Wimbo 152
Kuthamini Huruma za Mungu
1. Mali, ujuzi, hekima
Mungu Bwana zi kwake!
Lo! hazitafutikani
Hukumu, njia zake!
Nani amemushauri,
Kumupa musaada,
Hata adaiwe nasi
Au kwamba tulipwe?
2. Kwa huruma za Yehova
Tumushukuru yeye,
Miili yetu tutoe
Kwa Mungu mwadilifu.
Wakifu tukawa sisi,
Tufanye upasavyo,
Kwa nguvu za kufikiri
Tutende tuwezayo.
3. Tuache uulimwengu,
Akili ziwe mupya
Kwa kweli igeuzayo
Tujawe na imani.
Baraka tuombe Mungu,
Tuwe wa kujishusha,
Na hivyo, tukipendana;
Tutapata amani.