-
Sababu Gani Wewe Unataka Kutoa Hotuba ya Biblia?Mnara wa Mlinzi—1985 | Oktoba 1
-
-
kwenye “vitendo vitakatifu vya mwenendo na matendo ya utawa.”—2 Petro 3:11, NW.
Tamaa ya moyo mweupe ya kujenga waamini wenzetu na wengine inapasa pia kuwa ndilo kusudi letu la kutoa hotuba ya watu wote. Jambo hilo litatuzuia tusijaribu ‘kutekenya masikio’ ya wasikilizaji wetu kwa kuwaambia yale tu wanayotaka kusikia. (2 Timotheo 4:3, NW) Tamaa ya kujenga wengine kiroho itatusukuma pia tuepuke kufanya mizaha au kusema mambo yanayokusudiwa tu kufurahisha wasikilizaji au kuwafanya wacheke. Wala hatutatumia maneno yaliyotiwa sukari nyingi kwa kusudi la kujionyesha. Wala hatutaonyesha hekima ya kilimwengu kwa kujitahidi kufanya wasikiaji watushangae. Bali, tukiwa na kusudi linalofaa la kusema mbele ya watu wote, tutafuata mfano wa mtume Paulo, ambaye alionyesha ‘dalili ya roho na ya nguvu, ili imani ya wasikiaji wake isiwe katika hekima ya wana-damu, bali katika nguvu za Mungu.’—1 Wakorintho 2:3-5.
Mambo Matatu ya Msingi
Kutoa hotuba ya Kibiblia ya watu wote kunahusiana na hali ya akili na moyo. Basi, zaidi ya kuwa ni lazima wasemaji Wakristo wawe na nia inayofaa, ni lazima pia wawe na jambo lenye mafaa la kusema. Hiyo inataka wafikirie mambo matatu ya msingi. Hayo ni Maandiko, mambo hakika, na usadikishi unaotumia sababu zenye utimamu.
Kwanza, ni lazima ikumbukwe kwamba kwa wazi wazo kuu la hotuba ya Kibiblia ya watu wote linapasa kuonyeshwa na maandiko yanayotumiwa na msemaji. Ukipewa pendeleo la kutoa hotuba kama hiyo, inakupasa uijue vizuri habari yako na kuyatumia inavyofaa. Siku ya Pentekoste, 33 W.K., mtume Petro alitaja-taja Maandiko ili kuunga mkono maneno yake. (Matendo 2:14-41) Waberoya waliridhika kwamba Paulo alikuwa ametegemeza sana maneno yake juu ya msingi wa Maandiko. (Matendo 17:10, 11) Naye Apolo ‘alionyesha kwa maneno ya maandiko ya kuwa Yesu ni Kristo,’ Masihi aliyekuwa ametamaniwa kwa muda mrefu.—-Matendo 18:28.
Bila shaka, mtu anapewa msingi wa Kimaandiko wa hotuba ya watu wote katika muhtasari unaotolewa na Sosaiti yetu. Hata hivyo, msemaji anaweza kutumia maandiko ya ziada na mengine yanayolingana na yale yaliyoonyeshwa, mradi yanatumika kwa usawa ule ule na kwamba hayatumiwi kupita kiasi. Katika jambo hilo, ni lazima mhudumu Mkristo awe mwangalifu ayaeleze kulingana na nuru ya kiroho inayoendelea kuongezeka. Kwa mfano, huenda msemaji akatumia 1 Wakorintho 2:9 kwa njia isiyo sahihi kuhusiana na Paradiso ya kidunia ya wakati ujao, hali habari zinazozunguka (mstari 7 na 10) zinaonyesha kwamba andiko hilo linahusu mambo yale ya ndani zaidi ya hekima ya Mungu.
Pili, inafaa kufikiria mambo hakika yanayotumiwa ili kuunga mkono maneno yaliyonenwa na msemaji wa watu wote. Uangalifu unapasa utumiwe ili mambo yanayotolewa yasiwe yanaweza kutiliwa mashaka halali au kufanyiwa ubishi. Hasa uangalifu unahitajiwa ikiwa jambo fulani linaelekea kuchochea kwa urahisi maoni ya kutokubaliana na yaliyosemwa. Ni jambo la hekima—tena linahitajiwa kabisa—kuhakikisha kwamba yanayosemwa ni ya kweli. Kwa sababu hiyo, sikuzote inakuwa vizuri zaidi mtu aweze kuelekeza kwenye vyanzo vinavyotegemeka vya habari kwa kuwa huenda ikatukia kwamba maneno fulani yanatiliwa mashaka. Siku ya Pentekoste, Petro alionyesha mambo hakika yaliyojulikana sana na watu. Ndivyo pia alivyofanya mtume Paulo katika Areopago, au Kilima Mars, katika Athene.—Matendo 2:22; 17:22, 23, 28.
Tatu, ni wazi kabisa kwamba kuna uhitaji wa sadikisho lenye sababu zenye utimamu. Msemaji wa watu wote aliye Mkristo anahitaji kufikiri pamoja na wasikilizaji wake kwa kuwapa sababu. Hivyo tunasoma kwamba Paulo “akaanza kusemezana pamoja na Wayahudi na watu wale wengine walioabudu Mungu akiwatolea sababu katika sinagogi na pamoja na wale waliopatikana katika soko kila siku.” (Matendo 17:17, NW) Katika hotuba ya watu wote, sababu zinazotolewa katika kusema mambo zinapasa kuwa zenye utimamu, rahisi kufahamika, zenye kuelezwa waziwazi, nyepesi kueleweka. Msaada mkubwa katika jambo hilo ni matumizi ya viunzi vinavyoonyesha uhusiano kati ya mambo ambayo yamekwisha kusemwa na yale yanayoyafuata.
Basi, ukipewa pendeleo la kuwa msemaji wa watu wote, hakikisha kwamba una nia ya akilini inayofaa kuelekea hotuba ya Kibiblia. Moyoni mwako uwe na upendo kuelekea Muumba wako na wanadamu wenzako. Kusanya kisha utokeze maandiko na mambo hakika kwa kutumia sadikisho lenye sababu zilizo na utimamu. Ndipo mithali hii itakapokuhusu wewe: “Ulimi wa mwenye haki ni afya.” (Mithali 12:18) Zaidi ya hilo, kutoa hotuba nzuri za Kibiblia zinazotukuza Mungu ni njia moja ya ‘kuokoa nafsi yako na wale wakusikiao pia.’—1 Timotheo 4:16.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1985 | Oktoba 1
-
-
Maswali Kutoka kwa Wasomaji
■ Kwa sababu ya ripoti zinazosema kwamba huenda madaktari wakawa wanaweza kufungulia nguvu za uzazi za mtu ambaye alikuwa amefungwa kwa hiari yake mwenyewe, je! Wakristo fulani hawawezi kuichagua hiyo iwe namna moja ya kupanga uzazi?
Biblia inaonyesha kwamba Mungu anaheshimu sana nguvu za uzazi. Yeye alikusudia kwamba wanadamu waijaze dunia kwa kuzaa viumbe vya jinsi yao. (Mwanzo 1:28; 9:6, 7) Baadaye, Waisraeli waliziona jamaa kubwa-kubwa kuwa baraka kutoka kwa Yehova, na mtu alipoteza upendeleo wa Mungu alipocheza-cheza na nguvu za uzazi. (Zaburi 127:3-5; Kumbukumbu la Torati 1:11; 23:1; 25:11, 12) Mawazo hayo yaliyo katika Maandiko ya Kiebrania yamekuwa na nguvu zenye kuongoza kufikiri kwa wengi wa watumishi wa Mungu kwa habari ya zoea la kufunga nguvu za uzazi kwa hiari ya mtu.a
Ingawa hivyo, tunakuta nini katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo juu ya jambo hilo? Kwanza, tunajifunza kwamba Wakristo hawako chini ya Sheria ya Musa. (Wagalatia 3:24, 25) Tena, Yesu alihimiza Ukristo upanuliwe kwa kuhubiri habari njema, si kwa kuzaa. Kwa kuwa mavuno makubwa ya wanafunzi yangetokana na jambo hilo, Yesu aliwapa mauidha wawe matowashi kiroho wale ambao kati ya wanafunzi wangeweza kufanya hivyo, huku wakionyesha kujiweza wakiwa waseja. Kuhusiana na maana iyo hiyo, mtume Paulo aliwatia moyo Wakristo wasioe au kuolewa na hivyo wawe na uhuru mkubwa zaidi wa kuhubiri na kufundisha. Kwa njia hiyo wangekusanya watoto wa kiroho na kuwaleta ndani. Hata wenzi waliooana walipaswa kukumbuka kwamba “muda ubakio si mwingi”; mradi wao unapasa uwe ‘kutokuwa na masumbufu’ ya maisha ya kijamaa.—1 Wakorintho 7:29-32, 35; Mathayo 9:37, 38; 19:12.
