-
Matangulizi ya Kutumia Katika Huduma ya ShambaniKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
● ‘Habari. Jina langu ni ——. Kusudi langu la kuja hapa ni kuongea nawe baraka za Ufalme wa Mungu na jinsi tunavyoweza kuzipata. Lakini naona kwamba una shughuli nyingi (au, unataka kuondoka). Je, nikueleze jambo fupi tu?’
KATIKA ENEO LINALOHUBIRIWA MARA NYINGI
● ‘Nimefurahi kukukuta nyumbani. Tunafanya ziara ya kila juma katika mtaa huu, nasi tuna jambo zaidi la kushiriki pamoja nawe kuhusu mambo mazuri ajabu ambayo Ufalme wa Mungu utawafanyia wanadamu.’
● ‘Hujambo. Nimefurahi kukuona tena. . . . Je, kila mtu nyumbani ni mzima? . . . Nimepitia kidogo hapa ili nishiriki pamoja nawe wazo fulani kuhusu . . . ’
● ‘Habari ya asubuhi. . . . Nimekuwa nikitafuta nafasi nyingine ya kuongea na wewe. (Kisha taja jambo hususa unalotaka kuzungumzia.)’
-
-
Jinsi Unavyoweza Kujibu Vizuia-Mazungumzo VikitokeaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Jinsi Unavyoweza Kujibu Vizuia-Mazungumzo Vikitokea
Maelezo: Matarajio ya watu ya uzima hutegemea mtazamo wao kwa Yehova Mungu na Ufalme wake mikononi mwa Kristo Yesu. Ujumbe wa Ufalme wa Mungu unavutia, nao unaelekeza kwenye tumaini pekee linalotegemeka kwa ajili ya wanadamu. Ni ujumbe unaobadili maisha. Tunataka kila mtu ausikie. Tunafahamu kwamba ni wachache tu watakaoupokea na kuuthamini, lakini tunajua kwamba angalau watu wanahitaji kuusikia ili wafanye uchaguzi wa jambo wanalojua. Hata hivyo, si kila mtu aliye tayari kusikiliza, nasi hatujaribu kumlazimisha. Lakini tukiwa na utambuzi mara nyingi inawezekana kuvigeuza vizuia-mazungumzo viwe nafasi za mazungumzo zaidi. Hii ni mifano ambayo baadhi ya Mashahidi wenye uzoefu wametumia wakijitahidi kutafuta wanaostahili. (Mt. 10:11) Hatupendekezi kwamba ukariri moyoni lolote la majibu haya bali uweke wazo akilini, ulitie katika maneno yako mwenyewe na kulieleza kwa njia inayoonyesha kwamba unapendezwa kikweli na mtu unayesema naye. Unapofanya hivyo, unaweza kuwa na uhakika kwamba wale ambao mioyo yao ina mwelekeo unaofaa watasikiliza na kuthamini yale ambayo Yehova anafanya ili kuwavuta kwenye maandalizi yake ya upendo ya kupata uzima.—Yoh. 6:44; Mdo. 16:14.
‘MIMI SIPENDEZWI’
● ‘Hebu nikuulize, Unamaanisha kwamba hupendezwi na Biblia, au hupendezwi na dini kwa ujumla? Nauliza hivyo kwa sababu tumekutana na watu wengi ambao wakati mmoja walikuwa watu wa dini lakini hawaendi tena kanisani kwa sababu wanaona unafiki mwingi katika makanisa (au, wanaona kwamba dini ni biashara tu; au, hawaoni inafaa dini kujiingiza katika siasa; n.k.). Biblia pia haikubali matendo hayo, nayo huandaa msingi pekee unaotuwezesha kuutazamia wakati ujao tukiwa na uhakika.’
● ‘Ikiwa unamaanisha kwamba hupendezwi na dini nyingine, ninaelewa hilo. Lakini inaelekea unapendezwa na wakati ujao tunaoweza kutazamia kwa sababu ya hatari ya vita vya nyukilia (au, jinsi tunavyoweza kuwalinda watoto wetu ili wasitumie vibaya dawa za kulevya; au linaloweza kufanywa kuhusu uhalifu ili tusiogope kutembea barabarani; n.k.). Je, unaona kuna tarajio lolote la kupata utatuzi wa kweli?’
● ‘Je, ni kwa sababu tayari una dini . . . Hebu niambie, Je, unafikiri kuna wakati ambapo watu wote watakuwa katika dini moja? . . . Ni nini kinachozuia jambo hilo lisitendeke? . . . Ili hilo lifaulu, ni msingi gani unaohitajiwa?’
● ‘Ninaweza kuelewa jambo hilo. Miaka michache iliyopita nilikuwa na maoni kama hayo. Lakini nilisoma jambo fulani katika Biblia lililonisaidia niwe na maoni tofauti. (Mwonyeshe mtu huyo lilikuwa nini.)’
● ‘Ungependa nikuonyeshe katika Biblia jinsi unavyoweza kuwaona tena wapendwa wako waliokufa (au, kusudi la kweli la maisha; au, jinsi inavyoweza kutusaidia kuziunganisha familia zetu; n.k.)?’
● ‘Ikiwa unamaanisha kwamba hupendi kununua kitu, hebu nikutulize akili. Mimi sifanyi biashara. Lakini je, unapenda kuwa na nafasi ya kuishi katika paradiso duniani, bila magonjwa na uhalifu, ukiwa na jirani wanaokupenda kwelikweli?’
● ‘Je, wewe hujibu hivyo sikuzote Mashahidi wa Yehova wanapokutembelea? . . . Je, umewahi kujiuliza kwa nini tunaendelea kuwatembelea watu au jambo tunalotaka kusema? . . . Kwa ufupi, sababu ya kuja kukuona ni kwamba ninajua jambo fulani ambalo wewe unapaswa kulijua pia. Kwa nini usisikilize mara hii tu?’
‘SIPENDEZWI NA DINI’
● ‘Ninaelewa maoni yako. Kusema kweli, makanisa hayaufanyi ulimwengu huu kuwa mahali salama zaidi pa kuishi, sivyo? . . . Hebu nikuulize, Umekuwa na maoni hayo sikuzote? . . . Lakini unamwamini Mungu?’
-