Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 6/15 uku. 32
  • Alimtumikia Yehova kwa Unyenyekevu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Alimtumikia Yehova kwa Unyenyekevu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 6/15 uku. 32

Alimtumikia Yehova kwa Unyenyekevu

“LA MAANA si mahali utumikapo bali yule umtumikiaye.” John Booth alipenda sana kusema maneno hayo, naye aliishi kwa kupatana nayo. Mwendo wake wa maisha duniani, ulioisha Jumatatu, Januari 8, 1996, haukuacha shaka lolote juu ya ni nani aliyechagua kumtumikia.

Akiwa kijana huko nyuma katika 1921, John Booth alikuwa akitafuta kusudi maishani. Alifundisha shule ya Jumapili kwenye Dutch Reformed Church, lakini alikinza wazo la kuzoezwa kuwa wahudumu kwa kuwa alihisi kwamba makasisi waliishi maisha ya ubinafsi. Alipoona kikaratasi cha kutangazia hotuba yenye kichwa “Mamilioni Wanaoishi Sasa Hawatakufa Kamwe,” bila kupoteza wakati aliomba fasihi zilizotangazwa nacho. Akivutiwa na yale aliyokuwa amesoma, upesi akaanza kwenda kwenye mikutano ya Wanafunzi wa Biblia, kama vile Mashahidi wa Yehova walivyojulikana wakati huo, akiendesha baiskeli yake mwendo wa kilometa 24. Alibatizwa katika 1923, akaanza kuhubiri mlango hadi mlango katika eneo la Wallkill, New York, ambako familia yake ilikuwa na shamba la ng’ombe wa maziwa.

Ndugu Booth aliingia katika huduma ya wakati wote Aprili 1928. Alihubiri katika eneo la nyumbani kwake na mashambani Kusini, akibadilishana fasihi za Biblia na chakula na malazi. Alilazimika kukabili hatari mbalimbali zilizotia ndani wenye nyumba za kufanyizia alkoholi haramu, waliowatisha kwa bunduki, mmoja wao alimpiga risasi na kumjeruhi painia-mwenzi wa John Booth. Katika 1935, Ndugu Booth aliwekwa rasmi kuwa mwangalizi asafiriye, akaanza kutembelea makutaniko na vikundi vidogo-vidogo nchini. Alitayarisha makusanyiko na kusaidia ndugu na dada wastahimili licha ya upinzani. Kukabili ghasia za watu wenye hasira, kuchukua msimamo mahakamani, na kufungwa gerezani, yote yakawa mambo ya kawaida kwa Ndugu Booth. “Kitabu kingehitajiwa ili kueleza mambo yote ya nyakati hizo zenye kusisimua,” akaandika wakati mmoja.

Katika 1941, Joseph F. Rutherford, aliyekuwa msimamizi wa Watch Tower Society wa wakati huo, alimpa Ndugu Booth mgawo wa kufanya kazi kwenye Shamba la Ufalme, karibu na Ithaca, New York. Huku alitumikia kwa uaminifu kwa miaka 28. Kupenda kwake huduma kukiwa hakujazimika, alifurahi kwa miaka kadhaa kushirikiana na maelfu ya wanafunzi wa Shule ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower ya kuzoeza wamishonari, iliyokuwa huko katika Shamba la Ufalme hadi 1961. Katika 1970, Ndugu Booth aliombwa atumikie katika Mashamba ya Watchtower katika Wallkill, New York, na hivyo akajikuta akiwa katika eneo lilelile aliloanzia kupainia miaka 45 hivi mapema.

Katika 1974, Ndugu Booth aliwekwa rasmi kuwa mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova katika Brooklyn, New York. Alitumikia kwa uaminifu katika wadhifa huo hadi kifo chake akiwa na umri wa miaka 93. John Booth alipendwa kwa sababu ya utu wake wa Kikristo wa unyenyekevu na fadhili zenye kina. Hadi afya na nguvu zake zilipomwishia, alikuwa akihubiri kwa uaminifu mlango hadi mlango na kwenye barabara za jiji.

Ingawa wale waliotumikia pamoja naye wanaomboleza kufa kwake, wanapata faraja katika ahadi ya Biblia kuhusu Wakristo watiwa-mafuta kama yeye, kwamba wanafufuliwa kwenye uhai wa kimbingu na kwamba “matendo yao yafuatana nao.” (Ufunuo 14:13; 1 Wakorintho 15:51-54) Bila shaka mbingu ni mazingira mapya, walakini ambamo John Booth ataweza kumtumikia Yehova milele!

[Picha katika ukurasa wa 32]

John Booth 1903-1996

[Picha katika ukurasa wa 32]

HERALD-AMERICAN, ANDOVER 1234

76 Jehovites Jailed in Joliet

[Hisani]

Chicago Herald-American

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki