-
Ukurasa wa Kichwa/Ukurasa wa WachapishajiMashahidi wa Yehova na Elimu
-
-
Ukurasa wa Kichwa/Ukurasa wa Wachapishaji
Mashahidi wa Yehova na Elimu
Broshua hii haiuzwi. Ni sehemu ya kazi ya elimu ya Biblia ya ulimwenguni pote inayotegemezwa kwa michango ya hiari.
Ikiwa ungependa kutoa mchango, tafadhali tembelea donate.jw.org.
Isipokuwa imeonyeshwa vingine, manukuu ya Maandiko yametoka katika Biblia ya Union Version ya Kiswahili
Chapa ya Januari 2019
Swahili (ed-SW)
© 1995, 2002, 2015 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
-
-
Kusudi la Broshua HiiMashahidi wa Yehova na Elimu
-
-
Kusudi la Broshua Hii
MWANAFALSAFA Mholanzi Spinoza aliandika hivi: “Nimejaribu kutoyacheka matendo ya binadamu, kutoyatolea machozi, wala kutoyachukia, bali kuyaelewa.” Ukiwa mwelimishaji, wewe hukabili ugumu wa kujaribu kuelewa maoni, malezi, na masadikisho ya wanafunzi unaowatunza, kutia na wanafunzi ambao ni watoto wa Mashahidi wa Yehova. Nyakati nyingine, wanafunzi hao huenda wakachukua msimamo ambao waonekana si wa kawaida juu ya masuala fulani. Lakini inapokuwa wazi kwamba matendo hayo yatokana na masadikisho ya mwanafunzi ya kidini na ya kiadili, yanastahili uangalifu wako. Broshua hii imetolewa na Watch Tower Bible and Tract Society (shirika la utangazaji la Mashahidi wa Yehova) na imekusudiwa kukusaidia uwaelewe vizuri zaidi wanafunzi Mashahidi. Twatumaini utachukua wakati kuisoma kwa uangalifu.
Kuelewa itikadi za kidini za mtu mwingine hakutaki kwamba uzikubali au uzifuate, na kumjulisha mtu si kumgeuza imani. Broshua hii haijaribu kukulazimisha wewe wala wanafunzi wako kukubali maoni fulani ya kidini. Tamaa yetu ni kukujulisha tu kanuni na itikadi ambazo baadhi ya wanafunzi wako wanafundishwa na wazazi wao ili iwe rahisi kwako kuwaelewa watoto Mashahidi na pia kushirikiana nao. Bila shaka, yale ambayo watoto wanafundishwa na yale wanayofanya hayapatani sikuzote, kwa kuwa kila mtoto anajifunza kusitawisha dhamiri yake mwenyewe.
Kama vile wazazi walio wengi, Mashahidi wa Yehova hutaka watoto wao wanufaike kikamili na elimu yao. Kwa kusudi hilo, wao huwafundisha watoto wao washirikiane na walimu wao. Kisha, wazazi Mashahidi na watoto wao huthamini wakati waelimishaji wanapowatendea kwa uelewevu na staha.
Mashahidi wa Yehova ni Wakristo wanaojulikana ulimwenguni pote. Hata hivyo nyakati nyingine watu huwaelewa vibaya. Kwa hiyo, tumaini letu ni kwamba broshua hii itakusaidia uwaelewe vizuri zaidi watoto Mashahidi unaowatunza. Hasa, twatumaini utaona ni kwa nini, katika hali fulani hususa, huenda wakadai haki ya kuwa tofauti.
-
-
Jinsi Mashahidi wa Yehova Huona ElimuMashahidi wa Yehova na Elimu
-
-
Jinsi Mashahidi wa Yehova Huona Elimu
Kama vile wazazi wote, Mashahidi wa Yehova wanahangaikia wakati ujao wa watoto wao. Kwa hiyo wao huiona elimu kuwa ya maana sana. “Elimu yapaswa kusaidia watu wawe washiriki wa jamii wenye mafaa. Yapaswa pia kuwasaidia wasitawishe ufahamu wa urithi wao wa kitamaduni na kuishi maisha yenye kuridhisha zaidi.”
