Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Wewe Ni Rafiki ya Mungu?—kinachofunuliwa na sala zako
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Julai 1
    • katika hicho, kwa sababu Mungu ni mkubwa zaidi kuliko mioyo yetu na ajua mambo yote.”

      Hata hivyo, hatuhitaji kuwa katika hali ngumu, ili kufurahia hangaiko la Mungu lenye upendo. Yehova hupendezwa na chochote kiwezacho kuathiri hali njema yetu ya kiroho na ya kihisia-moyo. Ndiyo, hatuhitaji kamwe kufikiri kwamba hisia zetu, mawazo yetu, na mahangaiko yetu ni yasiyo ya maana sana yasiweze kutajwa katika sala. (Wafilipi 4:6) Unapokuwa na rafiki wa karibu, je, nyinyi huzungumza juu ya matukio makuu tu maishani mwenu? Je, hamshiriki pia mahangaiko madogo kwa kadiri? Katika njia sawa na hiyo, waweza kujihisi huru kuzungumza juu ya sehemu yoyote ya maisha yako pamoja na Yehova, ukijua kwamba ‘yeye hukujali wewe.’—1 Petro 5:7.

      Bila shaka, yaelekea urafiki hautadumu muda mrefu ikiwa yote unayozungumza ni juu yako mwenyewe. Hali kadhalika, sala zetu hazipaswi kuwa zenye ubinafsi. Twapaswa kutaja pia upendo wetu na hangaiko letu kwa Yehova na mapendezi yake. (Mathayo 6:9, 10) Sala si fursa ya kuomba msaada kutoka kwa Mungu tu bali pia ni nafasi ya kutoa shukrani na sifa. (Zaburi 34:1; 95:2) “Kuendelea kutwaa ujuzi” kupitia funzo la kawaida la kibinafsi kutatusaidia katika jambo hilo, kwa kuwa hilo hutusaidia kufahamiana zaidi na Yehova na njia zake. (Yohana 17:3) Huenda ukapata kwamba ni jambo lenye kusaidia hasa kusoma kitabu cha Zaburi na kuona jinsi watumishi wengine waaminifu walivyojieleza wenyewe kwa Yehova.

      Urafiki wa Yehova kwa kweli ni zawadi yenye thamani. Na tuonyeshe kwamba tunauthamini kwa kufanya sala zetu ziwe za ukaribu, zenye kuhisiwa moyoni, na za kibinafsi hata zaidi. Ndipo tutakaposhiriki furaha iliyoonyeshwa na mtunga-zaburi, aliyetangaza hivi: “Heri mtu yule umchaguaye, na kumkaribisha.”—Zaburi 65:4.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Julai 1
    • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

      Tulisisimuliwa na funzo letu la mfano wa Yesu wenye somo wa kondoo na mbuzi. Kwa kufikiria uelewevu mpya uliotolewa katika “Mnara wa Mlinzi” la Oktoba 15, 1995, je, twaweza bado kusema kwamba Mashahidi wa Yehova wangali wakishiriki katika kazi ya kutenganisha leo?

      Ndiyo. Kwa kueleweka, wengi wamejiuliza juu ya hili kwa sababu Mathayo 25:31, 32, husema: “Wakati Mwana wa binadamu awasilipo katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu. Na mataifa yote yatakusanywa mbele yake, naye atatenganisha watu mmoja na mwenzake, kama vile mchungaji atenganishavyo kondoo na mbuzi.” Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 1995, lilionyesha ni kwa nini mistari hiyo itatumika baada ya dhiki kubwa kuanza. Yesu atawasili katika utukufu pamoja na malaika wake na ataketi juu ya kiti chake cha ufalme cha hukumu. Kisha, atawatenganisha watu. Katika maana gani? Atatoa maamuzi yatakayotegemea yale ambayo watu walifanya au hawakufanya kabla ya wakati huo.

      Twaweza kulinganisha hilo na hatua za utaratibu wa kisheria zinazoongoza kwenye kesi ya mahakama. Uthibitisho wakusanyika kwa kipindi kirefu cha wakati kabla ya mahakama kutoa uamuzi na hukumu. Uthibitisho wa ikiwa watu wanaoishi sasa watakuwa kondoo au mbuzi umekuwa ukikusanyika kwa muda mrefu. Na bado waongezeka. Lakini Yesu aketipo juu ya kiti chake cha ufalme, kesi itakuwa imekamilika. Atakuwa tayari kutoa hukumu. Watu watatenganishwa ama kwenye kukatiliwa-mbali kudumuko milele ama kwenye uhai udumuo milele.

