Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jitoe Mwenyewe kwa Usomaji
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Mei 15
    • na mpango wa ndoa ya ndugu-mkwe, kupitia Boazi Ruthu amzaa mwana “[kwa] Naomi.” Ruthu awa mzazi wa kale wa Daudi na hatimaye wa Yesu Kristo. Kwa hiyo yeye alipokea “thawabu kamili.” Na zaidi, wale wanaosoma hilo simulizi la Kimaandiko hujifunza somo muhimu: Uwe mwaminifu-mshikamanifu kwa Yehova, na utabarikiwa sana.—Ruthu 2:12; 4:17-22; Mithali 10:22; Mathayo 1:1, 5, 6.

      16. Wale Waebrania watatu walipitia mtihani gani, na simulizi hilo laweza kutusaidiaje?

      16 Simulizi la Waebrania walioitwa Shadraka, Meshaki, na Abednego laweza kutusaidia kuwa waaminifu kwa Mungu katika hali zenye kujaribu. Piga picha akilini tukio hilo wakati Danieli sura ya 3, inaposomwa kwa sauti kubwa. Sanamu kubwa sana ya dhahabu yasimama katika uwanda wa Dura, ambako maofisa Wababilonia walikuwa wamekusanywa. Kwa mlio wa ala za muziki, wao waanguka na kuabudu sanamu ambayo Mfalme Nebukadreza alikuwa amesimamisha. Wote ila Shadraka, Meshaki, na Abednego wafanya hivyo. Kwa staha, lakini kwa uthabiti, wao wamwambia mfalme kwamba hawatatumikia miungu yake na kuabudu ile sanamu ya dhahabu. Waebrania hao wachanga watupwa ndani ya ile tanuri iliyopashwa moto kupita kiasi. Lakini ni nini ambalo latendeka? Akitazama ndani, mfalme aona wanaume wanne wenye nguvu, mmoja wao akiwa “mfano wa mwana wa miungu.” (Danieli 3:25) Wale Waebrania watatu waondolewa kutoka ndani ya tanuri, naye Nebukadreza abariki Mungu wao. Imethawabisha kupiga picha akilini simulizi hilo. Nayo yaandaa somo lililoje kuhusu uaminifu kwa Yehova chini ya jaribu!

      Nufaikeni Kutokana na Kusoma Biblia Mkiwa Familia

      17. Taja kifupi baadhi ya mambo yenye manufaa ambayo familia yako yaweza kujifunza kwa kusoma Biblia pamoja.

      17 Familia yako yaweza kupata manufaa nyingi ikiwa mnatumia wakati kwa ukawaida kusoma Biblia pamoja. Ukianza na Mwanzo, mwaweza kushuhudia uumbaji na kuchungulia makao ya mwanadamu ya Paradiso ya awali. Mnaweza kushiriki mambo waliyoona wazee wa ukoo waaminifu na familia zao na kufuata Waisraeli wavukapo Bahari Nyekundu ikiwa imekauka. Mwaweza kuona kijana mchungaji Daudi akilishinda jitu Mfilisti Goliathi. Familia yako yaweza kuona ujenzi wa hekalu la Yehova katika Yerusalemu, yaweza kuona likifanywa ukiwa na majeshi ya Babiloni, na kuona likijengwa upya chini ya Gavana Zerubabeli. Pamoja na wachungaji wanyenyekevu karibu na Bethlehemu, mwaweza kusikia tangazo la kimalaika la kuzaliwa kwa Yesu. Mwaweza kupata mambo madogo-madogo kuhusu ubatizo na huduma ya Yesu, kumwona akitoa uhai wake wa kibinadamu ukiwa fidia, na kushiriki shangwe ya kufufuliwa kwake. Kisha mwaweza kusafiri pamoja na mtume Paulo na kutazama kuanzishwa kwa makutaniko huku Ukristo ukienea. Kisha, katika kitabu cha Ufunuo, familia yako yaweza kufurahia ono tukufu la mtume Yohana la wakati ujao, kutia ndani Utawala wa Miaka Elfu Moja wa Kristo.

      18, 19. Ni madokezo gani yanayotolewa kuhusu usomaji wa Biblia wa familia?

      18 Ikiwa mnasoma Biblia kwa sauti kubwa mkiwa familia, mwisome kwa uwazi na kwa idili. Mnaposoma sehemu fulani za Maandiko, mshiriki mmoja wa familia—labda baba—huenda akasoma maneno ya usimulizi. Wengine wenu mwaweza kuchukua sehemu za wahusika wa Biblia, mkisoma sehemu zenu kwa hisia zifaazo.

      19 Mnaposhiriki katika usomaji wa Biblia mkiwa familia, uwezo wenu wa kusoma waweza kuboreka. Yaelekea, ujuzi wenu juu ya Mungu utaongezeka, na hilo lapaswa kuwavuta karibu naye zaidi. Asafu aliimba: “Nami kumkaribia Mungu ni kwema kwangu; nimefanya kimbilio kwa Bwana MUNGU, niyahubiri matendo yako yote.” (Zaburi 73:28) Hili litasaidia familia yako kuwa kama Musa, ambaye “alistahimili kama amwonaye yeye asiyeonekana,” yaani, Yehova Mungu.—Waebrania 11:27.

      Kusoma na Huduma ya Kikristo

      20, 21. Utume wetu wa kuhubiri unahusianaje na uwezo wa kusoma?

      20 Tamaa yetu ya kumwabudu “yeye asiyeonekana” yapaswa kutusukuma kufanyia kazi kuwa wasomaji wazuri. Uwezo wa kusoma vizuri hutusaidia kutoa ushahidi kutoka kwa Neno la Mungu. Kwa hakika hutusaidia kuendelea katika kazi ya kuhubiri juu ya Ufalme ambayo Yesu aliagiza wafuasi wake kuihusu aliposema hivi: “Enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi.” (Mathayo 28:19, 20; Matendo 1:8) Kutoa ushahidi ndiyo kazi kuu ya watu wa Yehova, na uwezo wa kusoma hutusaidia kuitimiza.

      21 Jitihada inahitajika ili kuwa msomaji mzuri na mwalimu stadi wa Neno la Mungu. (Waefeso 6:17) Basi, ‘jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, ukitumia kwa halali neno la kweli.’ (2 Timotheo 2:15) Ongeza ujuzi wako wa kweli ya Kimaandiko na uwezo wako ukiwa Shahidi wa Yehova kwa kujitoa mwenyewe kwa usomaji.

  • Soma Neno la Mungu na Umtumikie Katika Kweli
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Mei 15
    • Soma Neno la Mungu na Umtumikie Katika Kweli

      “Ee BWANA, unifundishe njia yako; nitakwenda katika kweli yako.”—ZABURI 86:11.

      1. Toleo la kwanza la gazeti hili lilisema nini hasa kuhusu kweli?

      YEHOVA hutoa nuru na kweli. (Zaburi 43:3) Yeye hutupa pia uwezo wa kusoma Neno lake, Biblia, na kujifunza kweli. Toleo la kwanza la jarida hili—Julai 1879—lilisema: “Kweli, kama ua dogo kati ya mimea mingi sana, imezungukwa na hata karibu kusongwa na usitawi mwingi wa magugu ya makosa. Ili uipate ni lazima uwe macho wakati wote. Ili uone umaridadi wayo ni lazima uondoe magugu ya makosa na michongoma ya ushupavu. Ili uipate ni lazima uiname kuichukua. Usiridhike na ua moja la kweli. Kama ua moja la kweli lingalitosha kusingalikuwa na mengine. Endelea kukusanya, tafuta mengine zaidi.” Kusoma na kujifunza Neno la Mungu hutuwezesha kupata ujuzi sahihi na kutembea katika kweli yake.—Zaburi 86:11.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki