-
UbatizoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
atayateketeza kwa moto usioweza kuzimwa.” (Uharibifu wa makapi hayo utakuwa wa milele.)
Mt. 13:49, 50: “Hivyo ndivyo itakavyokuwa katika umalizio wa mfumo wa mambo: malaika watatoka kwenda na kuwatenga waovu kutoka katikati ya waadilifu nao watawatupa ndani ya tanuru ya moto.”
Luka 17:29, 30: “Siku ambayo Loti alitoka Sodoma kulinyesha moto na kiberiti kutoka mbinguni na kuwaangamiza wote. Itakuwa vivyo hivyo siku ile ambayo Mwana wa binadamu atafunuliwa.”
Si sawa na ubatizo kwa roho takatifu, uliokuwa wa wanafunzi
Mdo. 1:5: “Yohana, kwa kweli, alibatiza kwa maji, lakini ninyi [mitume waaminifu wa Yesu] mtabatizwa kwa roho takatifu siku chache baadaye.”
Mdo. 2:2-4: “Ghafula kukatokea kutoka mbinguni kelele kama ile ya upepo wenye nguvu unaovuma, nao ukaijaza nyumba yote ambamo walikuwa wameketi. Nao wakaona ndimi kama za moto, nazo zikagawanyika huku na huku, na mmoja ukaketi juu ya [lakini haukumfunika au kumzamisha] kila mmoja wao, nao wote wakajazwa roho takatifu wakaanza kusema katika lugha tofauti, kama vile roho ilivyokuwa ikiwawezesha kusema.”
-
-
UfalmeKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Ufalme
Maana: Ufalme wa Mungu huwakilisha enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu wote kuelekea viumbe wake, au njia anayoitumia kuonyesha enzi hiyo. Neno hili linatumiwa hasa kurejelea enzi kuu ya Mungu kupitia serikali inayoongozwa na Mwana wake, Yesu Kristo. Neno “ufalme” linaweza kurejelea utawala wa yule aliyetiwa mafuta awe Mfalme, au linaweza kurejelea dunia inayotawaliwa na serikali hiyo ya mbinguni.
Je, Ufalme wa Mungu ni serikali halisi?
Au ni hali iliyo katika mioyo ya wanadamu?
Luka 17:21, UV: “Wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama ufalme wa Mungu umo ndani yenu [pia ZSB, NAJ; lakini “kati yenu,” BHN, VB; “katikati yenu,” NW].” (Ona kwamba, kama vile mstari wa 20 unavyoonyesha, Yesu alikuwa akizungumza na Mafarisayo, ambao pia aliwashutumu kuwa wanafiki, kwa hiyo, hangeweza kumaanisha kwamba Ufalme ulikuwa katika mioyo yao. Lakini Ufalme kama unavyowakilishwa na Kristo ulikuwa katikati yao.)
Je, kweli Biblia inasema kwamba Ufalme wa Mungu ni serikali?
Isa. 9:6, 7, UV: “Kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme [“mamlaka ya kutawala,” BHN; “utawala,” NW, ZSB] utakuwa begani mwake; naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani hayatakuwa na mwisho kamwe.”
Watawala wa Ufalme huo ni nani?
Ufu. 15:3: “Matendo yako ni makuu na ya ajabu, Yehova Mungu, Mweza-Yote. Njia zako ni za uadilifu na za kweli, Mfalme wa umilele.”
Dan. 7:13, 14: “Mtu fulani kama mwana wa binadamu [Yesu Kristo; ona Marko 14:61, 62] alikuwa anakuja na mawingu ya mbingu; naye akaja kwa Mzee wa Siku [Yehova Mungu], nao wakamleta karibu mbele zake Yule. Naye [Yesu Kristo] akapewa utawala na heshima na ufalme, ili vikundi vyote vya watu, vya mataifa na lugha vimtumikie yeye.”
Ufu. 5:9, 10; 14:1-3: “[Wewe Yesu Kristo] ulichinjwa na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu kutoka katika kila kabila na lugha na watu na taifa, nawe ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, nao watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia.” (Katika Ufunuo 14:1-3, hao ambao “wamenunuliwa kutoka duniani” wakatawale pamoja na Mwana-Kondoo juu ya Mlima Sayuni wa mbinguni wanatajwa kuwa watu 144,000.)
Ufalme huo utazitendeaje serikali za wanadamu?
Dan. 2:44: “Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo.”
Zab. 2:8, 9: “Niombe, ili nikupe mataifa yawe urithi wako na miisho ya dunia iwe miliki yako mwenyewe. Utawavunja kwa fimbo ya chuma ya enzi, utawavunja vipande-vipande, kama chombo cha mfinyanzi.”
Ufalme wa Mungu utatimiza nini?
Kutakasa jina la Yehova na kutegemeza enzi yake kuu
Mt. 6:9, 10: “Basi, ninyi msali hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. Ufalme wako na uje.’” (Hapa kutakaswa kwa jina la Mungu kunahusianishwa na kuja kwa ufalme wake.)
Eze. 38:23: “Nami hakika nitajitukuza mwenyewe na kujitakasa mwenyewe na kujijulisha mwenyewe mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” (Jina la Mungu litaondolewa lawama zote; litaonwa kuwa takatifu na lenye kustahili heshima, na wote wanaoishi watakuwa watu wanaotegemeza enzi kuu ya Yehova kwa hiari, wanaopenda kufanya mapenzi yake. Amani na hali njema ya ulimwengu wote inategemea kutakaswa huko kwa jina la Yehova.)
