-
Kuitikia Mwito wa Visiwa vya MicronesiaMnara wa Mlinzi—1987 | Novemba 15
-
-
sana machoni petu.” James, ambaye amekuwa mmisionari kwa miaka zaidi ya kumi, anaeleza hivi: “Kuuona uvumilivu wa ndugu Wakosrae mwaka baada ya mwaka ni baraka kweli kweli.” Huko Belau, Roger anatoa maelezo hivi: “Sisi tumebarikiwa kuwa na Jumba la Ufalme jipya na kikundi kishikamanifu cha wahubiri.” Na akitazama nyuma katika miaka iliyopita, Placido anasema: “Mwelekezo na roho takatifu ya Yehova vimeonekana wazi maishani mwetu. Jambo hili limetusaidia sisi kumkaribia yeye sana.”
Mambo yaliyoonwa kama hayo yamewatia moyo wamisionari wabaki katika migawo yao. Wengi wao wanaweza kutazama nyuma na kukumbuka kuanzishwa kwa kundi la kwanza katika sehemu yao. Kama vile mtume Paulo, wao wana furaha isiyo na kifani ya ‘kutojenga juu ya msingi wa mtu mwingine.’ (Warumi 15:20) Wanaeleza wanavyohisi vizuri sana kwa elezo hili: “Kungali kuna kazi nyingi ya kufanya. Mimi nina itikadi ya kwamba bado Yehova atafungua nafasi nyingi za kuleta ndani wenye mfano wa kondoo wengi kutoka katika visiwa hivi, nasi tumependelewa kushiriki katika kazi hiyo.”
“Baraka ya BWANA [Yehova, NW] hutajirisha, wala hachanganyi huzuni nayo,” inasema Biblia kwenye Mithali 10:22. Wale ambao wameuitikia mwito wa umisionari katika visiwa vya Micronesia kweli kweli wameona baraka hii pamoja na furaha na kutosheka kunakotokana na kumtumikia Yehova.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1987 | Novemba 15
-
-
Maswali Kutoka kwa Wasomaji
■ Je! Paulo alikuwa akielekeza kwa Yehova au kwa Yesu alipoandika: “Bwana akaniambia, uweza wangu hutimilika katika udhaifu”’?
Inaonekana kwamba mtume Paulo alikuwa akielekeza kwa Bwana Yehova. Kwa kuangalia maneno ya Paulo yanayozunguka mstari huo, si kwamba tu sisi tunaweza kuona kwa nini ndivyo ilivyo, bali tunaweza pia kuongeza kina kwa uthamini wetu kwa uhusiano uliopo kati ya Mungu na Mwana wake. Paulo aliandika:
“Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi. Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke. Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.”—2 Wakorintho 12:7-9.
Huenda ikawa kwamba mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo ulikuwa ugonjwa fulani wa macho au mitume wa uwongo waliobisha juu ya kuwa kwake mtume. (Wagalatia 4:15; 6:11; 2 Wakorintho 11:5, 12-15) Uwe ulikuwa nini, ulielekea kumvunja Paulo moyo au kumfanya asishangilie kwa ajili ya huduma yake. Hivyo yeye alisihi mara tatu ili uondolewe. Lakini yeye alimwomba nani, na ni nani aliyeitikia kwa kuzungumza juu ya “uweza wangu”?
Kwa kuwa mstari huo unataja “uweza wa Kristo,” huenda ikaonekana kwamba Paulo alimwomba Bwana Yesu. Pasipo shaka, yeye ana nguvu naye anaweza kuwapa wanafunzi wake uweza huo. (Marko5:30; 13:26; 1 Timotheo 1:12) Kwa hakika, Mwana wa Mungu ‘anategemeza vyote kwa neno la nguvu zake.’—Waebrania 1:3, NW; Wakolosai 1:17,29.
Hata hivyo, Bwana Mungu ndiye chanzo cha kikuu kabisa cha nguvu, ambao anaweza kuwapa na anawapa waabudu wake. (Zaburi 147:5; Isaya 40:26, 29-31) Nguvu hiyo kutoka kwa Mungu ilimwezesha Yesu afanye miujiza na bado itamwezesha atende.(Luka5:17; Matendo 10:38) Vilevile, mitume wa Yesu na wanafunzi wengine walipokea nguvu kutoka kwa Yehova.(Luka 24:49; Waefeso 3:14-16; 2 Timotheo 1:7,8) Hii ilitia ndani Paulo, aliyehudumia “kwa kadiri ya kipawa cha neema ya Mungu [alichopewa huyo mtume] kwa kadiri ya utendaji wa uweza wake Waefeso 3:7.
Kwa kuwa Paulo aliomba ili aondolewe ‘mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani,’ ni jambo la akili kwamba yeye alimtazamia Bwana Mungu afanye hivyo, Yehova akiwa yule ambaye sala zinaelekezwa kwake. (Wafilipi 4:6; Zaburi 145:18) Zaidi ya hayo, kitia-moyo cha Yehova kwa Paulo kwa maneno haya, “Uweza wangu hutimilika katika udhaifu,” hayamwachi Kristo nje. Huenda nguvu kutoka Bwana Mungu ikaelezwa kama “uweza wa Kristo [uliokuwa kama hema, NW” ukae juu ya Paulo, kwa kuwa ‘Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.’ (1 Wakorintho 1:24) Hivyo, 2 Wakorintho 12:7-9 inatusaidia sisi tuthamini vizuri zaidi njia yenye matokeo ambayo katika hiyo Yehova anatumia Mwana wake katika kutendesha mapenzi yake ya kimungu.
-