      Hata hivyo, uhakika wa kwamba kutenganishwa kwa watu kwenye uhai au kwenye kifo kunakotajwa kwenye Mathayo 25:32 kungali mbele haumaanishi kwamba hakuna kutenganisha, au kugawanya, kunakotukia kabla ya huko. Katika Mathayo sura ya 13, Biblia yataja kazi moja ya kutenganisha inayotukia mapema zaidi. Kwa kupendeza, kitabu Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli, ukurasa wa 180, chashughulikia hilo chini ya kichwa “Kutenganishwa kwa Watu.”a Hicho kitabu chasema hivi: “Pia kuna matukio ya maana mengine ambayo Yesu alihusisha waziwazi na umalizio wa mfumo wa mambo. Moja la hayo ni kutenganishwa kwa ‘wana wa ufalme’ kutoka ‘wana wa yule mwovu.’ Yesu alisema juu ya hilo katika mfano wake juu ya shamba la ngano ambalo adui alipanda magugu kwa wingi.”

      Hicho kitabu kilikuwa kikirejezea mfano wenye somo wa Yesu ulio kwenye Mathayo 13:24-30 na kufafanuliwa katika mstari wa 36-43. Ona katika mstari wa 38 kwamba zile mbegu nzuri za ngano zafananisha wana wa Ufalme, lakini magugu yanawakilisha wana wa yule mwovu. Mstari wa 39 na wa 40 waonyesha kwamba katika “umalizio wa mfumo wa mambo”—wakati tunamoishi sasa—magugu yanakusanywa. Yanatenganishwa na hatimaye yanachomwa, yanaharibiwa.

      Kielezi hicho chashughulika na Wakristo watiwa-mafuta (ambao katika mfano wenye somo wa kondoo na mbuzi wanaitwa ndugu za Yesu). Hata hivyo, hoja iko wazi kwamba kutenganishwa kwa maana kwatukia katika wakati wetu, watiwa-mafuta wakitofautishwa na wanaodai kuwa Wakristo lakini wale ambao wanajithibitisha kuwa “wana wa yule mwovu.”

      Yesu aliandaa vielelezo vingine vya watu kugawanywa, au kutenganishwa. Kumbuka kwamba alisema hivi kuhusu ile barabara pana inayoongoza kwenye uharibifu: “Wengi ndio wanaoingia kupitia hiyo.” (Mathayo 7:13) Hilo halikuwa elezo tu juu ya tokeo la mwisho. Lilikuwa elezo juu ya jambo lenye kuendelea, kama ilivyo kweli leo kuhusu wachache wanaoipata barabara yenye kufinyana inayoongoza kuingia katika uhai. Pia, kumbuka kwamba alipokuwa akiwatuma mitume wake, Yesu alisema kwamba wangepata watu fulani ambao wangestahili. Wengine wasingestahili, nao mitume walipaswa kuyakung’uta mavumbi kutoka kwenye miguu yao “ili kuwa ushahidi dhidi ya” watu hao. (Luka 9:5) Je, si kweli kwamba jambo kama hilo hutukia Wakristo waendelezapo huduma yao ya hadharani leo? Watu fulani huitikia vizuri, ilhali wengine hukataa ujumbe wa kimungu tunaoleta.

      Makala katika Mnara wa Mlinzi hilo zilizoshughulika na mbuzi na kondoo zilieleza hivi: “Ingawa kule kuhukumu kama kunavyofafanuliwa katika huu mfano kuko karibu sana, hata sasa jambo muhimu linatukia. Sisi Wakristo tunashiriki katika kazi ya kuokoa uhai ya kutangaza ujumbe unaotokeza mgawanyiko kati ya watu. (Mathayo 10:32-39).” Katika fungu hilo la maneno katika Mathayo sura ya 10, twasoma kwamba Yesu alisema kwamba kumfuata kungesababisha mgawanyiko—baba dhidi ya mwana, binti dhidi ya mama.

      Hatimaye, ndugu za Kristo watiwa-mafuta kwa roho wameongoza kuhubiriwa kwa ujumbe wa Ufalme ulimwenguni pote. Watu wausikiapo na kuitikia kwa kupendezwa au kwa kutopendezwa, wanajitambulisha wenyewe. Sisi wanadamu hatuwezi, na hatupaswi, kusema, ‘Mtu huyu ni kondoo; yule ni mbuzi,’ katika maana iwasilishwayo katika Mathayo sura ya 25. Hata hivyo, kujulisha kwetu watu habari njema huwaruhusu kuonyesha msimamo wao—ni watu wa aina gani na wanawaitikiaje ndugu za Yesu. Kwa sababu hiyo, sawa na uthibitisho wenye kuongezeka wa kesi ya mahakamani, mgawanyo kati ya wale wanaotegemeza ndugu za Yesu na wale wanaokataa kuwategemeza waanza kuwa dhahiri. (Malaki 3:18) Kama Mnara wa Mlinzi lilivyoonyesha, karibuni Yesu ataketi kwenye kiti chake cha ufalme na kutangaza hukumu, ndipo watu watakapotenganishwa kihukumu katika maana ya mwisho kwenye uhai au kwenye kukatiliwa-mbali.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki