Wimbo 51
Kufurahisha Moyo wa Yehova
1. Mungu tumenadhiria
Kufanya mapenzi yako.
Tutafanya kwa hekima
Kukufurahisha moyo.
2. Tusitoke kwako Wewe;
Tumupinge Mushawishi.
Kanuni zako ni njema
Tutazipenda daima.
3. ‘Mutumwako mwaminifu,’
Anatujulisha mema,
Ifaapo atulisha,
Hivyo hututia nguvu.
4. Tupe kani ya ’tendaji
Tushike uaminifu,
Tukupe tunda la sifa,
Tupendeze moyo wako.