Kuukomesha utawala wa Shetani ulimwenguni
Ufu. 20:2, 3: “Naye [Mfalme wa mbinguni, Yesu Kristo] akamkamata yule joka mkubwa, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, na kumfunga kwa miaka elfu. Naye akamtupa ndani ya abiso na kuifunga na kuitia muhuri juu yake, ili asipotoshe mataifa tena mpaka ile miaka elfu itakapokwisha. Baada ya mambo hayo yeye atafunguliwa kwa muda kidogo.” (Kwa hiyo, wanadamu watawekwa huru kutokana na uvutano wa Shetani ambao umefanya maisha yawe magumu sana kwa watu wanaotaka kufanya yaliyo sawa. Uvutano wa kishetani ambao umesababisha ukatili wenye kupita kiasi na uvutano wa roho waovu ambao umefanya watu wengi waishi kwa woga, utatoweka.)
Kuunganisha uumbaji wote umwabudu Mungu wa pekee wa kweli
Ufu. 5:13; 15:3, 4: “Na kila kiumbe kilicho mbinguni na juu ya dunia na chini ya dunia na juu ya bahari, na vitu vyote vilivyo ndani ya hivyo, nikasikia vikisema: ‘Kwake Yule anayeketi juu ya kile kiti cha ufalme [Yehova Mungu] na kwa Mwana-Kondoo [Yesu Kristo] kuwe na baraka na heshima na utukufu na nguvu milele na milele.’” “Matendo yako ni makuu na ya ajabu, Yehova Mungu, Mweza-Yote. Njia zako ni za uadilifu na za kweli, Mfalme wa umilele. Ni nani ambaye kwa kweli hatakuogopa wewe, Yehova, na kulitukuza jina lako, kwa sababu wewe peke yako ni mshikamanifu? Kwa maana mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa sababu amri zako za uadilifu zimefunuliwa.”
Kuwapatanisha tena wanadamu pamoja na Mungu
Rom. 8:19-21: “Uumbaji [wanadamu] unangojea na kutazamia kwa hamu kufunuliwa kwa wana wa Mungu [uthibitisho wa kwamba wale watakaofufuliwa ili waishi mbinguni pamoja na Yesu Kristo wameanza kutawala]. Kwa maana uumbaji ulitiishwa chini ya ubatili, si kwa mapenzi yake wenyewe bali kupitia yeye aliyeutiisha hivyo, juu ya msingi wa tumaini kwamba uumbaji wenyewe [wanadamu kwa ujumla] pia utawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu na kuwa na uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.”
Kuwaweka huru wanadamu kutokana na matisho yote ya vita
Zab. 46:8, 9: “Njooni, tazameni matendo ya Yehova, jinsi ambavyo ameweka matukio ya kushangaza duniani. Anakomesha vita mpaka kwenye mwisho wa dunia.”
Isa. 2:4: “Watafua panga zao ziwe majembe na mikuki yao iwe miundu. Taifa halitainua upanga juu ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.”
Kuwaondoa watawala wafisadi na wakandamizaji duniani
Zab. 110:5: “Yehova mwenyewe akiwa upande wako wa mkono wa kuume hakika atawavunja vipande-vipande wafalme katika siku ya hasira yake.”
Zab. 72:12-14: “[Masihi, Mfalme aliyewekwa na Yehova] atamkomboa maskini anayelilia msaada, pia mwenye kuteseka na yeyote ambaye hana msaidizi. Atamsikitikia mtu wa hali ya chini na maskini, naye ataziokoa nafsi za maskini. Ataikomboa nafsi yao kutoka katika ukandamizaji na katika jeuri, nayo damu yao itakuwa na thamani machoni pake.”
Kuwaandalia wanadamu wote chakula kingi
Zab. 72:16: “Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani; juu ya milima kutakuwa na mafuriko.”
Isa. 25:6: “Yehova wa majeshi hakika atavifanyia vikundi vyote vya watu, katika mlima huu [katika Mlima Sayuni wa mbinguni, kiti cha Ufalme wa Mungu, raia wake wataandaliwa mahitaji], karamu ya vyakula vinono vilivyotiwa mafuta, karamu ya divai iliyowekwa kwenye machicha, ya vyakula vinono vilivyotiwa mafuta vilivyojazwa urojorojo, ya divai iliyowekwa kwenye machicha, iliyochujwa.”
Kuondoa magonjwa na ulemavu wa aina zote
Luka 7:22; 9:11: “Nendeni, mkamwambie Yohana yale mliyoona na kusikia: vipofu wanaona, vilema wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa na viziwi wanasikia, na wafu wanafufuliwa, maskini wanaambiwa ile habari njema.” “Naye [Yesu Kristo] akawapokea kwa fadhili na kuanza kuwaambia juu ya ufalme wa Mungu, naye akawaponya wale wanaohitaji kuponywa.” (Kwa njia hiyo, Yesu aliyaonyesha yale ambayo atawatendea wanadamu akiwa Mfalme mbinguni.)
Kuwaandalia watu wote nyumba nzuri
Isa. 65:21, 22: “Hakika wao watajenga nyumba na kukaa ndani yake; na hakika wao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. Hawatajenga na mtu mwingine akae ndani yake; hawatapanda na mtu mwingine ale.”
Kuhakikisha wote wana kazi yenye kuridhisha
Isa. 65:23: “Hawatafanya kazi ya bure, wala hawatazaa kwa ajili ya kupata usumbufu; kwa sababu wao ni uzao wa watu wa Yehova waliobarikiwa, na wazao wao pamoja nao.”
Kuhakikisha kuna usalama kwa mtu na mali zake
Mika 4:4: “Nao wataketi, kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, wala hakutakuwa na mtu yeyote anayewatetemesha; kwa maana kinywa cha Yehova wa majeshi kimesema hivyo.”
Zab. 37:10, 11: “Bado muda kidogo tu, na mtu mwovu hatakuwako tena; nawe hakika utapaangalia mahali pake,
-