upendeleo na baraka ya Yehova kushiriki kwetu kunathibitisha upendo wetu kwake na kwa jirani yetu. (Mathayo 22:37-39) Kwa hiyo acheni tuifanye kazi hii mpaka imalizike.—Linganisha Wafilipi 1:6.
21. (a) Yaelekea angalau, ni wapi lilipo takwa gumu la kwenda tena kwenye maeneo ambayo yanafanyiwa kazi mara kwa mara? (b) Tutazungumzia nini katika makala inayofuata?
21 Lazima tukubali uhakika wa kwamba sikuzote si watu wanaofanya iwe vigumu kufanyia eneo kazi mara kwa mara. Nyakati nyingine ni sisi wenyewe. Je! tunaanza tukiwa na maoni hasi, tukihisi kwamba tunawajua watu wote na mijibizo yao itakuwa nini? Hilo linaweza kuathiri mwelekeo wetu na yaelekea inaweza kuathiri sauti na sura yetu. Je! tungali tunatumia njia zile zile na maneno yale yale ambayo tumetumia kwa miaka mingi? Kwa kuwa sasa eneo linabadilika, kile ambacho wakati mmoja kilikuwa na mafanikio huenda kisiwafikie wengine “wanaostahili.” Labda tunahitaji njia nyingine ya kufikia na kuiona kazi yetu kwa njia tofauti. Jambo la pili, acheni tuone kile ambacho tunaweza kufanya ili “tusichoke” bali tuweze ‘kuvuna kwa wakati wake.’
Je! Unaweza Kueleza?
◻ Kwa nini hatupaswi “kuchoka” kuwaendea majirani zetu tukiwa na habari njema?
◻ Ni nani aliyetuambia tufanye wanafunzi katika njia tunayofanya, na mambo ya msingi ya njia hiyo ni yapi?
◻ Ni hali gani ambayo imetokea katika maeneo mengi, na ni nini kitakachotusaidia tudumishe mwelekeo unaofaa kuhusu hali hiyo?
◻ Kwa nini tunapaswa ‘kuendelea kusema’ habari njema “bila kukoma”?
-
-
Toa Uangalifu Daima kwa Fundisho LakoMnara wa Mlinzi—1988 | Julai 15
-
-
Toa Uangalifu Daima kwa Fundisho Lako
“Toa uangalifu daima kwa wewe mwenyewe na kwa fundisho lako. Endelea katika vitu hivyo, kwa kuwa kwa kufanya hivyo utaokoa wote wawili wewe mwenyewe na wale wanaosikiliza wewe.”—TIMOTHEO 4:16, NW
1 Kwa nini huu sio wakati wa sisi kupunguza mwendo katika kazi yetu ya kuhubiri Ufalme?
SASA Yehova anaharakisha kukusanywa kwa watu wa aina ya kondoo. Kwa kweli, basi, huu si wakati wa watu wake kupunguza mwendo katika kazi yao ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi. (Isaya 60:8, 22; Mathayo 24:14; 28:19, 20) Tunahitaji kutenda kulingana na kusudi ya yale ambayo Mungu anafanya katika wakati wetu. Mwisho unapokaribia zaidi, tutakuwa tunawarudia majirani zetu mara nyingi zaidi. Kweli kweli, utendaji wa ushuhuda ulioongezeka unaofanywa na wahubiri na mapainia wengi zaidi sasa unaamsha shamba la ulimwengu. Na mwendo wa kukusanya huku kwa shangwe utakua.—Isaya 60:11; linganisha Zaburi 126:5, 6.
2. (a) Kulingana na Isaya 40:28-31, ni chanzo kipi cha nishati ambacho sisi tunaweza kuchota uthabiti unaohitajiwa ili kumaliza kazi ya kuhubiri Ufalme? (b) Kuna sababu nzuri gani ya kutoa uangalifu zaidi kuelekea huduma yetu wakati huu?
2 Badala ya kuanguka katika hisia yo yote ya ‘kuchoka’ kwa sababu eneo fulani linaenezwa mara kwa mara, tunapaswa kung’amua kwamba huu ndio wakati wetu sisi kusali kwa Yehova kwa ajili ya “nishati msukumo” inayohitajiwa kumaliza kazi hii. (Isaya 40:28-31; 1 Yohana 5:14, NW) Kweli, mamilioni ya “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” tayari wamekusanywa. Lakini kitu fulani ambacho wakati mmoja kilikuwa chenye mafanikio katika kuwasaidia watu fulani huenda kisiwe tena chenye matokeo katika kuwasaidia watu wengine ambao wangali katika maeneo yetu. (Ufunuo 7:9, 10; Yohana 10:16) Kwa sababu hiyo, ubora wa huduma yetu unahitaji uangalifu zaidi.
3. Idili mpya inawezaje kuingizwa katika huduma yetu ya shambani?
3 Kwa kupiga moyo konde tena, tunaweza kukaza fikira kufanyia maendeleo matokeo yetu katika huduma. Hilo linaweza kuupa utumishi wetu wa shambani idili mpya. Lakini jambo hilo linaweza kufanywa kwa jinsi gani? Kwa ‘kutoa uangalifu daima kwetu wenyewe na kwa fundisho letu,’ si kwa kufanya huduma yetu kama kawaida tu. (1 Timotheo 4:16, NW) Midomo yetu inapasa kutoa zaidi ya “dhabihu ya sifa” ya haraka haraka tu. (Waebrania 13:15) Tunapaswa kuwa stadi katika kazi yetu. (Mithali 22:29) Basi, kinachohitajiwa ni kufanyia eneo letu kazi kwa ustadi. Hapa pana pande fulani za huduma yetu ambazo tunahitaji ‘kutoa uangalifu daima.’
Jinsi ya Kusitawisha Eneo “Jipya”
4. Ni katika njia gani tunaweza kusitawisha eneo “jipya” katika ule mgawo wetu wa kundi?
4 Acheni tuangalie hali hii katika njia yenye mafaa. Katika sehemu nyingi, hakuna eneo jipya wala lisilofanyiwa kazi mara nyingi. Kwa hivyo basi mbona msisitawishe eneo “jipya” katika mgawo wa kundi? Jinsi gani? Basi, tunapotembea mara kwa mara, hatuwezi kutenda kana kwamba hatujawahi kutembelea maskani hayo wakati mwingine kwa kusema tu yale ambayo tumesema kwa kawaida milangoni. Yaelekea, kwa vyo vyote mwenye nyumba atatung’amua ikiwa tumeeneza eneo hilo kwa kurudia-rudia. Kitabu Reasoning From the Scriptures kinatoa zaidi ya matangulizi 40 ambayo tunaweza kutumia katika huduma yetu. Lazima tuyatayarishe vizuri kama kitu kipya na chenye kuvutia kwa kuyaunganisha na mambo yanayopendeza ya karibuni na ya mahali petu. Badala ya kuhisi sikitiko kuhusu kutembea kwetu mara kwa mara, tunahitaji kuwa na mwelekeo chanya na kufanya eneo letu liwe “jipya” kwa kutoa utoaji ulio bora. Lakini je! hili litasaidia ikiwa wenye nyumba si wenye urafiki?
5. (a) Tunaweza kufanyaje mwelekeo usio wa kirafiki uliotangulia kuonyeshwa utufaidi? (b) Wewe umepata mambo gani yanayotokeza matokeo mazuri mahali penu? (c) Kwa nini kusikiliza na kusifu kwa kufuata haki kunasaidia?