Safari ile iliyokuwa yetu ya mwisho kuzungumza katika safu hii* juu ya kufunga nguvu za uzazi kwa hiari ya mtu mwenyewe, matabibu walio wengi walikuwa na maoni ya kwamba zikiisha kufungwa haziwezi kufunguliwa na hivyo ni jambo la kudumu. Lakini, matukio ya kitiba katika miaka kumi iliyopita yamebadili kidogo hali hiyo, Kwa mfano, kichapo Population Reports (Novemba-Desemba 1983, Chuo Kikuu cha Johns Hopkins) kinasema hivi juu ya visa vya upasuaji wa kufunga katika wanaume sehemu fulani ya kile kifereji kinachovuta shahawa kutoka kwenye eneo la mapumbu: “Katika ripoti za hivi majuzi, kufunguliwa kwa sehemu hiyo kumeiacha wazi tena—yaani, mbegu za uzazi zimepatikana katika umajimaji wenye kutoka humo—katika asilimia 67 mpaka 100 ya wanaume. Mafanikio yanayohusu utendaji wa kiungo hicho—yaani, uchukuaji mimba kati ya wake za wanaume ambao wamefunguliwa tena kifereji hicho—umekuwa kati ya asilimia 16 na 85.” Njia mpya za upasuaji na za kuweka vizibo vinavyokifunga kwa muda kifereji hicho zinatajwa pia kuwa zinaonyesha kwamba bado kutakuwa na mafanikio zaidi ya kufungua tena kisehemu hicho kilichokuwa kimefungwa.
Kwa kuwa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo hayatoi mwongozo wa moja kwa moja juu ya mambo hayo, ni lazima Wakristo wafanye maamuzi ya kibinafsi juu ya kuzuia jamaa yao isiwe kubwa sana na juu ya kupanga uzazi. Kwa habari ya kufunga nguvu za uzazi, inawapasa wazingatie akilini kwamba ingawa sasa inafikiriwa kwa-mba uwezekano umeongezeka wa kufungulia tena nguvu za uzazi kuliko vile ilivyokuwa miaka kumi iliyopita, matabibu hawawezi kuhakikisha kabisa kwamba nguvu za uzazi zinaweza kurudishwa.
Juu ya yote, wenzi wa ndoa wanapaswa kuendeleza dhamiri safi mbele za Yehova na kuelekea Wakristo wenzao. Ikiwa wenzi wa ndoa wanafikiria kufunga nguvu za uzazi kuwa namna fulani ya kupanga uzazi, bado inawapasa wafikirie matokeo yo yote ambayo vitendo vyao vinaweza kuleta juu ya wengine. Ingawa kwa kawaida wenzi waliooana hawatangazi-tangazi uamuzi wao juu ya kupanga uzazi, ikijulikana na watu wengi kwamba wenzi wa ndoa walienda kufungwa nguvu za uzazi kwa hiari yao wenyewe, je! ingeweza kuwa kwamba kundi litaudhika sana na kuacha kuwaheshimu?(1 Timotheo 3:2,12,13) Hayo ni mambo ya kufikiria kwa uzito sana, hata katika jambo hilo la faragha na la kibinafsi. Mwisho kabisa, maneno haya ya Paulo yanafaa: “Kwa [Yehova] bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka.”—Warumi 14:4,10-12.
-