-
RohoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Mungu. Ili kupata maelezo zaidi kuhusu ‘roho ambayo humrudia Mungu,’ ona ukurasa wa 224, 225, chini ya kichwa “Nafsi.”)
Mtu Akisema—
‘Je, una roho takatifu?’
Unaweza kujibu hivi: ‘Ndiyo, na ndiyo sababu nimekuja kukutembelea leo. (Mdo. 2:17, 18)’
Au unaweza kusema: ‘Hiyo ndiyo inayoniwezesha kushiriki huduma ya Kikristo. Lakini nimeona kwamba watu wana maoni yanayotofautiana kuhusu kile kinachoonyesha kwamba mtu kweli ana roho ya Mungu. Wewe unaangalia mambo gani?’ Kisha unaweza kuongezea: (Zungumzia baadhi ya habari zilizo katika ukurasa wa 243, 244.)
-
-
Roho ya UlimwenguKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Roho ya Ulimwengu
Maana: Nguvu zinazowachochea wanadamu ambao si watumishi wa Yehova Mungu, zikiwafanya watu hao waseme na kutenda mambo kulingana na tabia fulani ya kawaida. Ijapokuwa watu hutenda kulingana na mapendezi yao binafsi, wale walio na roho ya ulimwengu wana maelekeo fulani ya msingi, njia za kutenda mambo, na miradi maishani ambayo ni kawaida ya mfumo wa mambo uliopo ambao mungu na mtawala wake ni Shetani.
Kwa nini mtu anapaswa kuhangaikia kwa uzito asitiwe uchafu na roho ya ulimwengu?
1 Yoh. 5:19: “Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.” (Shetani amesitawisha roho inayotawala fikira na shughuli za wanadamu ambao si watumishi waliokubaliwa wa Yehova. Ni roho ya ubinafsi na kiburi ambayo imeenea sana hivi kwamba ni kama hewa ambayo wanadamu wanapumua. Tunahitaji kuwa waangalifu sana ili tusijiweke chini ya mamlaka ya Shetani kwa kuruhusu roho hiyo iongoze maisha yetu.)
Ufu. 12:9: “Yule joka mkubwa akatupwa chini, yule nyoka wa zamani, yeye anayeitwa Ibilisi na Shetani, anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa; akatupwa chini duniani,
-