5 Kujua mwelekeo wa wakati uliopita wa mwenye nyumba unaweza kufanya tuwe na hisia hasi kuhusu kutembelea tena. Lakini mbona usifanye maarifa hayo yakufaidi? Jinsi gani? Labda kwa kuyataja kijuu-juu kwanza kisha kuendeleza yale yaliyosemwa wakati wa ziara iliyopita. Huenda ukasema: “Habari ya asubuhi, Bw. Harris!” Ikiwa linaonekana kuwa jambo linalofaa unaweza kuongezea hivi: “Umeshindaje?” Kisha unaweza kusema: “Nilipokuwa hapa juma lililopita, uliniambia kwamba kanisa lako lilishughulikia mahitaji yako yote ya kiroho na kwamba wewe ni mshiriki anayejihusisha sana nalo. Nikiwa jirani ambaye anachukua dini kwa uzito pia ebu niulize kanisa lako linasema nini juu ya tumaini la kuokolewa katika kizazi hiki cha nyukilia?” Kisha acha akueleze. Msifu mwenye nyumba mahali ambapo unaona unaweza kufanya hivyo kwa ufuataji haki. Kumsikiliza na kumsifu huenda kukabadili mwelekeo wake. Mara nyingi, watu watakubali kutembelewa tena ikiwa wao wenyewe wanaweza kuzungumza. Bila shaka, utataka kurekebisha ujumbe wako kulingana na yale ambayo mwenye nyumba anasema.
6. (a) Tunaweza kuwazoezaje wenye nyumba watutazamie tuzuru kwa ukawaida? (b) Ni maneno gani ya msingi yanayoweza kutusaidia tufanikiwe? (c) Ni mambo gani yanayotokeza matokeo mazuri mahali penu?
6 Kwa yale ambayo unasema, unaweza kuwazoeza wenye nyumba watutazamie tuzuru kwa ukawaida. Jaribu kusema: “Habari, Bi. Fredericks! U hali gani leo? Katika ziara hii kwa majirani wetu, tunazungumzia . . .” Au unaweza kusema: “Habari ya asubuhi! Tunafanya ziara zetu za kila juma. Ni vizuri kuwa hapa tena. Majirani wako wamefurahia habari mpya ambayo tunazungumza katika ziara hii.” Kisha endelea. Jambo hilo linafanya eneo liwe “jipya” kwako pia. Maneno yenyewe yanaweza kutofautiana kidogo katika bara lako, Iakini hii inatoa wazo kuu. Mbona usiitumie kadiri uwezavyo kwa faida yako?
7. (a) Wakati wa kuondoka, Mashahidi fulani fulani wanatayarishaje mwenye nyumba kwa ajili ya ziara nyingine? (b) Kwa habari hii, ni mambo gani yanayotokeza matokeo mazuri mahali penu?
7 Ili kumtayarisha mwenye nyumba kwa ajili ya ziara itakayofuata, Mashahidi fulani wana mafanikio kwa kumalizia hivi: “Tunatazamia kukutembelea tena karibuni.” Kwa wale ambao hawakutaka kuzungumza nawe mara ya kwanza, unaweza kusema hivi: “Nimefurahia mazungumzo yetu. Kwa kweli ulisema maneno fulani mazuri. Hii ilichukua dakika chache, lakini angalau hatukuongea habari mbaya, ambazo tunaweza kusikia wakati wo wote. Hakika mazungumzo yalikuwa yenye kujenga.” Bila shaka, utasitawisha njia nyingine zinazofaa za kuzungumza na wenye nyumba. Kwa vyo vyote, kwa maneno yanayofaa, utoaji ulio bora, na urafiki, jitahidi kusaidia halaiki wasichukizwe na ziara zetu za kawaida.
Toa Ushuhuda Kikamili
8, 9. Ni madokezo gani yanayotolewa kwa kutafuta-tafuta wanaostahili kwa ukamili?
8 Jambo jingine ambalo tunaweza kutoa uangalifu kwalo ambalo litaendeleza idili yetu ni kutafuta-tafuta kwa ukamili zaidi wale wanaostahili. (Matendo 8:25; 20:24) Mathalani, huenda ndugu akaomba mume wa nyumba aje ikiwa mke au mtoto anakuja mlangoni wakati wa miisho juma au jioni. Pengine mke ndiye tumezungumza naye mara nyingi. Kwa hiyo tunaweza kuanza upya na jamaa kwa kuzungumza na kichwa cha jamaa. Tunaweza kurekebisha ujumbe umfae yeye, tukisema mambo kama vile, “Unafikiri ni nini kitakachohakikishia jamaa yako wakati ujao wenye furaha?” au, “Angalia jinsi Biblia inavyoendeleza umoja wa jamaa.” Sifu mwanamume huyo kwa maoni mazuri ambayo huenda akatoa.