KAMA vile nukuu hili kutoka katika The World Book Encyclopedia lidokezavyo, mojapo makusudi makuu ya elimu ni kuzoeza watoto kwa ajili ya maisha ya kila siku, ambalo latia ndani kuwawezesha kutunza mahitaji ya familia siku moja. Mashahidi wa Yehova huamini kwamba hili ni daraka takatifu. Biblia yenyewe husema hivi: “Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.” (1 Timotheo 5:8) Miaka inayotumiwa shuleni hutayarisha watoto kwa ajili ya madaraka watakayopata maishani. Kwa hiyo, Mashahidi huhisi kwamba elimu yapasa kuchukuliwa kwa uzito sana.
“Elimu yapaswa kusaidia watu wawe washiriki wa jamii wenye mafaa. Yapaswa pia kuwasaidia wasitawishe ufahamu wa urithi wao wa kitamaduni na kuishi maisha yenye kuridhisha zaidi.” —The World Book Encyclopedia
Mashahidi hujitahidi kuishi kulingana na amri hii ya Biblia: “Lolote mfanyalo, mlifanye kwa moyo wenu wote, kana kwamba mwamfanyia Bwana na si wanadamu.” (Wakolosai 3:23, Today’s English Version) Kanuni hiyo yatumika kuhusu sehemu zote za maisha ya kila siku, kutia ndani shule. Hivyo Mashahidi hutia moyo vijana wao wasome kwa bidii na kuchukua kwa uzito kazi wanazogawiwa shuleni.
“Lolote mfanyalo, mlifanye kwa moyo wenu wote, kana kwamba mwamfanyia Bwana.”—Wakolosai 3:23, Today’s English Version
Biblia hufundisha pia kutii sheria za nchi ambako mtu aishi. Kwa hiyo elimu inapokuwa ya lazima hadi umri fulani, Mashahidi wa Yehova hutii sheria hiyo.—Warumi 13:1-7.
Starehe ifaayo, muziki, mambo ya kujifurahisha, mazoezi ya kimwili, na kuzuru maktaba na nyumba za kuhifadhi mambo ya kale yote ni sehemu ya maana katika elimu yenye usawaziko
Bila kupunguza umaana wa mazoezi kwa ajili ya maisha ya kila siku, Biblia huonyesha kwamba hili si lengo pekee wala lengo kuu la elimu. Elimu yenye mafanikio yapasa pia ikuze ndani ya watoto shangwe ya kuishi, na kuwasaidia wachukue mahali pao katika jamii wakiwa watu mmoja-mmoja wenye usawaziko mzuri. Hivyo, Mashahidi wa Yehova huhisi kwamba chaguo la utendaji wa ziada baada ya masomo ya darasani ni la maana sana. Wao huamini kwamba starehe ifaayo, muziki, mambo ya kujifurahisha, mazoezi ya kimwili, kuzuru maktaba na nyumba za kuhifadhi mambo ya kale, na kadhalika, ni sehemu ya maana katika elimu yenye usawaziko. Kwa kuongezea, wao hufundisha watoto wao wastahi watu wenye umri mkubwa na kutafuta fursa za kuwasaidia.
Namna Gani Elimu ya Ziada?
Kwa sababu ya tekinolojia mpya, fursa za kupata kazi zinabadilika daima. Likiwa tokeo, vijana wengi watalazimika kufanya kazi katika sehemu au katika ufundi mbalimbali ambao hawajapata mazoezi hususa juu yao. Hali ikiwa ni hivyo, tabia zao za kufanya kazi na mazoezi yao ya kibinafsi, na hasa uwezo wao wa kubadilikana na hali, utakuwa wenye thamani
-