Wimbo 171
Wimbo wa Ushindi
1. ‘Mwimbieni Yah, Kwa sababu amekwezwa sana.
Farasi na mutu Watupwa baharini.
Nguvu zangu ndiye Yah, ’mekuwa wokovu wangu.
Mungu wangu; Nitamutukuza.
‘Jeshi ya Farao yafa majini Yametupwa baharini. Na
Mukono kuume, Yehova, Ni wenye nguvu sana.’
2. Waisraeli, Yehova akawapa ushindi.
Na Ushindi mwingi Twaona leo hii.
Yesu sasa Mufalme, Mufumo wa kale kwisha.
Twafurahi, Waja ukombozi!
Joka, Shetani, na malaika ‘ovu—Wametupwa mpaka chini.
Na Mwana-Kondoo ashinda Sasa giza laisha.
3. Musifuni Yah. Utukufu wa Yehova Mungu.
Ufalme tayari, Utakomesha mambo.
Na tumusifu Mungu. Na tumushukuru Yesu.
Tufurahi Tunaishi leo.
Mungu Yehova na Masihi wake Twawatolea shukurani.
Ni hao tu wenye wokovu. Tutaimba ushindi!