9 Njia nyingine ya kupata eneo “jipya” ni kutafuta washiriki wengine wa jamaa wanaoishi katika nyumba ile ile—nyanya, mpwa au binamu anayeenda shule, shemeji wa kike anayefanya kazi wakati wa juma. Limekuwa jambo lenye mafaa pia kuangalia ni mita ngapi za stima au sanduku za posta zilizopo katika makao. Hii inaweza kuonyesha mahali ambapo watu wametengeneza upya orofa ya chini, orofa ya juu kabisa, au sehemu nyingine ya kupangisha. Jaribu kuwafikia wale ambao wamepanga—wanafunzi, wafanya kazi waseja, wajane, na wengine. Jambo hili pia linasaidia kupanua eneo linalopatikana.
10. Ni njia gani nyingine ya kupanua eneo letu la nyumba kwa nyumba, na wengine wamefanya nini ili kuwafikia wafanya kazi wa usiku?
10 Njia nyingine zaidi ya kupanua eneo la nyumba kwa nyumba ni kwa kuliacha lipumzike nyakati nyingine tunaposhiriki katika sehemu nyingine za huduma yetu. Kwa mambo mbalimbali, tunaweza kufanyia eneo kazi tukitoa moja kwa moja funzo la nyumbani la jamaa la Biblia bure. Watu fulani ambao hawapatikani nyumbani tunapozuru wanaweza kupatikana mahali pao pa biashara au pa kazi. Na kutoa ushuhuda katika maeneo ya kibiashara kunaweza kuwa kwenye matokeo sana. Wengine wa watu hawa wanaweza kufikiwa ikiwa tunatoa ushuhuda barabarani wakati unaofaa, masaa yenye matokeo. Katika Kanada, mapainia wamekuwa na matokeo mazuri kutokana na kuwatembelea wafanya kazi wanaofanya kazi usiku wote kwenye vituo vya petroli, maduka, na mahoteli ambapo karani hawana kazi nyingi wakati huo na mara nyingi wanathamini kuwa na kitu cha kusoma. Bila shaka, akina dada wangehitaji kuepuka sehemu fulani-fulani saa za usiku-usiku.
11. (a) Mashahidi fulani wanafanya nini mahali ambapo wengi hawapatikani nyumbani wakati wa ziara ya kwanza? (b) Juhudi katika kurudia wasiopatikana nyumbani inaweza kuathirije eneo letu na kukiwa na matokeo gani katika huduma?
11 Namna gani wale ambao hawako nyumbani tunapozuru? Hapa tena, lazima tuwe kamili. Mashahidi fulani wanatumia maandishi yao ya mlango kwa mlango yaliyotunzwa vizuri baada tu ya kazi yao ya nyumba kwa nyumba na kurudia sehemu ambazo watu hawakupatikana nyumbani mapema siku hiyo. Mara nyingi, wenye nyumba wamerudi nyumbani au wafanya kazi wa usiku wameamka kufikia wakati huo. Katika sehemu nyingi, asilimia 50 au zaidi hawamo manyumbani wakati wa mchana. Kwa hiyo kwa kweli tunaweza, kwa matokeo mazuri, kuzidisha maradufu eneo hilo kwa kufanya ziara za wasiopatikana nyumbani saa tofauti-tofauti mpaka tupate mtu fulani nyumbani. Mapainia na wahubiri wenye ujuzi wanakubali kwamba juhudi katika kufanyia kazi nyumba zisizopatikana watu mara nyingi inatokeza matokeo mazuri kuliko kueneza eneo mara ya kwanza. Kwa kutoa uangalifu kwa upande huu wa huduma yetu inaelekea tutavuna baraka nyingi.—Mithali 10:22.
Wale Wanaolalamika
12. Tunapaswa kujibizaje wakati watu wanapolalamika kwamba sisi tunazuru mara nyingi mno? Kwa nini?
12 Ni jambo gani linaloweza kuambiwa watu ambao wanalalamika kwamba sisi tunazuru mara nyingi sana? Zaidi ya yote, lazima tuonyeshe ufahamivu. (Mathayo 7:12) Kwao inaonekana kwamba tumerudi haraka sana. Lakini ni vizuri kukumbuka kwamba hata miaka mingi iliyopita watu walikuwa wakisema, ‘Mlikuwa hapa juma lililopita’ hali tulijua vizuri kabisa kwamba ilikuwa miezi sita au zaidi tangu tulipozuru. Mbali na hilo, ziara za mara kwa mara zinaweza kuamsha kupendezwa. Katika Guadeloupe, mwanamume mmoja alimkimbilia Shahidi ili amwambie: “Mimi nimekuchunguza kwa majuma mengi sasa. Kwa kawaida, mimi sisikilizi Mashahidi, lakini ninataka kujua kwa nini mnatembelea watu mara nyingi sana!” Funzo la Biblia jipya lilianzishwa.
13, 14. Wengine wa waitikadi wenzetu wanashughulikiaje mambo wakati wenye nyumba wanapolalamika?
13 Akina ndugu fulani wamewaambia walalamikaji kwa fadhili tarehe yenyewe ya zaira yao ya mwisho na wakatoa magazeti ya karibuni, wakionyesha wazi kwamba makala zinatofautiana na zile zilizokuwa katika majarida ambayo tulikuwa nao wakati wa mwisho tulipozuru. Kwa kusababu pamoja na wenye nyumba hao, tunaweza kusema kwamba pengine wamepokea karatasi-habari na magazeti mengi tangu tulipozuru mara ya mwisho, lakini si sikuzote hayo yamekuwa na habari njema. Tunaweza kueleza kwamba tunaleta habari njema na kwamba ziara zetu si ndefu. Lakini ikiwa mwenye nyumba ana shughuli nyingi, tungeweza kusema: “Ikiwa huu sio wakati unaofaa kusema nawe, nitakuona tutakapozuru tena baada ya juma moja hivi.”
14 Ni jambo gani lingine tunaloweza kusema? Hii inategemea mwelekeo wa mwenye nyumba na heshima ya kawaida inayotazamiwa mahali tunapoishi. Dada mmoja katika Japani anaeleza juu ya ziara zetu za mara kwa mara katika njia hii: ‘Habari za televisheni zitaripoti juu ya mwendo wa kimbunga tena na tena, zikirudia habari hiyo mara kwa mara kwa manufaa ya wale ambao huenda wakawa wamezikosa wakati wa matangazo yaliyotangulia. Jambo hilo linafanywa kwa sababu uhai unahusika. Kurudia ripoti hizo mara kwa mara kunaongezeka tufani hiyo inapokaribia. Kwa hiyo, tufani ya Har–Magedoni inapokaribia, lazima ujumbe wa kuonya utangazwe mara nyingi iwezekanavyo ili kuokoa uhai.’ Bila shaka, tungesema maneno hayo kwa fadhili na kwa weupe wa moyo, tukitumaini kufikia moyo wa msikilizaji.
Kushinda Tatizo la Ubaridi
15. (a) Ni tatizo gani lenye kukua linaloweza kutokea wakati tunapolifanyia eneo letu kazi mara kwa mara? (b) Kwa sababu gani watu fulani ni wenye ubaridi?
15 Ziara zetu zinapoongezeka, tatizo linaloongezeka ni ubaridi ambao tunakabiliana nao mara kwa mara. Lakini tunapochunguza sababu nyingine za ubaridi, inaweza kututia moyo kuona kwamba bado inawezekana kufikia mioyo ya wengine wa watu hawa. Ubaridi wao unaweza kuonyesha kuvurugika akili na kukosa kwao tumaini. Huenda wakahisi kwamba hakuna njia ya kutoka katika hali iliyopo ya ulimwengu huu, wakisababu kwamba wataishi tu maisha zao katika njia nzuri wanayoweza. Wengine wanaona kinyaa kwa sababu viongozi fulani wa kidini wanahusika katika siasa, wana hatia ya mwenendo usio wa adili, au wanashindwa kuchukua msimamo imara dhidi ya ukosefu wa adili katika ngono. Kwa hiyo wenye nyumba hawa wamezinduka na wanaishi kwa ajili ya leo tu.
16. Moyo wa mtu mwenye ubaridi unawezaje kufikiwa?
16 Tunajua kwamba wahudumu Wakristo wa mapema walikabili mwelekeo huo huo kwa mafanikio, kwa kuwa wakati huo watu fulani walisema, “Na tule, na tunywe, maana kesho tutakufa.” (1 Wakorintho 15:32) Kwa sababu hiyo, tunajua kwamba tuna kile ambacho watu hao wanahitaji kusikia. Bado, tunawezaje kufikia moyo wao? Njia moja ni kuweka kando kichapo chetu cha Biblia kwa wakati huo, ukiwaacha waone wewe ukifanya hivyo. Kisha tunaweza kuwauliza maswali yaliyofikiriwa vizuri kama haya: “Je! wewe unafikiri kuna utatuzi fulani kwa matatizo yaliyopo siku hizi? Je! inaweza kuwa kwamba watu wengi hawajapata utatuzi bado? Je! unafikiri tunapaswa kuwa na mwelekeo chanya na kuendelea kutafuta?” Kwa wengine, tunaweza kusema: “Kwa kweli unakubali kwamba ni afadhali kuishi ukiwa na tumaini kuliko kutokuwa na taraja lo lote la vitu vizuri. Wewe unatumaini kuona nini?” Tunaweza kuuliza: “Wewe mwenyewe unahisi ni nini kilicho kizuizi kikubwa cha umoja na amani ya ulimwengu?” Bado wengine wanaweza kuulizwa: “Je! wewe unafikiri dini zote ziko kama vile umeeleza?” Mara nyingi maswali ya namna hiyo yatawafanya wenye nyumba kueleza rai yao. Kisha, wanapoitikia, hakikisha kwamba unasikiliza. Ndiyo, acha wakuambia kilicho moyoni mwao. Wengi wao ‘wanatweta na kupiga kite juu ya vitu vyote vyenye kukirihika vinavyofanywa sasa.’—Ezekieli 9:4, NW.
17. Vichapo vyetu vinaweza kutumiwaje kuwafikia watu fulani hata wakati wanaposisitiza mara ya kwanza kwamba hawapendezwi?
17 Njia nyingine ya kushughulikia ubaridi ni kukumbuka neno moja au kipingamizi ambacho mwenye nyumba anatokeza na kurudi ukiwa na gazeti au kichapo cha Mnara wa Mlinzi kinachoshughulikia habari hiyo. Kwanza, huenda hata ikawa si habari ya kidini, kama vile makala yenye kuzungumzia kifo cha ghafula cha mtoto au kumalizika kwa misitu. Eleza kwamba ulikuwa ukifikiria jambo lililopendeza mwenye nyumba na ukakumbuka makala hiyo. Kisha onyesha mambo ya msingi katika habari hiyo. Mwanamke mmoja ambaye alikuwa amekataa kichapo chetu alikubali gazeti sekunde chache baadaye. Kwa nini? Kwa kuwa Shahidi aliuliza ikiwa mwanamke huyo alijua kwamba kulikuwa na utoaji mimba milioni 55 kila mwaka. Kwa kugutuka kujua hilo, aliomba gazeti lenye habari hizo.
Ione Ikimalizika
18, 19. (a) Tunapaswa ‘kutoa uangalifu’ kwa mambo gani ya kuongezea tunapofanya huduma yetu? (b) Watu fulani wana maoni gani ya kuchukia sisi na itikadi zetu bila sababu, nasi tunaweza kuwajibuje?
18 Zaidi ya yote, tunahitaji kuwaonyesha watu subira. Zungumza kwa polepole, kwa uchangamfu. Onyesha upendo na fadhili. (Wagalatia 5:22, 23) Kabla ya kwenda kwenye mlango unaofuata, fikiria kilichotokea kwenye mlango uliotangulia ili uone mahali ambapo maendeleo yanaweza kufanywa. Uwe mwenye kufahamu, kwa kuwa watu wengi wana maoni mabaya juu ya Mashahidi wa Yehova. Huenda wakasema: ‘Ninyi mnakataa siasa na kazi za kiserikali,’ ‘Ninyi mnakataa utumishi wa kijeshi,’ au ‘Ninyi mnavunja jamaa.’ Lakini mwelekeo huu ni kama ule wa ulimwengu kuelekea waitikadi wenzetu wa karne ya kwanza. Waonyeshe wenye nyumba hilo, labda ukitumia manukuu yaliyo chini ya kichwa “Kutokuwamo” katika kitabu Reasoning.
19 Kwa habari ya Wakristo wa mapema, mwanahistoria Will Durant aliandika hivi: “Kwa Mkristo dini yake ilikuwa kitu fulani zaidi ya na kikubwa kuliko jamii ya kisiasa; utii wake ulio mkubwa ulikuwa kwa Kristo si kwa Kaisari. . . . Mtengano wa Mkristo kutoka kwa shughuli za kidunia ulionekana kwa wapagani kuwa kukimbia kazi ya kiserikali, kudhoofika kwa uzi na mapenzi ya kitaifa. Tertullian alishauri Wakristo wakatae utumishi wa kijeshi;... Wakristo walisihiwa na viongozi wao wawaepuke watu wasio Wakristo, wajiepushe na karamu zao za michezo ya kishenzi, na mahali pao pa maneno ya matusi. Ukristo [ulipokuwa ukifanya waongofu] ulishtakiwa kuwa unavunja nyumba.”—Caesar and Christ, uku. 647.
20, 21. (a) Tunataka kuhakikisha nini watu wasipoitikia? (b) Kwa nini hatupaswi ‘kuchoka’ bali tuendelee na kazi yetu nzuri ya kuhubiri Ufalme?
20 Watu fulani fulani hawatasikiliza, hata tuseme nini. Lakini hiyo inapasa kuwa kwa sababu ya kukataa kwao ujumbe wa Ufalme si kwa sababu ya kushindwa kwetu kutoa utoaji ulio bora katika huduma yetu. (Luka 10:8-11; Matendo 17:32; Ezekieli 3:17-19) Tunapaswa kufanya vizuri tuwezavyo kwa msaada wa Mungu, naye Yehova ataimaliza kazi.—Linganisha Wafilipi 1:6.
21 Basi, mkiwa na utumainifu kamili, endeleeni kuwa na “mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi yenu yenye bidii si ya bure kuhusiana na Bwana.” (1 Wakorintho 15:58, NW) “Toa uangalifu daima kwa wewe mwenyewe na kwa fundisho lako. Endelea katika vitu hivyo, kwa kuwa kwa kufanya hivyo utaokoa wote wawili wewe mwenyewe na wale wanaosikiliza wewe.” (1 Timotheo 4:16, NW) Zaidi ya yote, “tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.”—Wagalatia 6:9.
Je! Unaweza Kukumbuka?
◻ Ni njia fulani zipi za kudumisha mwelekeo chanya katika eneo linalofanyiwa kazi kwa ukawaida?
◻ Tunawezaje kutafuta-tafuta wanaostahili kwa ukamili zaidi?
◻ Tunaweza kujaribu kushughulikaje na wale ambao wanalalamika kwamba tunazuru mara nyingi?
◻ Ni katika njia gani tunaweza kushughulikia tatizo la ubaridi?
◻ Ni nini kitakachofanyia maendeleo ubora wa huduma yetu?
-